Maswali kumi kwa Edward Lowassa na Wafuasi wake

HIZI NDIZO HOJA 10 ZINAZOMTAFUNA
LOWASSA. Soma hapa kujua:

1. Gazeti la Raia Mwema la Novemba 2010 , liliripoti na kuonyesha picha ya nyumba ambayo familia yako inamiliki Uingereza. Ukasema ni ya mwanao. Je, kwa nchi maskini kama ya kwetu, ni sahihi kwa kiongozi mkubwa kumiliki nyumba kubwa na ya kifahari nje ya nchi?

2. Mkapa alipounda Baraza la Mawaziri jipya mwaka 1995 alikuacha. Wengi wanasema kwamba Mwalimu alimwambia asikupe hata Uwaziri. Je, Kwanini mwalimu Alikukataa?

3. Tangu mwaka 1994, yaani miaka 20 sasa, Afrika ya Kusini imekuwa inakodisha nyumba yako Masaki kama Ubalozi wake. Kuna tetesi kwamba huko nyumba walitaka kuhama lakini wakaogopa kuihama nyumba inayomilikiwa na kiongozi mkuu na kuna tetesi kwamba sasa wanataka kuhama lakini wanatishiwa kwamba hamuwezi kuhama nyumba ya Rais ajaye. Ni kiasi gani cha fedha umepata kwa miaka 20 ya kukodisha nyumba hiyo ? Je, kiasi hicho kimeripotiwa kwenye fomu ya maadili?

4. Kuna maelezo kwamba nyumba hiyo ya Masaki ambayo Mzee Mandela alikuja mwaka 1994 kuufungua ubalozi mpya wa Afrika ya Kusini ndicho chanzo kikuu cha Mwalimu kusema kwamba inakuwaje kijana wa miaka 41, akiwa mtumishi wa umma maisha yake yote na mshahara wake unajulikana, anamiliki hekalu kama lile na tena kulikodisha kwa Serikali ya kigeni. Je, unasemaje kuhusu hili?

5. Pia unamiliki ranchi kubwa sana kule Mzeri Handeni. Ranchi hiyo ilikuwa ranchi ya Taifa lakini ukajimegea na sasa umeipanua kwa kumega maeneo zaidi. Ranchi hiyo uliipata ukiwa bado kiongozi wa umma. Je, mtu aliyewahi kuwa Waziri wa Mifugo na Waziri Mkuu kujiuzia ranchi iliyokuwa ya Serikali inaendana na dhana ya uongozi safi na uliotukuka? Tukikupa madaraka makubwa zaidi hautajiuzia kila kitu? Vilevile, katika nchi ambayo wananchi wengi hawamiliki ardhi, kwa kiongozi anayetaka kuwa Rais wetu, kuhodhi eneo kubwa la ardhi, inatuma picha gani kwa
wananchi hao?

6. Kwenye sakata la Richmond, ujasiri ni kusema ukweli au kubwaga manyanga? Kama ungesema ukweli na usingejiuzulu kwenye Richmond, Chama kingeathirika vipi wakati unasema hakuna kosa lililofanyika?

7. Kwanini kwenye kila tukio la kitaifa ukisimama tu karibu na Kikwete unahangaika kutuma picha kwenye magazeti na mitandao?

8. Katika miaka yako 40 ya utumishi wa umma, kuna jipi jipya ambalo umelisahau na sasa utalifanya kwenye Urais?

9. Umekuwa Waziri wa Ardhi, mbona matatizo ya ardhi bado tele nchini? Umekuwa Waziri wa Maji, mbona matatizo ya maji bado tele? Umekuwa Waziri wa Mazingira, mbona kuna matatizo ya uchafuzi wa mazingira? Umekuwa Waziri wa Mifugo, mbona wafugaji bado maskini na wanahangaika? Huo urais unautaka wa nini kama uwaziri umekushinda?

10. Kwenye sikukuu ya Mwaka Mpya, kila MNEC kapata milioni 1, hizo ni milioni 370 na kila mjumbe 500, 000 hizo ni bilioni 2. Hizi pesa zinatoka wapi na zitarudishwa vipi? Je, kuna zoezi la usafishaji wa pesa chafu linalofanywa kupitia kampeni yako?

1. Mkuu mtu kuwa na nyumba nje ya nchi si neno bali ishu ya msingi ni kwamba ameipataje. Wapo watz wengi wengi wenye nyumba nje ya nchi hata miki au yule jamaa wa dubai.

2. Kuhusu kuachwa kwenye baraza la mkapa 1995 haimaanishi chochote kwa sababu haijaandikwa kwenye katiba kwamba kila baraza lazima edu awepo.

3. Usiamini sana tetesi maana ndo kazi kubwa ya wabongo waleo kuzusha maneno. Lakini tatizo liko wapi nyumba yake kukodishwa na ubalozi, mbona taasisi nyingi za umma na binafsi even international ones zipo kwenye nyumba za watu binafsi? ??? Au tatizo edu?

4. Miaka 41 si kidogo ndugu yangu wapo vijana siku hizi wanamiliki mijumba ya hatari at age of 23-30. Nenda kaangalie kwa msando alafu thamanisha.

5. Ranchi ya mzeri wala hajajimilikisha kama unavydhani wewe na kupotosha jukwaa. Ranchi ina shareholders 9 na mchakato ulifuata taratibu zote au ulitaka wazungu wawekeze. Kumbuka ufugaji ni asili yake so sioni tatizo.

6. Richmond majibu yake unayo but hulazimishwi kuamini

7. Suala la picha ni kama humu jf niambie kuna nyuzi ngapi zinazomhusu je ameziazisha yeye ???? Simple like that tofautisha picha ya kujipiga na iliyopigwa na mtu mwingine. Kiufupi imefika mahali magazeti hayauziki bila story ya mshikaji na ndiyo ishara ya kupendwa the same to jf.

To be continued. ..
 
nakala ya uzi huu iwafikie ndugu kiloriti , ocampo four , young tanzanian , needsela , hamis mngeja na WAPENDA MISHIKAKI YA BURE wote wa MONDULI NA DSM pamoja na jamaa wote wanaohusika .
 
1. Bahati nzuri taarifa za gazeti like bado zipo mtandaoni. Sanga unachojaribu kukiremba hapa ni kionekane ni ukweli ni chuki dhidi ya Lowassa. Na mwanae Fred Lowassa alishawajibu waandishi Wa habari ile ambaye iliandikwa 2010 baada ya uchaguzi mkuu Wa urais na ubunge. Aliyeandika habari aliandika akihofia pengine Lowassa angeteuliwa kwenye baraza la mawaziri. Hivyo hii ilikuwa ni kuendeleza dhana ile yakuchafuana kupitia baadhi ya magezeti ambaye wamiliki wake dhidiya Lowassa inafahamika!

2. Kuhusu jengo la ubalozi wa Afrika kusini rejea makala ya Profesa Kitila Mkumbo. Hapa wewe mleta hoja inaonekana unawasilisha hoja nyepesi ambazo ndani yake imejaa chuki dhidi ya ndugu Lowassa kipenzi cha watanzania wengi kwa sasa. Hili halipingiki!

3. Kuhusu uteuzi katika baraza la mawaziri' aliyekuwa na mandate ya uteuzi ni ndugu Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wakati huo Benjamin w. Mkapa mzee wa uwazi na ukweli na siyo Nyerere. Je kama Lowassa alikuwa na tatizo kwa nini ndugu Benjamin Mkapa alimteuwa na kumuita yeye pamoja na Waziri wengine askari wa miamvuli? Ukitaka kudangaya usiwe msahaulifu. Je unayo memory lapse? Mbona katika hoja zako hujasema Edward kasimamia usambazaji wa maji ziwa Victoria kwenda Shinyanga kwa kupuuza mikataba isiyotija ya kikoloni baada ya uteuzi ule!

4. Mleta mada inaonekana ndugu Sanga umejawa na chuki dhidi ya Lowassa unapoorodhesha wizara ambazo Lowassa amepita na kutegemea kuwa matatizo yatakwisha. Hiyo inaonesha njinsi mawazo yako ni finyu na yasiyotaka kupanuka. Hapa ulitakiwa kufanya comparative analysis na siyo vinginevyo. Lowassa katika maisha yake hajawahi kutungiwa msamiati wa Waziri mzigo Kama ilivyofanywa Kwa wengine tena na wenyewe Chama kikongwe kuliko vyama vyote barani Afrika(CCM).

5. Kuhusu kuorodhesha Mali zake kwenye tume ya maadili ya viongozi wa umma tunakuomba tena uwache uvivu, wivu wa kike na chuki binafsi dhidi ya Edward. Jaribu kwenda kwenye Ofisi zile na kuomba faili la Edward Lowassa utakuta kila kitu kimeorodheshwa! Unasahau mleta mada kwamba Mungu akiamua kukubariki anakubariki kweli kweli. Naomba umuone Lowassa akufundishe siri ya kutoa iliyojificha kwenye kitabu cha Malaki katika maandiko takatifu! Pia fahamu pia kutoa ni ibada ya kweli na wewe nakusihi kalijaribu hili na wewe pia utabarikiwa Kama alivyobarikiwa ndugu Lowassa.

6. Kuhusu umiliki wa Mazera Ranch nafikiri ile ilikuwa Sera ya serikali kumilikisha wazawa mashamba haya ya kufugia mifugo. Leo kuna watu wengi ambao siyo wazawa wanamiliki ardhi chungu nzima Manyara na maeneo mengine ya nchi lakini hamsemi! Ikiwa ni Lowassa anamiliki itakuwa nongwa! Hoja yako ni hafifu Sana. Hata wewe Leo hii Sanga ukitaka Ranchi ya kufugia mifugo nenda pale NARCO jengo la Mavuno posta mpya watakushauri namna yakupata eneo la kufugia. Kwa hivyo acha uvivu changamkia fursa. Majungu na chuki havijengi!

7. Kuhusu Lowassa kuutaka urais na Kama atabadilisha maisha ya watanzania, hili halina ubishi hata mtoto mdogo analifahamu hili.

Mkuu umepangua Hizi hoja vizuri..big up
 
As much as I don't like Lowassa as my President but I think he is hard-done by on this wealth thing.But I think most of Tanzanians are still stuck in socialist thinking. Socialists think everyone who is rich is evil.

Mkuu bora ungeandika kwa kiswahili tu
 
1. Mkuu mtu kuwa na nyumba nje ya nchi si neno bali ishu ya msingi ni kwamba ameipataje. Wapo watz wengi wengi wenye nyumba nje ya nchi hata miki au yule jamaa wa dubai.

2. Kuhusu kuachwa kwenye baraza la mkapa 1995 haimaanishi chochote kwa sababu haijaandikwa kwenye katiba kwamba kila baraza lazima edu awepo.

3. Usiamini sana tetesi maana ndo kazi kubwa ya wabongo waleo kuzusha maneno. Lakini tatizo liko wapi nyumba yake kukodishwa na ubalozi, mbona taasisi nyingi za umma na binafsi even international ones zipo kwenye nyumba za watu binafsi? ??? Au tatizo edu?

4. Miaka 41 si kidogo ndugu yangu wapo vijana siku hizi wanamiliki mijumba ya hatari at age of 23-30. Nenda kaangalie kwa msando alafu thamanisha.

5. Ranchi ya mzeri wala hajajimilikisha kama unavydhani wewe na kupotosha jukwaa. Ranchi ina shareholders 9 na mchakato ulifuata taratibu zote au ulitaka wazungu wawekeze. Kumbuka ufugaji ni asili yake so sioni tatizo.

6. Richmond majibu yake unayo but hulazimishwi kuamini

7. Suala la picha ni kama humu jf niambie kuna nyuzi ngapi zinazomhusu je ameziazisha yeye ???? Simple like that tofautisha picha ya kujipiga na iliyopigwa na mtu mwingine. Kiufupi imefika mahali magazeti hayauziki bila story ya mshikaji na ndiyo ishara ya kupendwa the same to jf.

To be continued. ..

Mkuu hongera umepangua hoja vyema sana
 
Ameshibia wapi? Yaani mtu aibe mali za umma na fedha za wananchi alafu unasema bora alieshiba, acheni kupenda kutumika njaa mbaya mtachagua visivyochagulika matokeo yake nchi inaangamia.
Kuna watu walikuwa kapuku tena just wanafunzi waliomaliza chuo wameenda kuwa mabilionea ikulu.... umefanya nini kuzuia hilo?? Unaongea ongea tu uwezo huna wa kuwafanya lolote
 
Acha siasa ambazo hazi fact yoyote,tatizo watz hatupendi kusoma wala kutafiti mambo,tukisikia sehemu ndilo tutaloliamini.tuwe na fact za kuandika humu sio kusikia tu na kupelekwa na watu kisiasa.
 
HIZI NDIZO HOJA 10 ZINAZOMTAFUNA
LOWASSA. Soma hapa kujua:

1. Gazeti la Raia Mwema la Novemba 2010 , liliripoti na kuonyesha picha ya nyumba ambayo familia yako inamiliki Uingereza. Ukasema ni ya mwanao. Je, kwa nchi maskini kama ya kwetu, ni sahihi kwa kiongozi mkubwa kumiliki nyumba kubwa na ya kifahari nje ya nchi?

2. Mkapa alipounda Baraza la Mawaziri jipya mwaka 1995 alikuacha. Wengi wanasema kwamba Mwalimu alimwambia asikupe hata Uwaziri. Je, Kwanini mwalimu Alikukataa?

3. Tangu mwaka 1994, yaani miaka 20 sasa, Afrika ya Kusini imekuwa inakodisha nyumba yako Masaki kama Ubalozi wake. Kuna tetesi kwamba huko nyumba walitaka kuhama lakini wakaogopa kuihama nyumba inayomilikiwa na kiongozi mkuu na kuna tetesi kwamba sasa wanataka kuhama lakini wanatishiwa kwamba hamuwezi kuhama nyumba ya Rais ajaye. Ni kiasi gani cha fedha umepata kwa miaka 20 ya kukodisha nyumba hiyo ? Je, kiasi hicho kimeripotiwa kwenye fomu ya maadili?

4. Kuna maelezo kwamba nyumba hiyo ya Masaki ambayo Mzee Mandela alikuja mwaka 1994 kuufungua ubalozi mpya wa Afrika ya Kusini ndicho chanzo kikuu cha Mwalimu kusema kwamba inakuwaje kijana wa miaka 41, akiwa mtumishi wa umma maisha yake yote na mshahara wake unajulikana, anamiliki hekalu kama lile na tena kulikodisha kwa Serikali ya kigeni. Je, unasemaje kuhusu hili?

5. Pia unamiliki ranchi kubwa sana kule Mzeri Handeni. Ranchi hiyo ilikuwa ranchi ya Taifa lakini ukajimegea na sasa umeipanua kwa kumega maeneo zaidi. Ranchi hiyo uliipata ukiwa bado kiongozi wa umma. Je, mtu aliyewahi kuwa Waziri wa Mifugo na Waziri Mkuu kujiuzia ranchi iliyokuwa ya Serikali inaendana na dhana ya uongozi safi na uliotukuka? Tukikupa madaraka makubwa zaidi hautajiuzia kila kitu? Vilevile, katika nchi ambayo wananchi wengi hawamiliki ardhi, kwa kiongozi anayetaka kuwa Rais wetu, kuhodhi eneo kubwa la ardhi, inatuma picha gani kwa
wananchi hao?

6. Kwenye sakata la Richmond, ujasiri ni kusema ukweli au kubwaga manyanga? Kama ungesema ukweli na usingejiuzulu kwenye Richmond, Chama kingeathirika vipi wakati unasema hakuna kosa lililofanyika?

7. Kwanini kwenye kila tukio la kitaifa ukisimama tu karibu na Kikwete unahangaika kutuma picha kwenye magazeti na mitandao?

8. Katika miaka yako 40 ya utumishi wa umma, kuna jipi jipya ambalo umelisahau na sasa utalifanya kwenye Urais?

9. Umekuwa Waziri wa Ardhi, mbona matatizo ya ardhi bado tele nchini? Umekuwa Waziri wa Maji, mbona matatizo ya maji bado tele? Umekuwa Waziri wa Mazingira, mbona kuna matatizo ya uchafuzi wa mazingira? Umekuwa Waziri wa Mifugo, mbona wafugaji bado maskini na wanahangaika? Huo urais unautaka wa nini kama uwaziri umekushinda?

10. Kwenye sikukuu ya Mwaka Mpya, kila MNEC kapata milioni 1, hizo ni milioni 370 na kila mjumbe 500, 000 hizo ni bilioni 2. Hizi pesa zinatoka wapi na zitarudishwa vipi? Je, kuna zoezi la usafishaji wa pesa chafu linalofanywa kupitia kampeni yako?

hiv EL katangaza nia?
 
HIVI HIZI NI KASHFA DHIDI YA LOWASA AU NI FACTS?

Nekutana na maswali fulani kwenye mitandao ya kijamii yakiwa yanamgusa E.Lowasa, binafsi sijaelewa kama ni kashfa za makusudi dhidi ya EL au ni facts


1 .Edward Lowasa gazeti la Raia Mwema la Novemba 2010 ,liliripoti na kuonyesha picha ya nyumba ambayo familia yako inamiliki Uingereza . Ukasema ni ya mwanao . Je, kwa nchi maskini kama ya kwetu , ni sahihi kwa kiongozi mkubwa kumiliki nyumba kubwa na ya kifahari nje ya nchi ?

2 . Mkapa alipounda Baraza la Mawaziri jipya mwaka 1995 alikuacha . Wengi wanasema kwamba Mwalimu alimwambia asikupe hata Uwaziri je Kwanini mwalimu Alikukataa???

3 . Tangu mwaka 1994 , yaani miaka 20 sasa, Afrika ya Kusini imekuwa inakodisha nyumba yako Masaki kama Ubalozi wake . Kuna tetesi kwamba huko nyumba walitaka kuhama lakini wakaogopa kuihama nyumba inayomilikiwa na kiongozi mkuu na kuna tetesi kwamba sasa wanataka kuhama lakini wanatishiwa kwamba hamuwezi kuhama nyumba ya Rais ajaye . Ni kiasi gani cha fedha umepata kwa miaka 20 ya kukodisha nyumba hiyo ? Je kiasi hicho kimeripotiwa kwenye fomu ya maadili?

4 . Kuna maelezo kwamba nyumba hiyo ya Masaki ambayo Mzee Mandela alikuja mwaka 1994 kuufungua ubalozi mpya wa Afrika ya Kusini ndicho chanzo kikuu cha Mwalimu kusema kwamba inakuwaje kijana wa miaka 41 , akiwa mtumishi ya umma maisha yake yote na mshahara wake unajulikana , anamiliki hekalu kama lile na tena kulikodisha kwa Serikali ya kigeni . Je, unasemaje kuhusu hili ?

5 . Pia unamiliki ranchi kubwa sana kule Mzeri Handeni . Ranchi hiyo ilikuwa ranchi ya taifa lakini ukajimegea na sasa umeipanua kwa kumega maeneo zaidi . Ranchi hiyo uliipata ukiwa bado kiongozi wa umma. Je, mtu aliyewahi kuwa Waziri wa Mifugo na Waziri Mkuu kujiuzia ranchi iliyokuwa ya Serikali inaendana na dhana ya uongozi safi na uliotukuka? Tukikupa madaraka makubwa zaidi hautajiuzia kila kitu? Vilevile, katika nchi ambayo wananchi wengi hawamiliki ardhi , kwa kiongozi anayetaka kuwa Rais wetu , kuhodhi eneo kubwa la ardhi , inatuma picha gani kwa wananchi hao ?

6 . Kwenye sakata la Richmond , ujasiri ni kusema ukweli au kubwaga manyanga? Kama ungesema ukweli na usingejiuzulu kwenye Richmond , kingeathirika vipi wakati unasema hakuna kosa lililofanyika?

7 . Kwanini kwenye kila tukio la kitaifa ukisimama tu karibu na Kikwete unahangaika kutuma picha kwenye magazeti na mitandao yote ???


8 . Katika miaka yako 40 ya utumishi wa umma, kuna jipi jipya ambalo umelisahau na sasa utalifanya kwenye Urais?

9 . Umekuwa Waziri wa Ardhi , mbona matatizo ya ardhi bado tele nchini ? Umekuwa Waziri wa Maji , mbona matatizo ya maji bado tele ? Umekuwa Waziri wa Mazingira, mbona kuna matatizo ya uchafuzi wa mazingira ? Umekuwa Waziri wa Mifugo, mbona wafugaji bado maskini na wanahangaika ?? huo urais unautaka wa nini kama uwaziri umekushinda?

10 . Kwenye sikukuu hii , kila MNEC kapata milioni 1 , hizo ni milioni 370 na kila mjumbe 500 , 000 hizo ni bilioni 2 . Hizi pesa zinatoka wapi na zitarudishwa vipi? Je, kuna zoezi la usafishaji wa pesa chafu linalofanywa kupitia kampeni yako?

CHANZO; FULL HABARI
 
Back
Top Bottom