Maswali kuntu kuhusu uchawi

Maswali kuntu kuhusu uchawi

Uchawi ulianza kabla ya Sayansi, Vitabu vya dini vinauzungumzia uchawi kuwa upo na kutukataza tusiufanye. Qur an inauzungumzia uchawi kama ni dhambi kubwa sana kuitenda kuliko dhambi zote za duniani, yaan ukifanya uchawi umefanya dhambi kubwa ziadi kuliko zote duniani, then inafata ushirikina, japo ushirikina na uchawi ni baba mmoja mama tofauti. Hizi ni dhambi kubwa kuliko kuua. Naomba niwasihi ndugu zangu waislam wasitamani kuujua wala kuufanya uchawi ila wajue tu kuwa upo na wajue namna ya kujikinga nao.

Wanasayansi wanaujua uchawi na wanaufanya pia, katika sayansi zao lazima washirikishe na uchawi pia, kwamfano ndege kupaa juu kupasua mawimbi... Bila kushirikisha uchawi mwanasayansi hafanikishi hili,
Ujenzi wa barabara, kuna sehemu barabara zinapita inakatwa miti mikubwa.... Miti ambayo wachawi wanaitumia katika mambo yao, hivyo basi mkandarasi kama hajafanya uchawi na kwenda nao sawa hawezi kufanikisha jambo lake, wachina wanaojenga barabara kubwa na madaraja makubwa nao ni wachawi sana tena sana.
Muelevu hawezi kunipinga, mjinga anaweza kunipinga kutokana na kutokujua kwake.

Note: Uchawi upo, utakuja kuujua kama upo yakikufika mambo, ipo siku.


Mkuu, umeandika baadhi ya mambo usiyo na elimu nayo. Umechanganya uchawi na ushirikina, pia unasema katika uislamu dhambi kuu ni uchawi, pia unasema wazungu hurusha ndege angani kwa kutumia uchawi, pia unasema wajenzi wa barabara na wanapong'oa miti hutumia uchawi.

Sio kweli mkuu.
 
Mkuu, umeandika baadhi ya mambo usiyo na elimu nayo. Umechanganya uchawi na ushirikina, pia unasema katika uislamu dhambi kuu ni uchawi, pia unasema wazungu hurusha ndege angani kwa kutumia uchawi, pia unasema wajenzi wa barabara na wanapong'oa miti hutumia uchawi.
Sio kweli mkuu.
Tofauti ya uchawi na ushirikina ni ipi?
 
kinachanishangaza pale mtu anaumwa kabanwa hasa afu daktari anapima anakuta hamna ugonjwa wowote lakn mgonjwa analalamika.then mgonjwa anapelekwa kwa mganga wa kienyeji ana chezesha ndumba zake mgonjwa anapona.h ni zaid ya tehama kwakweli
Ndio maana mie nasema waganga wote wangekuwa waongo au hakuna uchawi basi hadi leo biashara ya uganga isingekuwepo,kwa sababu kusingekuwa na shuhuda za watu kufanikiwa au kupoma matatizo yao hivyo watu wasingekuwa wanaenda na biashara ya uganga ingeisha.
 
Kuna dau nilishaweka na bado lipo.... niroge upate sh laki 3 cash (kutokana na uwezo wangu) usiulize kuhusu detail zangu maana uchawi ni supernatural unaweza kuja kwangu bila hata kujua jina langu..
Ila uchawi si kuroga tu unatumika kwa mambo mengi sasa sioni haja ya wewe kutoa dau na kusubiri kurogwa na hata ukirogwa utajuaje kuwa hapa nimerogwa?
 
Mshana Jr: funguka zaidi sote tupate kujua kilichonyuma ya pazia. Mimi ni kati ya wale wanao amini kuwa elimu hii ikiwekwa wazi na kutumika ipasavyo tunaweza kuendelea hadi wazungu watushangae. Pia naamini uchawi hauna kitu cha ajabu zaidi ya kujua namna ya
sayansi ambayo haijawekwa wazi kwasababu aghalabu misingi yake inakiuka maadili na utu wa mtu.mmh hapana sio kweli kabisa
@Mshana Jr: Funguka zaidi sote tuweze kujua kilicho nyuma ya pazia. Mi naamini elimu hii ikijulikana na kutumika vyema tunaweza kuwa juu hadi wazungu watushangae. Nafikikiri uchawi hauna kitu cha ajabu kisichokiwepo kwenye nature, ila njia wanazotumia wachawi kupambana na nature zinaweza kuwa bado hazijulikani na wanasayansi au bado wanazitafiti. Kwa upande wangu nahisi elimu hii ya uchawi inatoka kwa majini na viumbe wengine ambao wanaweza kuwa sayansi yao imeendelea kuliko yetu. Shida kubwa kwetu watu weusi ni kuwa tunatumia elimu ya viumbe hao bila kuifahamu wala kutaka kuijua kwa undani. Hivyo, wewe kama umebahatika kuijua anza kutuelewesha tuweze kifaidika wote na vizazi vijavyo. Wazungu wenzetu wameanza kuandika mambo haya na hata kutengeza filamu. Sisi kwa nini tuendelee kufanya siri?
 
Hivi ni kweli wachawi wanaruka usiku na ungo?

Na kama wanaruka, nani aliwahi kuthibitisha kwa macho yake? (naked eyes)

Na wanasayansi mnazungumziaje suala hili la wachawi kuruka na ungo? Mnaliamini?

Teknolojia ya wireless ilitoka wapi? Idea yake....!??? Au ndio mliipata huku kupitia uchawi? Mtu yupo Kihonda Morogoro anamroga mtu yupo Masaki Dar es salaam

Au wachawi nao wanaminara ili kurusha mawimbi?

Nawasilisha!!!!!

.
 
Mwenyewe nimetafuta sana uchawi ata niwe napaaa, miaka 7 saivi sijapata kila nikienda kwa wahusishwaji wanasema hawajui kama vile rupea ya Germany

Natumain apa lazima tupate huo mchanganyiko ili nipae maana uko juu angani hamna foleni
we hututakii mema wewe
 
Mwenyewe nimetafuta sana uchawi ata niwe napaaa, miaka 7 saivi sijapata kila nikienda kwa wahusishwaji wanasema hawajui kama vile rupea ya Germany

Natumain apa lazima tupate huo mchanganyiko ili nipae maana uko juu angani hamna foleni
 
Tofauti ya uchawi na ushirikina ni ipi?



Mkuu, Ushirikina ni jambo lolote ambalo mtu analichukua au analifanya pahala ambapo alitakiwa amuweke Mungu, mfano mtu akiamua kuabudu mti au jiwe au sanamu nk, hapo atakuwa anafanya ibada ya kishirikina kwasababu mahala pa kumuabudu Mungu yeye ameweka jiwe au sanamu nk, kwa jinsi hiyo huyo mtu amemshirikisha Mungu katika hiyo ibada na jiwe au sanamu nk, ndiyo maana mtu huyo ataitwa mshirikina.
Ushirikina ni; (the association of something with God).

Baada ya kufahamu nini ushirikina sasa tuje kwenye Uchawi, Uchawi ni elimu ambayo mtu anaweza kujifunza, elimu hiyo inaweza kutumika au kufuatwa na kuwa ushirikina (superstitious), yaani jinsi uchawi utakavyotumika ndivyo unaweza kuwa ni ushirikina au laa, mfano kama uchawi utatumika kumdhuru mtu hapo huo uchawi siyo Ushirikina bali ni uhalifu kama uhalifu mwingine, lakini mfano kama mtu anatafuta kazi akaenda kwa mganga kufanya matambiko ili apate kazi au mtu akavaa hirizi ili apate ulinzi na watu wabaya au akaweka hirizi dukani awavute wateja basi imani na hayo matendo ni ushirikina kwasababu huyo mganga na hirizi zimekaa pahali ambapo Mungu alitakiwa aombwe ili asaidie.

Kuna ushirikina wa aina mbalimbali, mfano hata mtu akijisifia nafsini mwake kwa kupata mafanikio ya aina fulani katika maisha hiyo nayo ni ushirikina (self esteem) hata mtu akijisifia kwa uwezo wa akili zake kuwa kubwa nao ni ushirikina wa nafsi (egoism)--- kwa sababu inatakiwa Mungu pekee asifiwe pale ambapo mtu anapopata mafanikio na sio kujisifu kwa sababu kimsingi mafanikio hayo ni Mungu aliyekupatia na sio wewe mwenyewe na ndiyo maana sisi Waislamu tumefundishwa na Mtume wetu mtukufu kwamba tunapopata mafanikio au faraja ya aina yoyote basi tuseme; "Alhamdulillah" yaani; Sifa zote njema zinamuhusu Allah (Mungu) pekee, kwa dua hiyo mtu anakuwa amekata mzizi wa ushirikina wa nafsi yake.

Kwa Kifupi hiyo ndiyo maana ya ushirikina unavyohusiana na Uchawi.
 
Mkuu, Ushirikina ni jambo lolote ambalo mtu analichukua au analifanya pahala ambapo alitakiwa amuweke Mungu, mfano mtu akiamua kuabudu mti au jiwe au sanamu nk, hapo atakuwa anafanya ibada ya kishirikina kwasababu mahala pa kumuabudu Mungu yeye ameweka jiwe au sanamu nk, kwa jinsi hiyo huyo mtu amemshirikisha Mungu katika hiyo ibada na jiwe au sanamu nk, ndiyo maana mtu huyo ataitwa mshirikina.
Ushirikina ni; (the association of something with God).
Baada ya kufahamu nini ushirikina sasa tuje kwenye Uchawi, Uchawi ni elimu ambayo mtu anaweza kujifunza, elimu hiyo inaweza kutumika au kufuatwa na kuwa ushirikina (superstitious), yaani jinsi uchawi utakavyotumika ndivyo unaweza kuwa ni ushirikina au laa, mfano kama uchawi utatumika kumdhuru mtu hapo huo uchawi siyo Ushirikina bali ni uhalifu kama uhalifu mwingine, lakini mfano kama mtu anatafuta kazi akaenda kwa mganga kufanya matambiko ili apate kazi au mtu akavaa hirizi ili apate ulinzi na watu wabaya au akaweka hirizi dukani awavute wateja basi imani na hayo matendo ni ushirikina kwasababu huyo mganga na hirizi zimekaa pahali ambapo Mungu alitakiwa aombwe ili asaidie.
Kuna ushirikina wa aina mbalimbali, mfano hata mtu akijisifia nafsini mwake kwa kupata mafanikio ya aina fulani katika maisha hiyo nayo ni ushirikina (self esteem) hata mtu akijisifia kwa uwezo wa akili zake kuwa kubwa nao ni ushirikina wa nafsi (egoism)--- kwa sababu inatakiwa Mungu pekee asifiwe pale ambapo mtu anapopata mafanikio na sio kujisifu kwa sababu kimsingi mafanikio hayo ni Mungu aliyekupatia na sio wewe mwenyewe na ndiyo maana sisi Waislamu tumefundishwa na Mtume wetu mtukufu kwamba tunapopata mafanikio au faraja ya aina yoyote basi tuseme; "Alhamdulillah" yaani; Sifa zote njema zinamuhusu Allah (Mungu) pekee, kwa dua hiyo mtu anakuwa amekata mzizi wa ushirikina wa nafsi yake.
Kwa Kifupi hiyo ndiyo maana ya ushirikina unavyohusiana na Uchawi.
Umeeleza vizuri mkuu umeeleweka.
 
Back
Top Bottom