Maswali kwa Mhe. Mnyika na CHADEMA

Kwanza umenishangaza na title ya thread kuelekeza swali kwa Mnyika amabaye sikumbuki kama niliona jina lake miongoni mwa wanakati waliokwenda Ikulu. Kama alikwenda, utasahihisha. Pia Mnyika si kiongozi wa juu kabisa kiuongozi au kiutendaji. Swali lako lilipaswa kuelekezwa kwa Mbowe.

Pili, CHADEMA hawakutoka bungeni eti kwa sababu ya kupingana 100% na yaliyokuwemo ktk muswada, bali walitaka usomwe kwa mara ya kwanza ili upatiwe fursa ya kuuchonga vizuri. Kwa serikali kuusoma kwa mara ya pili, ilikuwa na maana kuwa marekebisho yamefanyika & no room for further editing. Ilikuwa wazi kwa uwingi wa CCM na wapenzi wao CUF kuwa muswada ungepita tu. So ingekuwa kazi bure kukaa na kuchangia.

Baada ya muswada kuwa umepita bungeni (kwa sababu CDM wasingeweza kuuzuia) njia iliyobaki ilikuwa ni kumwona rais na kumsihi asiusaini muswada ili mapendekezo ya CDM yajumuishwe. Kwa hiyo ilikuwa sahihi kumkimbia shangazi, kwenda kwa mjomba. Mjomba akakataa ushauri wa CDM.

Swali lako sasa unapaswa kuwauliza CUF wanaotaka kwenda kuuza sura ikulu wakidhani ile mipicha na rais imewaongezea umaarufu viongozi wa CHADEMA. Hawana sababu ya msingi kwenda ikulu kwa sababu kabrasha lao walishampa mkuu siku nyingi. Wanakwenda kutafuta umaarufu wa magazeti na TV.

Kimsingi, CHADEMA imenufaika na kukutana na rais kwa sababu kimeonesha kuwa mamlaka inajua umuhimu wake na hivyo kukubali haraka haraka ombi la kumwona mkuu. Endapo JK angegoma kukutana na CDM tungekuwa tunaongea habari nyingine sasa hivi. Hata mkuu wa mabalozi wa Euro (Tim) aliishauri serikali kukaa na CDM kwa sababu alihisi CDM ni moto wa kuotea mbali japo yeye ni raia wa kigeni.
 
Perhaps CDM wanted to try something spectacular in meeting JK. Apart from acquiring a seemingly moral legitimacy (which could turn to moral authority with time), that trip was bizzare to be modest.

Ok it was strategical stumble. It's not a monumental error as some potray here. But they should admit and move back to the right lane
 
Kukutana na Raisi lilikuwa jambo muafaka. CHADEMA walikosa pa kusemea hoja za wanaowawakilisha kwa vile ambavyo Spika alipuuza mapendekezo ya kambi ya upinzani. Kuendelea kubaki wakati majadiliano yanaendelea kusingeleta badiliko lolote la maana. Chama cha upinzani hakitumii njia moja tu (ya maandamano au mijadala ya bunge) katika kuwakilisha maoni ya wanaowawakilisha. Inapopatikana fursa ya kuonana na mkuu wa nchi wanapaswa kuitumia fursa hiyo katika kumuonyesha athari za maamuzi anayokusudia kufanya. Kwa hilo CHADEMA walitimiza wajibu wao na mimi nakipongeza kitendo hicho. Juu ya kile Raisi alichoamua baada ya mazungumzo hayo, si swala la kuitupia lawama CHADEMA. Historia imeandikwa kuwa Raisi alishauriwa! Chadema ina watu wazima ambao naamini wanajua wanachokifanya. Raisi naye katika hili anaonekana kama kutaka kulitumia kama njia yake ya mwisho ya kujitoa katika lawama zinazomuandama. Anajaribu kufurahisha pande zote licha ya mashinikizo ya Chama chake kilichopitisha rasimu hiyo na ambacho kisingetaka kikao cha majadiliano alichokifanya kiihusu CHADEMA pekee! Kwa upande wa upinzani wa kweli na kundi la wanaharakati nako kuna shinikizo linalomkosesha usingizi. Hebu tusubiri tuone anaicheza vipi karata hii ya mwisho.
 
Maamuzi yaliyofikiwa na viongozi wa CDM kwenda kumwona Rais ni kitendo cha busara, kiungwana na cha muono wa mbali kinyume na watu wenye jazba wanavyofikiria.

Kumbuka kwamba JK ana tabia ya kigeugeu. Mifano ni mingi, lakini ulio dhahiri bado unitesa CCM ni kauli ya KUJIVUA GAMBA. Maoni ya CDM kuhusu muswada wa katiba mpya kwa yeyote ambaye amebahatika kuyapitia, bila kuingiza itikadi za kisiasa yanalenga moja kwa moja kwenye maslahi ya nchi. Kitendo cha kumfikishia JK ili ayaone maoni hayo ambayo ni sababu ya kususia mjadala huo bungeni ni kumthibitishia yeye na umma wa Watanzania kwamba mapendekezo yaliyotolewa na CDM ni kwa maslahi ya taifa.


Kama nilivyoeleza hapo awali kwamba JK ni kigeugeu (rejea simulizi yake ya mbayuwayu). Siku ya siku angewageuka CDM na kudai kwamba kama walikuwa na jambo la kumwona, tena anavyodai kuwa yeye msikivu, kwa nini hawakufanya hivyo. Na hapo kwa watu wenye muono wa karibu kama wewe, ungekuwa wa kwanza kulaumu kwamba kwa nini kama kulikuwa na fursa hiyo viongozi wa CDM hawakufanya hiyo.

Kama ilivyokuwa bungeni, baada ya CDM kuwasilisha muswada mbadala, wabuge wa CCM na CUF walikosa hoja (points) za ku-challenge maoni ya upinzani, badala yake wakaanza kumshambulia Lissu na CDM. Rais naye pia hakuna hoja ambayo ameitoa angalau kwa kuelezea mapungufu ya maoni aliyopelekewa na CDM na hivyo kupelekea kuusaini muswada. Kimsingi Rais amekubaliana na CDM kuhusu mapungufu yaliyomo katika muswada aliokwisha saini. Suala la Rais kuona mapungufu ni jambo moja na uamuzi wa kusaini ni jambo jingine, huwezi kuzuia mkono wa kusaini. La msingi hata wewe umejua kwamba kumbe hata Rais ameyakubali maoni ya CDM lakini amefanya jeuri kwa kutumia madaraka yake. Hili halina tofauti na kitendo cha Rais kuwaambia wezi wa fedha za EPA kwamba wakizirejesha hawatachukuliwa hatua. Anaelewa sheria inasema nini juu ya makosa ya wizi lakini yeye anaamua kinyume chake. Sheria haiwezi kufuata mkondo wake kama kila mwenye mamlaka anapasua mkondo anaoona ni kwa maslahi yake. HAYA NDIYO MAMBO YA KUTAZAMWA KWENYE KATIBA MPYA.

Kitendo cha CDM kwenda kumwona Rais na kuwasilisha maoni, mapendekezo na ushauri kwa mambo ya msingi kama katiba kwa mstakabali wa taifa, wameramba karata dume. Siku ya siku mambo yakibadilika yasivyotegemewa sababu ipo kwamba, CDM TULIFANYA KILA NJIA, HATA KWA MAJADILIANO YA ANA KWA ANA LAKINI........

Well said!!!!
 
Umesema vyema kijana .What Chadema did ni kitu ambacho kila mtu atakisema baadaye .Chadema kuingia barabarani kupinga sasa wataeleweka zaidi kuliko ambavyo ingalilkuwa without seeking to meet the Prez na siasa si uadui ni utofauti wa mawazo na mitizamno .

I wish this could be true!!
 
Wasingefika Ikulu kupeleka mapendekezo yao then waandamane tungewang'ong'a!

sasa wamekwenda ikulu, mapendekezo yao yangekubaliwa ....TUNGEWAPONGEZA!

sasa wamekwenda ikulu, wamekwa kwa msanii wa bongo da'silama jk, TAWABEZA!
 
siasa hiyo mbowe.........acha hasira!

Waberoya, nimekuwa nikisoma comment zako mbali mbali kwa muda sasa na kwa kweli sijui kwa nini leo nimeamua na mimi ku"comment" ! On the other hand nafikiri ni bora niendelee kukaa kimya, siku njema Mkuu.
 
we baki nyuma tu!wanaume,tunaenda kupambana kisha utanufaika hata wewe....baki ulee watoto wala usijali si lazima tuwe front wote kuna wanaotakiwa kubaki kwaajili ya kuangalia watoto kama wewe unafaa sana

wewe cjui 2takuzika wapi vile...sasa hivi nguvu ya umma hatudanganyiki..cdm mnakurupuka...mkitangaza maandamano mtapasuka...ole wenu...
 
Hoja yako ni ya msingi saana, but kwenye siasa pia kuna namna nyingi coz CDM walikua wanajua kua JK hajui anacho kitetea
kuhusu mswaada na ndio maana kimsingi alikiri kwamba CDM wana hoja but asipo sign chama chake kingechukua
maamuzi magumu. coz ndani ya ccm wako waliotaka hata anyang'anywe uenyekiti, wote tunawajua washauri
wa jk hawamshauri vizuri na ndo maana nchi inakua kama imekosa rais mwenye kuthubutu kutoa maamuzi.
 
Back
Top Bottom