Masikini Sitta, Mwakyembe, Kinana, Nape n.k.

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,952
4,326
Kwa taratibu za vyama vyetu vingi vya siasa, Mwenyekiti wa chama ndiye alfa na omega. Yeye ndiye chama: msimamo wake hauwezi kupingwa na kikao cho chote cha maamuzi katika chama husika. Vikao kama vya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) maamuzi yake shurti yafuate kile ambacho Mwenyekiti anachotaka. Mwenyekiti ndiye CC na ndiye NEC; ndiye Chama!

Haikushangaza kwamba vikao vya CC na NEC vilimsafisha na kumruhusu aendelee na harakati zake za kuusaka umwenyekiti wa chama na uraisi wa nchi kwa utaratibu ule ambao alikuwa alishauanza kitambo uliokuwa umelalamikiwa na wengi, wakiwemo Katibu Mkuu wa Chama, Katibu Mwenezi wa Chama na vigogo wengi tu katika chama.

Kwa utaratibu wake huo aliokwisha jiwekea wa kuusaka uraisi wa nchi na uenyekiti wa chama, wa kutumia nguvu kubwa ya fedha (trions of TShs), sasa hakuna tena kitakachomzuia kupata hizo nyadhifa! Huu ndiyo ukweli. Hakuna kikao cho chote cha chama kitakachokata jina lake na hakuna chama cho chote cha upinzani kitakachomshinda! Usicheze na nguvu ya pesa. Ma- trionairs wa ndani na nje ya Tanzania wamejipanga vizuri nyuma yake kuhakikisha hili linafanikiwa. 'Money can buy anything in this planet except health'

Sana sana kitakachotokea ni kugawanyika kwa hicho chama. Pia Chaguzi kuu zijazo zitakuwa zinatumia mbinu hii. Enzi ya serikali kuwa ya Wanyonge sasa ni jambo lililopita. Tujiandae kisaikolojia, kuna mazuri na machungu tutakayovuna toka kwake.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Kwa taratibu za vyama vyetu vingi vya siasa, Mwenyekiti wa chama ndiye alfa na omega. Yeye ndiye chama: msimamo wake hauwezi kupingwa na kikao cho chote cha maamuzi katika chama husika. Vikao kama vya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) maamuzi yake shurti yafuate kile ambacho Mwenyekiti anachotaka. Mwenyekiti ndiye CC na ndiye NEC; ndiye Chama!

Haikushangaza kwamba vikao vya CC na NEC vilimsafisha na kumruhusu aendelee na harakati zake za kuusaka umwenyekiti wa chama na uraisi wa nchi kwa utaratibu ule ambao alikuwa alishauanza kitambo uliokuwa umelalamikiwa na wengi, wakiwemo Katibu Mkuu wa Chama, Katibu Mwenezi wa Chama na vigogo wengi tu katika chama.

Kwa utaratibu wake huo aliokwisha jiwekea wa kuusaka uraisi wa nchi na uenyekiti wa chama, wa kutumia nguvu kubwa ya fedha (trions of TShs), sasa hakuna tena kitakachomzuia kupata hizo nyadhifa! Huu ndiyo ukweli. Hakuna kikao cho chote cha chama kitakachokata jina lake na hakuna chama cho chote cha upinzani kitakachomshinda! Usicheze na nguvu ya pesa. Ma- trionairs wa ndani na nje ya Tanzania wamejipanga vizuri nyuma yake kuhakikisha hili linafanikiwa. 'Money can buy anything in this planet except health'

Sana sana kitakachotokea ni kugawanyika kwa hicho chama. Pia Chaguzi kuu zijazo zitakuwa zinatumia mbinu hii. Enzi ya serikali kuwa ya Wanyonge sasa ni jambo lililopita. Tujiandae kisaikolojia, kuna mazuri na machungu tutakayovuna toka kwake.

Mungu ibariki Tanzania.

Tatizo wagombea wenu hawakubariki. Mwacheni mwenye maamuz magumu Angie Ikuru. Hatutaki watu wa kulialia saiz.
 
Ni kweli kabisa pesa inaweza kununua karrribu kila kitu, lakini haiwezi kumhonga Mwenyezi Mungu. Wakati huu tutamwomba Mungu aingilie kati mateso na vilio vya Watanzania
 
Nawaomba watu wenzangu kuweni na akili japo kidogo kwa huyo mgombea wenu mnayempigia debe kila saa. ..hamjiulizi tu kweli mtu anayetegemea kuingizwa madarakani na akina Chenge, Karamagi, Rostam, huyu ni mtu wa aina gani? Yaani hamuoni kiasi hicho? Yaani hamna akilo hata kidogo? Ptuuuuu
 
Nadhani n wakat wa kuzungumzia mabadiliko! Nyerere alisema kama mabadiliko hayatapatikana ndan ya ccm wananch watayafuata nje ya ccm! Bado cjaona mgombea mwenye ushawish ndan ya ccm kumzidi lowassa! Mwachen apite huko aje kuchezea kichapo huku kwenye sanduku la maamuzi magumu yakuamua mtawala wa awamu ya tano! Suleiman na fahar zake zote alidondoka,hitler,gaddaf na saddam walidondoka pamoja na ubabe wao ije kua haka ka lowassa!
 
Fisadi papa na jambazi sugu lowasa pamoja na kutumia mihela yote hiyo hasafishiki na wala hakuna anayeweza kumtetea. NI KUPOTEZA MUDA JAPO WATETEZI WATAKUWA WAMENUFAIKA NA PESA ZA KIFISADI ANAZOGAWA HOVYO
 
Ukisikia game iliyochezwa na kina Chenge utabaki mdomo wazi....kuanzia uspika wa mzee sita kwenye mabunge yote,mjadala kuhusu richmond na mzee bila kujuwa game akajiingiza na baadhi ya watu wake na sasa wanamalizika ki siasa kabisa.Wabunge wengi ni Team Lowassa...mawaziri ni wachache saana maana waliaminishwa vingine...Bungeni utadhani kuna msiba...mawaziri hawakai na wanaokaa wananuna na wengine wamepoteza mvuto wa sura siku hizi mbili tatu aliporuhusiwa EL kuendeleza harakati zake za safari ya matumaini.Baadhi ya wanaotia nia ni team EL na watajiondoa na kumuunga mkono.EL akishinda usitegemee mawaziri hawa wa sasa kurudi serikalini.Ukimya wake bungeni alikuwa anawasoma vizuri.Chenge hawezi rudi serikalini sidhani kama anapataka tena.
 
ccm wamekwama. mbele ya lowasa hawapumui. ni vigumu sana kumshinda lowasa ndani ya ccm. ameteka idadi kubwa ya wajumbe wa vikao vya ccm vinavyoshiriki kwenye mchakato wa kumpata mgombea. sio cc, NEC Wala mkutano mkuu.
 
Ni kweli kabisa pesa inaweza kununua karrribu kila kitu, lakini haiwezi kumhonga Mwenyezi Mungu. Wakati huu tutamwomba Mungu aingilie kati mateso na vilio vya Watanzania


Unamuomba Mungu wewe na nani? Hivi unajuwa mda huu kuna watu wanapewa kofia, shati za chama na elfu tano na wameridhika na wapo tayari kumpigia kura huyo usiyemtaka?
Hivi bado hamjawafahamu watanzania wenzenu vizuri eeh!!! Wake up kiongozi, kuna watu ni cheap sio wanawake tu bali hata wanaume, wapo watu wanajongeka na kurubunika kwa 'pipi' tu mkuu...our nation needs deliverance!!
 
Team Membe Mnahangaika. Tatizo jamaa yenu hakubariki.

ndani ya com mwenye kutumia mapesa Mengi atachaguliwa kupeperusha bendera ya CCM. Mamvi na wafanyabiashara wenzake WA-INVEST hela ya kutosha na katika investment yeyote LAZIMA Kuwa na return on investment. Hivyo Watanzania mkae mkao wa kusikia maepa, maescrow kibao pia ukwepaji kodi wa hali ya juu pia walewatakaothubutu na kujulikana kutoa taarifa za siri watajichiwa mbali kimya kimya. Hii NI katika kuhakikisha return on investment :hatari::hatari:
 
Ntaililia tanzania yangu kwa machozi ya damu kama hawa wahuni watakabidhiwa nchi.
 
Nawaomba watu wenzangu kuweni na akili japo kidogo kwa huyo mgombea wenu mnayempigia debe kila saa. ..hamjiulizi tu kweli mtu anayetegemea kuingizwa madarakani na akina Chenge, Karamagi, Rostam, huyu ni mtu wa aina gani? Yaani hamuoni kiasi hicho? Yaani hamna akilo hata kidogo? Ptuuuuu

Na wewe ndugu kuwa na Akili hata kiduchuu , mbona aleyekuwepo sasa kaingizwa na hao hao unaowahofia? ? Rostam , Chenge, Lowasa n.k
 
Back
Top Bottom