Maswali 11 juu ya ujio mpya wa Lipumba

Maswali 11 juu ya ujio mpya wa Lipumba

Anataka kuwa mwenyekiti wa CUF sio UKAWA.
Alipinga Lowassa kuwa mgombea wa UKAWA na sio kuwa mwanachama wa CHADEMA.
Au CHADEMA inataka uchaguzi ujao pia mgombea urais atoke kwao na lazima awe Lowassa???
mzee kashatangaza nia 2020 mapema kabisaaa... sasa unafikiri nani mwingine wa kusimama zaidi ya ENL
 
Na, Emmanuel Lukwaro.

Prof Ibrahimu Haruna Lipumba, Aliyekuwa mwenyekiti w Chama Cha Wananchi CUF, na kujiuzulu mwezi November mwaka jana. Ameibuka upya na kusema kuwa amemuandikia katibu mkuu wa chama hicho barua ya kuomba kutengua maamuzi yake ya kujiuzulu na kwamba arejeshwe kwenye nafasi yake ya uwenyekiti.

Prof Lipumba ametamka hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa hababari jijini Dar es salaam. Hata hivyo uamuzi huo wa Lipumba umenisukuma kufikiri na kutafakari kwa kina hatimaye kujiuliza maswali haya 11.

1.Tatizo kubwa na la msingi lililopelekea kujiuzulu kwa mujibu wa maelezo yake lilikuwa Lowasa kujiunga na ukawa,Je lowasa ameshaondoka ukawa? Au akirejeshewa nafasi yake ataitoa CUF UKAWA?

2.Prof Lipumba aliondoka wakati UKAWA wamemkariribisha Lowasa na kumpa nafasi ya kugombea uraisi ambayo naye aliihitaji. Je hakujivuwa uwenyekiti kwa hasira (kususa ) baada ya kukosa nafasi hiyo?

3.Prof Lipumba amekaa nje ya uongozi wa CUF kwa miezi takriban saba.Lakini katika kipindi chote hicho hakuona umuhimu wa kuongezea nguvu upinzani bali wakati huu kuelekea uchaguzi mkuu wa chama. Je huu sio mkakati wa kukivuruga chama na UKAWA?

4.Je kati ya sasa na kipindi cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu ni wakati gani ambao upinzani ulihitaji nguvu ya ziada?
Prof amejenga hoja kuwa anataka kurejea nafasi ya uwenyekiti ili kuuongezea upinzani nguvu katika kipindi hiki.

5.Je Prof Lipumba kama msomi haamini kuwa mwanachama wa kawaida (asiye kiongozi), anaweza kuwa na mchango mkubwa kukijenga chama wakati mwingine kuliko hata kiongozi? au yeye hajazoea kuwa mwanachama wa kawaida?.

6. Je Prof Lipumba haamini kuwa CUF kuna watu wengine wenye uwezo wa kuongoza, hasa nafasi ya uwenyekiti isipokuwa yeye tu?. NB, amekuwa mwenyekiti kwa takriban miaka 20.

7. Baada tu ya uchaguzi alifanya ziara ya kwanza ikulu, kuonana na kuzungumza na raisi hatuwezi kujua kuwa walizungumza nini zaidi na kukubaliana nini. Je tunashindwaje kuamini kuwa amekosa matumaini juu ya kile kilichompeleka kule na/au makubaliano ya alichokuwa akikitaka yameshindwa kutekelezwa hivyo kuamua kurudia tu matapishi yake?

8. Je kwanini tusiamini kuwa katika ziara hiyo vilevile huenda mambo yaliyojadiliwa ilikuwa ni namna ya kuusambaratisha upinzani na hiki anachokifanya sasa (Kutaka kuureja uwenyekiti) ni sehemu ya mkakati huo?

9. Endapo atafanikiwa kurejeshewa nafasi yake, Je siku ikitokea tena akatofautiana na viongozi wenzake hatajiuzulu na kama hatajiuzulu hatawashughulikia anaotofautiana nao?

11. Amesema ameandika barua ya kutengua uamuzi wake wa awali baada ya kuombwa na kushawishiwa sana na viongozi wa dini pamoja na wanachama wa Chama Cha Wananchi CUF. Je kati ya wakati huu na wakati akijiuzulu ni wakati gani ambao hao wanachama na viongozi wa dini walimshawishi na kumuomba asijiuzulu?.

Wakati ule nakumbuka wanachama na wafuasi walizuia press confference yake mpaka awaambie kwanza kile alichokusudia kuzungumza na waandishi wa habari. Lakini kipindi hiki sijawahi kusikia hata maandamano ya watu kumi kumuomba arejee.

11. Mwisho, Wakati akijiuzulu nafasi ya uwenyekiti alituambia nafsi imemsuta kuisapoti ukawa ambayo imekiuka misingi ya uanzishwaji wake. Je akirudi nafsi haitamsuta kufanya kazi na viongozi wenzake wa CUF na UKAWA aliowaachia kazi ngumu ya uchaguzi na sasa kurejea baada ya kazi hiyo kukamilika?, Je atafanyaje kazi na wa wabunge na madiwani wa CUF na UKAWA ambao akiwa kama kamanda mkuu aliwatelekeza wakati wa mapambano?.

Chama cha wananchi CUF kinapokwenda kufanya maamuzi kuhusu hoja hii ya lipumba, ni muhimu kuwa makini sana na kufanya tafakari ya kina ili kufikia maamuzi yatakayokuwa na afya katika ustawi wa demokrasia na harakati za UKAWA kukamata dola 2020.
Lipumba katumwa na ccm kuja kudhoofisha chana hana jipya wakiingia line wakamrejesha tu wajue CUF ndiyo mwisho wake.
 
Wewe ndiyo kituko kweli kweli wakati Lipumba yupo CUF ilikuwa na wabunge wangapi huku bara na baada kuisaliti CUF imepata wabunge wangapi, au kwa vile unajua kugonga gonga key board basi unajiropokea tu, abakie tu huko CCM hatumtaki tena huku.
Lipumba hana lolote ni njaa inamsumbua baada ya kuishiwa ile pesa aliyopewa na Membe akatoroka Kipindi cha kampeni, Mchepuko wake umembana mpaka kawaendea ccm wampatie pesa za kwenda kudhoofisha CUF na kuvuruga Ukawa, wajanja wa ccm akina January tayari wameomba funga kubwa kwa ajili ya kazi hiyo hiyo huku wakijipanga kupiga pesa kupitia humohumo ( kufa kufaana) Lipumba ataidhoofisha CUF huku wajanja wa ccm wakijinufaisha mara mbili, Yaani watapata pesa pia CUF itagawanyika.
 
Back
Top Bottom