Masoud Kipanya ana maana gani?

Masoud Kipanya ana maana gani?

Nahisi kipanya kajitunzia akiba ya maneno hivi.....
Akishinda Lowasa, atamfuata na kumwambia vile alivyo mchora na akiamini kwamba yeye ndie King of the Sea.
Na......
Akishindwa Lowasa, ataweza kumfuata mpinzani wa Lowasa na akim-beza kwa kushindwa pamoja na kujiona kama King of the Sea

Kama ulikuwepo hivi teh teh teh
 
Habari kubwa sasa ni uchaguzi.Naona kipanya katuletea matokeo ya kura ya maoni na pia hali halisi baada ya kupiga kura 25/10/2015.kipanya anaona mbali.wacha nikanunue "shampeni".
 
Hii katuni ya Kipanya unaweza andikia kitabu kabisa juu ya kinachoendelea kwenye kampeni na hata uchaguzi wa rais. Kuna jumbe nyingi sana toka katuni hii!
 
Hivyo vi samaki vidogo vya kijivu vinawakilisha akina - Bulembo, Nape, Lusinde, Mwigulu, Warioba, Makongoro nk ambao wametangulizwa kumprovoke huyo papa/samaki mkubwa (Ambaye ni Lowasa). Huyo samaki mdogo wa kijani aneyakaa nyuma nyuma ni Magufuli ambaye anamprovoke Lowasa kwa kujificha sana/kwa mafumbo. Sasa huyu samaki mkubwa/Lowasa anaonekana kuwa na uwezo wa kuwaangamiza hao samaki wadogo wanaomchokoza mbele ya uso wake, lakini anaonekana kutokuwajali/kuwapuuzia samaki hao; Mambo mawili makubwa Kipanya anashangaa; 1. Hawa samaki wadogo wamepata wapi ujasiri wa kumchokoza papa? 2. Kwa nini papa hajali uchokozi huo? Je! Ni uoga au huruma au busara zake tu?
 
Back
Top Bottom