Maskini JK namuonea huruma!

Maskini JK namuonea huruma!

Bra-joe

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
1,846
Reaction score
1,443
Nimekaa na kufikiri nikaona kama Jk ameingia ulingoni kupambana ngumi (kuiongoza Tz) ktk ulingo usiokuwa na muamuzi (raia ambao ni walalamikaji tu) na kocha wake (bunge). Halina mbinu mbadala. Jk kaelemewa sana na mpinzani wake (matatizo yaliyopo nchini) uso wake (wananchi) hautamaniki jinsi ulivyovimba na kutapakaa damu, kocha wake wala hana mpango wa kutupia taulo ulingoni na ni round ya 9, maskini Jk, sijui mwisho wake itakuwaje! Hapa namaanisha Raisi wetu nchi imekwishamshinda na hakuna chombo chochote cha serikali kitakacho mnyang'anya Raisi madaraka mpaka atakapo maliza muda wake (huu ni udhaifu wa muundo wa kuiongoza serikali) wala wananchi hatuna ubavu wa kuingia street kumtoa Raisi, wabunge nao wanaona poa tu Raisi hajiwezi (DHAIFU) lakini hawachukui hatua yoyote kuliokoa Taifa. Nafikiri katiba mpya ni lazima kuwe na kipengele kinachosema kama itaonekana Raisi hajiwezi kuiongoza nchi (DHAIFU) basi aondolewe kikatiba kulinusuru Taifa.
 
Aliulizwa kwa nini nchi ya Tanzania masikini akajibu hata yeye hajui!!!!!!!!!!!!! Mkuu wa kaya huyo!!!!!!
 
Vina panda bei kila siku vitu vinapanda bei x 3.
we mama weeee x 1.
Kajana mmoja anasikika akiimba redioni.
 
Hii hali tuliyonayo kiuchumi kwa sbb ya ufisadi ikimwachwa akiwa kama top wa kutoa kauli,Mi naenda kuomba uraia wa kudumu Sudan Kusini!
 
Kuna vituko duniani wewe ndio wa kumuonea huruma JK..
 
Jionee huruma wewe mwenyewe kabla hujawaonea huruma wengine
 
Hii hali tuliyonayo kiuchumi kwa sbb ya ufisadi ikimwachwa akiwa kama top wa kutoa kauli,Mi naenda kuomba uraia wa kudumu Sudan Kusini!

Tulijua wewe sio raia wa Tanzania hata kabla hujakwenda kwenu Sudan kusini... vita ya wenyewe kwa wenyewe imeisha umeamua kurudi kwenu ulijihifadhi Tanzania kuepuka vita.
 
Hakuna wizara hata moja inayoweza kukupatia picha ya Tanzania itakavyokuwa walau 2014.
Jk Mwenyewe hajui Tanzania itakuwaje japo 2015 zaidi kula perdiem za mamtoni siku zinakwenda. Ingawa ningependa aniambie 2020 Tanzania itakuwa mahali fulani Say Zaidi ya Kenya. Na 2040 tuwe sawa na South Africa. Tuna ongozwa na Vipofu wanaokula na kuondoa Ushahidi.
YES tuna tatizo kama taifa.
Tatizo lipo tena kubwa
NALO TUNA OMBWE LA UONGOZI
 
Amejitakiya hasikilizi,ni muoga mno na ana mapepe anadharau wananchi, muache mpaka atakapoona amefika kikomo atakabidhi nchi kwa wenyewe
 
Kuna vituko duniani wewe ndio wa kumuonea huruma JK..
aliulizwa mbona nchi yako iko gizani hamna umeme akasema Yeye sio Mungu alite mvua,sasa sijui akili yake na upeo wake vimeishia kwamba maji tu ndio yanazalisha umeme?
 
Kuna vituko duniani wewe ndio wa kumuonea huruma JK..

ndiyo yaani kama ni mgonjwa yupo Icu, kazidiwa sana halafu kocha wake hana dalili zozote za kutupia taulo ulingoni.
 
Jionee huruma wewe mwenyewe kabla hujawaonea huruma wengine

nijionee huruma kwa lipi? Yaani huyu jamaa anaomba hata 2015 ingekuwa kesho ili atue zigo linalomshinda, ana hali mbaya sana.
 
kituko kituko.... naunga mkono

Kweli kituko, mkuu wa kaya anashindwa kuongoza nchi halafu wewe unaona poa? Itafika kipindi watanzani itabidi kupimana akili, kwa nguvu utake usitake lazima upimwe.
 
Amejitakiya hasikilizi,ni muoga mno na ana mapepe anadharau wananchi, muache mpaka atakapoona amefika kikomo atakabidhi nchi kwa wenyewe

huenda wakati huo ikawa too late, ni bora akaachia sasa hivi, unakumbuka THB au RTC? ilikuwa hivyo hivyo mpaka maduka yote yakafa.
 
Jionee huruma wewe mwenyewe kabla hujawaonea huruma wengine

kwa hali jk aliyonayo sasa sioni haja ya kuanza kujionea huruma mimi ila yeye kwanza maana kama ni record mbovu kaziweka nyingi sana na sasa imebaki aweke record ya rais wa kwanza Tz kuachia madaraka kabla ya kumaliza muda wake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom