Maswahibu ya utafutaji nikiwa chuoni

Maswahibu ya utafutaji nikiwa chuoni

Bikira23

Member
Joined
May 25, 2020
Posts
18
Reaction score
30
Heshima kwenu wana Jf.

Mimi ni kijana ambaye nimetoka familia ya kipato cha kati yani tutachelewa kula lkn hatuwezi kulala njaa. Ni msichana wa miaka 23 mpaka sasa. Sina mali zaidi ya shamba la nyumbani na vitu vya gheto yani kitanda, godoro, jiko, redio, n.k.

Nimeingia chuoni mwaka 2017, nilikuwa na malengo ya kupata mwanga nikiwa nipo masomoni lakini tuseme niliangukia pua. Nikiwa mwaka wa kwanza nilijiingiza ktk kilimo cha mahindi japo nilitumia resources za nyumbani lkn bado nilikula mweleka. Kulima nililimia ng'ombe za nyumbani na shamba lilikuwa la nymbani. Mi nilinunua tu mbegu mbolea na kukudi vibarua wa kupalilia na kuweka mbolea kuvuna nilivuna mwenyewe. Lakini sikupata mazao kama ambavyo nilitarajia kwani nilichelewa msimu.

Mwaka wa Pili, nikasema sasa sihusishi na kitu chochote zaidi ya kuweka savings ktk pesa yangu ya boom. Aisee ktk hili nashukuru sana Mungu kwani pamoja na kulipa Kodi ya nyumba, ada, na chakula lkn nilifanikiwa kuweka savings ya Tsh 680,000. Nikaenda field nilipo rudi mwaka 3 nikaamua kuanzisha tena goli la kuuza mitumba ya viatu. Nilienda na jamaa angu pale soko la Memorial Moshi nikachukua mzigo wa 500,000 nikakodi meza soko fulani hivi hapa Arusha nilikuwa nalipia 25,000 kwa mwezi. Nikauza kweli nilipata changamoto mwanzoni lkn nilianza kuzoea na maisha yalianza kuendelea vzr. Lkn mbuzi wa masikini hazai na akizaa anazaa dume hilo soko liliungua mwezi machi na katika ya waathirika wa ajari hiyo na mimi nilikuwepo.

Ikumbukwe kipindi hicho tulikuwa tumeangezewa likizo ya CORONA sema kweli nilichanganyikiwa sana. Ila nashukuru Marafiki na familia yangu walikuwa karibu na mimi mpaka nikazoea. Niliamua kwenda nyumbani mkoani Mwanza ili niangaliye maisha mengine. Nilienda nikaanza kufanya biashara ya uchuuzi wa dagaa pale mwalo wa Kayenze ndogo wenyeji wa Mwanza wanapajua vzr. Nilipiga miezi 2 kweli maisha yalienda hata likizo sikuijutia sana.

Matarajio yangu: kwa vile nimebakiza takribani wiki 11 kumaliza chuo nimejipanga kama ifuatavyo nimefanikiwa kukusanya 375,000 mpaka saiv nikiongezea na boom lijalo inaweza kufika 625,000 baada ya kutoa hela ya kumalzia ada na pesa ya chakula kwa muda wa wiki 5. Hiyo pesa nitaenda kuanzia biashara ya kuku huku mkoani Mwanza kuku nakuwa nawatoa mkoa wa Simiyu. Karibu kwa Ushauri na maoni

Nawasilisha
 
Sina wasiwasi na wewe. Ungali mdogo sana. Ukiendelea na moyo huo wa upambanaji utatoboa tu. Cha muhimu usikate tamaa.

Jambo moja. Kabla hujaanzisha biashara zako huko mbele ya safari fanya kiupembuzi yakinifu kidogo kuhusu hiyo biashara. Upate habari zote
muhimu ikiwemo changamoto zake, upatikanaji wa soko na mengineyo. Kama sasa, una uhakika na soko la kuaminika kwa hao kuku?

Kila la heri nsabi (tajiri)
 
Sina wasiwasi na wewe. Ungali mdogo sana. Ukiendelea na moyo huo wa upambanaji utatoboa tu. Cha muhimu usikate tamaa.

Jambo moja. Kabla hujaanzisha biashara zako huko mbele ya safari fanya kiupembuzi yakinifu kidogo kuhusu hiyo biashara. Upate habari zote
muhimu ikiwemo changamoto zake, upatikanaji wa soko na mengineyo. Kama sasa, una uhakika na soko la kuaminika kwa hao kuku?

Kila la heri nsabi
Thanks so much mkuu. Kuhusu kuku nina uhakika wa soko boss ila upatikanaji sijatilia kivilee
 
Chukua piki piki hautajutia, Ila tembesha mwenyewe au fuga nguruwe
Mkuu kwa saaa pesa ya kununua piki sina, saiv nmepanga mpaka namalza chuo nitakuwa na pesa tajwa hapo kwenye uzi lkn bado haitoshi kununua piki piki.
 
Hongera, Pambana, Mimi nilimaliza Chuo Nov 2019 nikiwa na 1M na PC ya 600k, nilifanya uwekezaji nikiwatumia watu wangu wa Karibu nikapigwa 200k, yaani nilijuta sana 200k imepotea kwa siku chache, nilijiingiza kwenye Biashara ya kukopesha nilipoteza 470k, Daaa, sitakagi kukumbuka sabbu nauemiaga sana,

Kwasasa naogopa hata kufanya Biashara, Nina zaidi ya Laki saba benki Lakini siwazi kufanya lolote,. Lakini Hebu Mambo yawe Mambo tuone
 
Ungefanya biashara yako online na hapo sokoni. Unaweka baadhi ya mzigo home
 
Back
Top Bottom