MrFroasty
JF-Expert Member
- Jun 23, 2009
- 1,195
- 592
Masuala mazito yote tuletewe wananchi
Kwa kweli sijuwi kama Msekwa, Makamba na vibaraka vyao wamezidiwa na uzee?Mimi napenda kuamini kama msimamo unaendelea sasa hivi Barazani kutoka kwa ndugu zetu wa CCM, ni msimamo uliokuja kusisitizwa au kutisha wana CCM hapo Zanzibar katika kikao cha Jumapili iliyopita na kuzua msimamo wa kura ya maoni.
Kwanini kura ya moani?CCM Zanzibar (Mkema, Samia) wametumwa waje watwambie kama kila kitu ni lazima kifuate agizo la Butiama.Kama akili zenu zimedumaa na kuwafanyeni mukawa watumwa wa Bara, basi hilo ni tatizo la kiakili na kiafya linaloendelea kuwasibu na itatubidi tuwaombeeni dua mupate afya njema.Maana katika akili zangu mie hoja ya kura ya maoni, haina mshiko.Na ni matumaini yangu kila mwanaadamu na mpenda amani atakubaliana na mimi kuwa matatizo ya migogoro ya uchaguzi hayawezi kutatuliwa na uchaguzi.
Hapa sina maana ya kudharau kazi inayofanywa na ZEC, bali uhalisia wa hili tatizo ni kuwa ZEC ni sehemu moja ya huo mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzibar.Hili nina hakika kuwa munalifahamu, sasa kwa vile mmeshindwa kutueleza hoja za kungangania kura ya maoni.Mimi naomba kutoa masharti au maoni yangu juu ya hii kura itakavyofanyika.Natoa masharti nikijua wazi kuwa mutapinga kwa nguvu zote, kwani malengo yenu ya kukimbilia kwenye kura ya maoni yashafahamika katika jamii ya kizanzibari.Tuna uwezo kuzichambua hizo siasa zenu za kijima zinalenga nini na munataka kutupeleka wapi.Lakini tunaonya kwa maandishi yetu kuwa sisi hatutorudi gizani na kuingia mitafaruku ya wenyewe kwa wenyewe.
Ni imani yangu kuwa wengi wanaoshadidia kura ya maoni watakuwa na sehemu nyengine ya kwenda kuishi, na hivyo hawajali au Amani ya visiwani Zanzibar haina thamani kwao kwa vile wanazo sehemu za kwenda kukimbilia.Sisi wazanzibari hatuna sehemu nyengine, visiwa hivyo ndio sehemu pekee duniani ambayo tunaweza kujiskia kama ndio makwetu.Baada ya kuonesha kama hatuna pa kukimbilia, basi mujue kama hatutokubali kuharibiwa mazingira yetu ya kuishi kwa utashi wenu wa madaraka.Tushasubiri vya kutosha, na ustahamilivu wetu mushauchezea hadi sasa ile mbivu tunayosubiria iko njiani kuharibika.
Kwa vile wana CCM Zanzibar mlipewa ujumbe na vitisho muthamini Butiama na kutupilia mbali Zanzibar na maslahi ya watu wake.Nami nitatoa mashari ya utekelezaji wa kura hiyo:
Masharti ya kutekeleza kura ya maoni:
* Msimamizi wa kura hiyo awe kutoka nje ya Tanzania, ikiwezekana Umoja wa Mataifa.
* Kutokana na hoja ya wana CCM kudai kuwa hili suala la GNU ni zito, na hivyo hawawezi kulitolea maamuzi.Basi kuanzia sasa masuala mazito yote yaletwe kwetu wananchi tuyatolee maamuzi kwa vile kazi imekushindeni humo Barazani.Nitatoa orodha ndogo ya masuala ambayo itawabidi SMZ mutuletee wenyewe wananchi tuyatolee maamuzi
1. Muungano na mfumo wake upelekwe kwa wananchi ukafanyiwe maamuzi kama wanataka Muungano, na kama hawataki watoe maamuzi ni mfumo gani wa serekali wanaopendelea.
2. Wananchi pia tupewe fursa ya kuyajadili masuala mazito kama passport kwa wageni kuingia Zanzibar.
3. Nafasi ya rais wetu wa Zanzibar katika serekali ya muungano (mara baada ya kukubaliwa muungano wenyewe)
4. Na mjadala mzima wa kitu gani kiwe chini ya muungano na kipi kitolewe .
Sisi huku Zanzibar tutafurahi sana kama na hili agizo la Butiama, kama halitokuwa tuu ni kuhusiana na GNU bali pia itabidi maswala mazito yote niliorodhesha hapo juu tuletewe wenyewe wananchi tutie baraka zetu.Kama agizo la Butiama litaweza kufanya hivi basi naona inabidi lienziwe kweli kweli .
GR
Mrfroasty