Maswali 11 juu ya ujio mpya wa Lipumba

Aug 20, 2015
24
30
Na, Emmanuel Lukwaro.

Prof Ibrahimu Haruna Lipumba, Aliyekuwa mwenyekiti w Chama Cha Wananchi CUF, na kujiuzulu mwezi November mwaka jana. Ameibuka upya na kusema kuwa amemuandikia katibu mkuu wa chama hicho barua ya kuomba kutengua maamuzi yake ya kujiuzulu na kwamba arejeshwe kwenye nafasi yake ya uwenyekiti.

Prof Lipumba ametamka hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa hababari jijini Dar es salaam. Hata hivyo uamuzi huo wa Lipumba umenisukuma kufikiri na kutafakari kwa kina hatimaye kujiuliza maswali haya 11.

1.Tatizo kubwa na la msingi lililopelekea kujiuzulu kwa mujibu wa maelezo yake lilikuwa Lowasa kujiunga na ukawa,Je lowasa ameshaondoka ukawa? Au akirejeshewa nafasi yake ataitoa CUF UKAWA?

2.Prof Lipumba aliondoka wakati UKAWA wamemkariribisha Lowasa na kumpa nafasi ya kugombea uraisi ambayo naye aliihitaji. Je hakujivuwa uwenyekiti kwa hasira (kususa ) baada ya kukosa nafasi hiyo?

3.Prof Lipumba amekaa nje ya uongozi wa CUF kwa miezi takriban saba.Lakini katika kipindi chote hicho hakuona umuhimu wa kuongezea nguvu upinzani bali wakati huu kuelekea uchaguzi mkuu wa chama. Je huu sio mkakati wa kukivuruga chama na UKAWA?

4.Je kati ya sasa na kipindi cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu ni wakati gani ambao upinzani ulihitaji nguvu ya ziada?
Prof amejenga hoja kuwa anataka kurejea nafasi ya uwenyekiti ili kuuongezea upinzani nguvu katika kipindi hiki.

5.Je Prof Lipumba kama msomi haamini kuwa mwanachama wa kawaida (asiye kiongozi), anaweza kuwa na mchango mkubwa kukijenga chama wakati mwingine kuliko hata kiongozi? au yeye hajazoea kuwa mwanachama wa kawaida?.

6. Je Prof Lipumba haamini kuwa CUF kuna watu wengine wenye uwezo wa kuongoza, hasa nafasi ya uwenyekiti isipokuwa yeye tu?. NB, amekuwa mwenyekiti kwa takriban miaka 20.

7. Baada tu ya uchaguzi alifanya ziara ya kwanza ikulu, kuonana na kuzungumza na raisi hatuwezi kujua kuwa walizungumza nini zaidi na kukubaliana nini. Je tunashindwaje kuamini kuwa amekosa matumaini juu ya kile kilichompeleka kule na/au makubaliano ya alichokuwa akikitaka yameshindwa kutekelezwa hivyo kuamua kurudia tu matapishi yake?

8. Je kwanini tusiamini kuwa katika ziara hiyo vilevile huenda mambo yaliyojadiliwa ilikuwa ni namna ya kuusambaratisha upinzani na hiki anachokifanya sasa (Kutaka kuureja uwenyekiti) ni sehemu ya mkakati huo?

9. Endapo atafanikiwa kurejeshewa nafasi yake, Je siku ikitokea tena akatofautiana na viongozi wenzake hatajiuzulu na kama hatajiuzulu hatawashughulikia anaotofautiana nao?

11. Amesema ameandika barua ya kutengua uamuzi wake wa awali baada ya kuombwa na kushawishiwa sana na viongozi wa dini pamoja na wanachama wa Chama Cha Wananchi CUF. Je kati ya wakati huu na wakati akijiuzulu ni wakati gani ambao hao wanachama na viongozi wa dini walimshawishi na kumuomba asijiuzulu?.

Wakati ule nakumbuka wanachama na wafuasi walizuia press confference yake mpaka awaambie kwanza kile alichokusudia kuzungumza na waandishi wa habari. Lakini kipindi hiki sijawahi kusikia hata maandamano ya watu kumi kumuomba arejee.

11. Mwisho, Wakati akijiuzulu nafasi ya uwenyekiti alituambia nafsi imemsuta kuisapoti ukawa ambayo imekiuka misingi ya uanzishwaji wake. Je akirudi nafsi haitamsuta kufanya kazi na viongozi wenzake wa CUF na UKAWA aliowaachia kazi ngumu ya uchaguzi na sasa kurejea baada ya kazi hiyo kukamilika?, Je atafanyaje kazi na wa wabunge na madiwani wa CUF na UKAWA ambao akiwa kama kamanda mkuu aliwatelekeza wakati wa mapambano?.

Chama cha wananchi CUF kinapokwenda kufanya maamuzi kuhusu hoja hii ya lipumba, ni muhimu kuwa makini sana na kufanya tafakari ya kina ili kufikia maamuzi yatakayokuwa na afya katika ustawi wa demokrasia na harakati za UKAWA kukamata dola 2020.
 
12. Je aliposifiwa na Nape kuhusu uamuzi wake wa kujiengua UKAWA yeye na Dk. Slaa na kuonekana kama sifa hizo alistahili, ina maana aliridhishwa na matamshi yale? je ina maana UKAWA ya sasa hivi ina mabadiliko chanya kuliko ile aliyoiacha kiutendaji? je yeye anataka kuongezea kitu gani ambacho ukawa kimekosekana?
 
Lipumba ndio msomi pekee mwenye maono toka lipumba akae kando CUF imeyumba sana
 
Me huwa najiuliza huyu jamaa anatumika au? Y aliondoka wakat tunapambana? Ananipa mawazo sana aisee
 
Wala asikupe mawazo.hilo jambo liko wazi kabisa kwani inaonekana mshiko alopewa umekwisha au kaagizwa kuja kujua mambo ya ndani kabisa. Nina imani na hekima ya maalim ktk kufanya naanuzi Alito sahihi
 
Unapomwacha mke kwa matusi na kashifa nyingi ooh Hasan ooh mchumba oooh Malaya halafu ukienda kupuyanga huko halafu yakakushinda itakuwaje?so ndo hivyo hivyo? Nisamehe mke wangu shetani alinipitia tu siku zote ninakupenda sana.kazi kweikwei
 
Vipi kuhusu ile tuliskia aliahidiwa atakuwa mshauri wa Rais kwa masuala ya UCHUMI, ndo tuseme ilikuwa ahadi hewa imeota mbawa.?
 
Vipi kuhusu ile tuliskia aliahidiwa atakuwa mshauri wa Rais kwa masuala ya UCHUMI, ndo tuseme ilikuwa ahadi hewa imeota mbawa.?
Ahadi imeota mbawa! Amepewa new assignment ambao anaona bado usaliti tu kama ile mwanzo hakuweza kumtimizia na wamemgeuka sembuse hii! Anajuta! Nadhani angerudi kama mwanachama wa kawaida.....ingempa heshima
 
Sitashangaa na Dr. Slaa akiandika barua ya kuomba kurudi Chadema.
Siasa za nchi hii tamu sana, Dr. Slaa anazimisi kwelikweli.
Muda utasema.
 
Nimegundua Lipumba talalila nyiingi mpambano ulipokuwa mgumu alikimbia sasa anarudi tena , arudi CCM.
 
Na, Emmanuel Lukwaro.

Pr
1. Je Prof Lipumba haamini kuwa CUF kuna watu wengine wenye uwezo wa kuongoza, hasa nafasi ya uwenyekiti isipokuwa yeye tu?. NB, amekuwa mwenyekiti kwa takriban miaka 20.,,,

7. .

Hivi Maprof and Drs (PHds) wanashindwa kupata kazi mbadala wanapoondoka kwenye siasa. Ana tofauti gani na yule RC (PhD) wa Moorogoro aliyeimba RAP za kumwangukia Mkulu amrudishe kazini?

Bygones are bygones lets move forward without an upgraded Prof.

Just throw the bum out.
 
Kwa hilo la kumpinga Lowassa hata mimi namuunga mkono.Haikuwa sahihi kusaidia jitihada za kumfanya fisadi awe rais.
Ila Lipumba kashaongoza muda mrefu awaachie wengine.
 
Na, Emmanuel Lukwaro.

Prof Ibrahimu Haruna Lipumba, Aliyekuwa mwenyekiti w Chama Cha Wananchi CUF, na kujiuzulu mwezi November mwaka jana. Ameibuka upya na kusema kuwa amemuandikia katibu mkuu wa chama hicho barua ya kuomba kutengua maamuzi yake ya kujiuzulu na kwamba arejeshwe kwenye nafasi yake ya uwenyekiti.

Prof Lipumba ametamka hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa hababari jijini Dar es salaam. Hata hivyo uamuzi huo wa Lipumba umenisukuma kufikiri na kutafakari kwa kina hatimaye kujiuliza maswali haya 11.

1.Tatizo kubwa na la msingi lililopelekea kujiuzulu kwa mujibu wa maelezo yake lilikuwa Lowasa kujiunga na ukawa,Je lowasa ameshaondoka ukawa? Au akirejeshewa nafasi yake ataitoa CUF UKAWA?

2.Prof Lipumba aliondoka wakati UKAWA wamemkariribisha Lowasa na kumpa nafasi ya kugombea uraisi ambayo naye aliihitaji. Je hakujivuwa uwenyekiti kwa hasira (kususa ) baada ya kukosa nafasi hiyo?

3.Prof Lipumba amekaa nje ya uongozi wa CUF kwa miezi takriban saba.Lakini katika kipindi chote hicho hakuona umuhimu wa kuongezea nguvu upinzani bali wakati huu kuelekea uchaguzi mkuu wa chama. Je huu sio mkakati wa kukivuruga chama na UKAWA?

4.Je kati ya sasa na kipindi cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu ni wakati gani ambao upinzani ulihitaji nguvu ya ziada?
Prof amejenga hoja kuwa anataka kurejea nafasi ya uwenyekiti ili kuuongezea upinzani nguvu katika kipindi hiki.

5.Je Prof Lipumba kama msomi haamini kuwa mwanachama wa kawaida (asiye kiongozi), anaweza kuwa na mchango mkubwa kukijenga chama wakati mwingine kuliko hata kiongozi? au yeye hajazoea kuwa mwanachama wa kawaida?.

6. Je Prof Lipumba haamini kuwa CUF kuna watu wengine wenye uwezo wa kuongoza, hasa nafasi ya uwenyekiti isipokuwa yeye tu?. NB, amekuwa mwenyekiti kwa takriban miaka 20.

7. Baada tu ya uchaguzi alifanya ziara ya kwanza ikulu, kuonana na kuzungumza na raisi hatuwezi kujua kuwa walizungumza nini zaidi na kukubaliana nini. Je tunashindwaje kuamini kuwa amekosa matumaini juu ya kile kilichompeleka kule na/au makubaliano ya alichokuwa akikitaka yameshindwa kutekelezwa hivyo kuamua kurudia tu matapishi yake?

8. Je kwanini tusiamini kuwa katika ziara hiyo vilevile huenda mambo yaliyojadiliwa ilikuwa ni namna ya kuusambaratisha upinzani na hiki anachokifanya sasa (Kutaka kuureja uwenyekiti) ni sehemu ya mkakati huo?

9. Endapo atafanikiwa kurejeshewa nafasi yake, Je siku ikitokea tena akatofautiana na viongozi wenzake hatajiuzulu na kama hatajiuzulu hatawashughulikia anaotofautiana nao?

11. Amesema ameandika barua ya kutengua uamuzi wake wa awali baada ya kuombwa na kushawishiwa sana na viongozi wa dini pamoja na wanachama wa Chama Cha Wananchi CUF. Je kati ya wakati huu na wakati akijiuzulu ni wakati gani ambao hao wanachama na viongozi wa dini walimshawishi na kumuomba asijiuzulu?.

Wakati ule nakumbuka wanachama na wafuasi walizuia press confference yake mpaka awaambie kwanza kile alichokusudia kuzungumza na waandishi wa habari. Lakini kipindi hiki sijawahi kusikia hata maandamano ya watu kumi kumuomba arejee.

11. Mwisho, Wakati akijiuzulu nafasi ya uwenyekiti alituambia nafsi imemsuta kuisapoti ukawa ambayo imekiuka misingi ya uanzishwaji wake. Je akirudi nafsi haitamsuta kufanya kazi na viongozi wenzake wa CUF na UKAWA aliowaachia kazi ngumu ya uchaguzi na sasa kurejea baada ya kazi hiyo kukamilika?, Je atafanyaje kazi na wa wabunge na madiwani wa CUF na UKAWA ambao akiwa kama kamanda mkuu aliwatelekeza wakati wa mapambano?.

Chama cha wananchi CUF kinapokwenda kufanya maamuzi kuhusu hoja hii ya lipumba, ni muhimu kuwa makini sana na kufanya tafakari ya kina ili kufikia maamuzi yatakayokuwa na afya katika ustawi wa demokrasia na harakati za UKAWA kukamata dola 2020.
Dah!! Maswali kuntu kabisa,profesa thamani na heshima yake inashuka...wasomi wanakosa misimamo
 
Unapomwacha mke kwa matusi na kashifa nyingi ooh Hasan ooh mchumba oooh Malaya halafu ukienda kupuyanga huko halafu yakakushinda itakuwaje?so ndo hivyo hivyo? Nisamehe mke wangu shetani alinipitia tu siku zote ninakupenda sana.kazi kweikwei
Lipumba alijiuzuru uenyekiti, lkn bado alibaki mwanachama mwaminifu kwa CUF
 
Lipumba ndio msomi pekee mwenye maono toka lipumba akae kando CUF imeyumba sana

Wakati akiwa m/kiti alikua na wabunge wawili. Sasa hivi yuko nje ya uzio kuna wabunge tisa. Je nani ameipaisha CUF kati lipu na maalimu aliyebaki kama mpambanaji vitani pekee yake.
 
13.Je aliposema anaachana na siasa , pia anakwenda nchi za nje kujikita kwenye kufanya utafiti ilikuwa ni kweli?
Ameshafanya tafiti ngapi mpaka sasa?
 
Back
Top Bottom