Maswali kwa Twaweza (By MCL)

Maswali kwa Twaweza (By MCL)

Maswali 14 yaliyoibuliwa na tafiti ya Twaweza

1. Kwa mara ya kwanza Twaweza walisoma ripoti ya utafiti na kuonyeshwa moja kwa moja na TV. Nani alidhamini utafiti, matangazo hayo na kwa madhumuni gani?

2. Kwa nini waliamua kutoa matokeo ya utafiti wao katikati ya kampeni zenye ushindani mkali na mhemko mkubwa wa kisiasa?

3. Je, ni jinsi gani watu waliohojiwa walichaguliwa?

4. Je, watu waliohojiwa ni wa kutoka maeneo gani, makundi gani ya watu, ukiacha jinsia?

5. Je, waliohojiwa wamejiandikisha kupiga kura, mashabiki tu au mchanganyiko?

6. Twaweza wanajua kwamba kampeni za wagombea urais huanza baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuidhinisha wagombea waliopendekezwa na vyama. Kwa nini shirika hilo lilianza kufanya utafiti siku mbili kabla ya hapo?

7. Twaweza wanasema wahojiwa hawakupatiwa orodha ya majibu ya kuchagua. Je, ni kweli hawakuwa wanawajua wagombea wengine waliotajwa zaidi ya Dk John Magufuli na Edward Lowassa wakabaki kusema “mwingine?”

8. Katika nafasi ya ubunge na udiwani, wahojiwa wameonyesha kuwajua na kuwapigia kura wagombea wa ACT-Wazalendo. Inakuwaje watu hao hao washindwe kumtaja mgombea urais wa chama hicho badala yake Twaweza ikamweka katika kundi la “mwingine?”

9. Takwimu zote asilimia huwa ni 100 iliwezekanaje mgawanyo wa takwimu katika ripoti ya Twaweza katika baadhi ya maeneo asilimia zilizidi na au kupungua 100?

10. Tafiti zilizopita za Twaweza zilikuwa zinajumuisha watu wengi na zilikuwa zinaonyesha mtu aliyeshika nafasi ya kwanza pengine hadi 10. Kwa nini katika utafiti huu waliwalenga wawili tu Lowassa na Magufuli?

11. Ripoti inasema kwamba dodoso la utafiti huu liliandaliwa kabla ya uteuzi wa wagombea urais wa vyama vingine (nje ya mseto wa Ukawa), kikiwamo ACT-Wazalendo. Je, dodoso hilo lilikuwa na maelekezo gani kiasi kwamba ikawa vigumu kuwaingiza wagombea wengine?

12. Kwanini matokeo ya utafiti na kinachoonekana nje ni picha mbili tofauti?

13. Matokeo ya awali ya Twaweza yalionyesha Lowassa alipokuwa CCM aliongoza kwa ushawishi, iweje ndani ya wiki mbili baada ya kuhamia upande wa pili aporomoke hivyo?

14. Kwanini Twaweza hawakushirikisha Zanzibar katika utafiti wakati urais ni wa Muungano?

From Mwananchi Tanzania


Hivi TCRA hii haiwahusu ee?
 
Magamba yanachungulia tuu huu uzii...#HapaZikaTuu trh 25 oct....
 
Maswali 14 yaliyoibuliwa na tafiti ya Twaweza

1. Kwa mara ya kwanza Twaweza walisoma ripoti ya utafiti na kuonyeshwa moja kwa moja na TV. Nani alidhamini utafiti, matangazo hayo na kwa madhumuni gani?

2. Kwa nini waliamua kutoa matokeo ya utafiti wao katikati ya kampeni zenye ushindani mkali na mhemko mkubwa wa kisiasa?

3. Je, ni jinsi gani watu waliohojiwa walichaguliwa?

4. Je, watu waliohojiwa ni wa kutoka maeneo gani, makundi gani ya watu, ukiacha jinsia?

5. Je, waliohojiwa wamejiandikisha kupiga kura, mashabiki tu au mchanganyiko?

6. Twaweza wanajua kwamba kampeni za wagombea urais huanza baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuidhinisha wagombea waliopendekezwa na vyama. Kwa nini shirika hilo lilianza kufanya utafiti siku mbili kabla ya hapo?

7. Twaweza wanasema wahojiwa hawakupatiwa orodha ya majibu ya kuchagua. Je, ni kweli hawakuwa wanawajua wagombea wengine waliotajwa zaidi ya Dk John Magufuli na Edward Lowassa wakabaki kusema “mwingine?”

8. Katika nafasi ya ubunge na udiwani, wahojiwa wameonyesha kuwajua na kuwapigia kura wagombea wa ACT-Wazalendo. Inakuwaje watu hao hao washindwe kumtaja mgombea urais wa chama hicho badala yake Twaweza ikamweka katika kundi la “mwingine?”

9. Takwimu zote asilimia huwa ni 100 iliwezekanaje mgawanyo wa takwimu katika ripoti ya Twaweza katika baadhi ya maeneo asilimia zilizidi na au kupungua 100?

10. Tafiti zilizopita za Twaweza zilikuwa zinajumuisha watu wengi na zilikuwa zinaonyesha mtu aliyeshika nafasi ya kwanza pengine hadi 10. Kwa nini katika utafiti huu waliwalenga wawili tu Lowassa na Magufuli?

11. Ripoti inasema kwamba dodoso la utafiti huu liliandaliwa kabla ya uteuzi wa wagombea urais wa vyama vingine (nje ya mseto wa Ukawa), kikiwamo ACT-Wazalendo. Je, dodoso hilo lilikuwa na maelekezo gani kiasi kwamba ikawa vigumu kuwaingiza wagombea wengine?

12. Kwanini matokeo ya utafiti na kinachoonekana nje ni picha mbili tofauti?

13. Matokeo ya awali ya Twaweza yalionyesha Lowassa alipokuwa CCM aliongoza kwa ushawishi, iweje ndani ya wiki mbili baada ya kuhamia upande wa pili aporomoke hivyo?

14. Kwanini Twaweza hawakushirikisha Zanzibar katika utafiti wakati urais ni wa Muungano?

From Mwananchi Tanzania
Mbona inajulikana wazi kuwa tafiti hizo za 'TWAWEZESHWA' zimetolewa kutokana na 'kolabo' ya nguvu ya kada wa Sisiem Maria wa Sarungi wa Twaweza na kada mwingine kijana wa magamba Makamba Junior.

Lengo likiwa kuinusuru merikebu yao ya magamba ambavyo hivi sasa inaelekea kuzama kabisa.

Sasa mambo yameenda kinyume kabisa cha matarajio yao, jahazi la magamba badala ya kuokolewa ndiyo wamelizamisha kabisa ndani ya kina kirefu baada ya matokeo ya utafiti huo kutoka!
 
msiumize vichwa jamani hawa kenge tarehe 25 inacherewa kufika. TWAWEZA ya Nigeria walimtabiri Jonathan atashinda kwa 75% nadhan nyote ni mashahahidi kwa ilivyotokea Nigeria. Rais wa Nigeria sasaivi ni nani??

No tusiridhike kirahisi hivyo.. Hawa jamaa wanawaandaa watu kisaikolojia ili waanze kuzoea kuwa ccm inashinda naamini kutakua na matokeo mengine yatatolewa "yaliyotengenezwa" lengo in kuwazoeza watu. Then kwenye uchaguzi wakichakachua watu wakubali kwa urahisi..
 
Swali 1
Sio mara ya kwanza kwa Twaweza kutoa matokeo yao kupitia TV.hatukuwahi kuhoji udhamini wao huko nyuma.
Sio ajabu kwa Twawe kutumia projection na live media kudisseminate matokeo yao.
Labda nikuulize kwa nini Ukawa wanatumia drone kupiga picha?

2 utafiti umefanyika mwezi agust-sept ulitaka watoe baada ya uchaguzi?

3 watu waliohojiwa walichaguliwa kwa random sampling na Aidan alilieleza hili.inaelekea hujasikiliza au kusoma utafiti huo.of course wakosoaji wote wa utafiti ni lazima waongelee methodology.

4 hili swali usingeuliza kama ungesikiliza presentation au hata clip iliyorushwa kwenye taarifa ya habari.

5 hili swali vile vile usingeuliza kama ungesoma objectives na conclusion za utafiti wa Twaweza.
7 hujanyimwa kuanzisha utafiti wako ili kuthibitisha yale ya Twaweza.

8 hebu soma swali lako la 11 halafu uulize tena haya maswali mawili.

9 Naona utafiti huu uliusoma kwenye message za watsapp ndio maana ukaja na hiyo asilimia zaidi ya 100.kwa taarifa yako hiyo msg ya watsapp ilikuwepo mwezi mzima kabla.

10 kuna kanuni katika utafiti inayokataza kurudia mambo aka re-invent the wheel.Ulitaka Tafiti ya mwaka huu ilingane na mwaka jana kwa kila kitu?

12 konachoonekana nje au kinachooneshwa nje na vyombo vya habari vya mafisadi ni kukitekenya na kujichekesha.Twaweza wamehighlight ukweli wa kwenye 'site'

13 lowassa alibebwa na ccm na alichukiwa na upinzani hivyo ni wazi umaarufu wake uporomoke.CCM walimkata sasa kanunua na kuuharibu upinzani...unadhani hiyo dhambi ni ndogo?

14 Hiyo yaweza kuwa limitation kama ni kweli hawakushirikisha zanzibar.kwa wasomi wanaelewa kuwa kila tafiti ina limitation zake.


Mwisho niseme tusipende kukurupuka.

#Hapakazitu

Simple answers to critical questions. Mbona unajibu bora lipite. Swali la 3, 7 na 9 ni mwiba. Huwezi kurupuka kuyajibu pamoja na maswali mengine yaliyobaki. Embu hata wewe soma majibu yako then uone kama umetendea haki maswali yaliyotolewa
 
Simple answers to critical questions. Mbona unajibu bora lipite. Swali la 3, 7 na 9 ni mwiba. Huwezi kurupuka kuyajibu pamoja na maswali mengine yaliyobaki. Embu hata wewe soma majibu yako then uone kama umetendea haki maswali yaliyotolewa


Mimi najiuliza kama TWAWEZA wangetoa matokeo ya uchunguzi yanayoonyesha UKAWA ama LOWASA na asilimia kubwa wangeitwa majina haya wanayoitwa sasa? Kwanini UKAWA hawataki kuelewa Wolper kabadilisha hata jina anajiita Lowasa hawamsemi lakini kila kukicha wanamshambulia Diamond. Kweli nimeamini UKAWA hawatashinda uchaguzi Oktoba 2015 ndiyo maana wanajiandaa na visingizio ili waende mahakamani. Lakini tambueni Magufuri ataapishwa tarehe 30 Oktoba kabla kesi yenu haijaenda mahakama kuu.


Kuhusu Wabunge naomba wabunge wengi watoke Upinzani.......Wabunge wote walioitetea serikali kwa ESCROW watoswe na wale waliopinga katiba pia watoswe hayo ndo mabadiliko ninayoytaka mimi si kuleta kiinimacho cha CCM kupitia mlango wa nyuma (UKAWA)....BIG NOOOOOOOOOOOOOO
 
swali la 15 kwa nini walikataa wanaume wasiulize maswali?
 
Ni aibu kwa taifa kuandaa taarifa za kupika na huu ni ufisadi pia, wakati Magufuli anasema atafunga mafisadi wakati huhuo anatumia pesa za ufisadi wa escrow kununua watafiti ,wasanii na wanasiasa uchwara.


Yaani Magufuli anajidanganya kuwa ana uwezo wa kupambana na mafisadi wa CCM. Hao Mafisadi anaowasema ndio wanafinance campaign zake zote , kumchapishia mabango na kuhonga wapinzani. fedha zote zilizotumika kuwahadaa wapinzani na yeye kuahidi vyeo kwa wanaccm uchwara ambao ndio wanaomomonyoa nchi kwa ufisadi na kuwa na affiliation kwenye mikataba tata ya gesi na mafuta. akipita magufuli itakua hata bora kwa mr. Impotent kwa kuwa huyu hakubaliki bali pesa ndio inayofanya kazi kujenga ushawishi.
Aeleze jinsi atakavyoshughulika na Katiba mpya na adhabu kwa benk kuu ya Tanzania iliyoshindwa kusimamia madeni ya nje, fedha za NBC, fedha za kussuppport wajasiriamali, fedha za kusaidia waagiza bidhaa nje, escrow, madeni mengine ya nje kama Libya na watuambie walionufaika nazo wanatiwaje adabu.

watuambie waratibu wa safari za raisi walivyofisadi nchi na kujiona ndio wenye hatimilkiki ya ikulu atakavyoshughulika nao. na ufisadi wa miradi ya bandari bagamoyo na bomba la gesi baadae atakavyoshughulikia ujenzi wa chini ya kiwango barabara ya Kimara posta na atuambie anayekula 10% kutoka strabarg. wanataka wafunike wapite. slogan ya hapa ni kazi tu ni kuwa hapa kazi ni wizi tu. CCM ni syndicate ya wizi na kisima cha uongo na ufisadi. na pia atamfanyaje mke wa mgombea wa ubunge ubungo aliyezalishia watu ARV feki Arusha atakavyushughulika naye na raisi anayemaliza muda wake kwa mali zenye mashaka yeye na familia yake!!
 
No tusiridhike kirahisi hivyo.. Hawa jamaa wanawaandaa watu kisaikolojia ili waanze kuzoea kuwa ccm inashinda naamini kutakua na matokeo mengine yatatolewa "yaliyotengenezwa" lengo in kuwazoeza watu. Then kwenye uchaguzi wakichakachua watu wakubali kwa urahisi..

mjomba ww huelewi Lowassa anasema wewe mtilie kura yako tu huko mbele anajuwa yeye kama kuna mchezo watachezeana. UKAWA Imejiandaa kinomaa miaka 5 ni mingi kusubiri uchaguzi mwengine, matokeo ni jino kwa jino.
 
Back
Top Bottom