Junior counsel
Senior Member
- May 17, 2022
- 191
- 503
Ndugu wanajukwaa, nawasalimu Kwa jina la jamhuri.
Ama baada ya salamu, nichukue fursa hii kuzipongeza timu za Simba na Yanga Kwa kufanikiwa kuanza kampeni zao vyema kwenye hatua ya awali ya mashindano ya klabu bingwa Afrika, Hongereni sana mashabiki wa mnyama na hongereni pia mashabiki wa wananchi.
Baada ya pongezi hizo, Mimi kama shabiki wa Yanga Africans nimekua nikikerwa sana na baadhi ya mashabiki wenzangu wa Young ambao wemekua wakitumia nguvu kubwa kujaribu kumlinganisha mchezaji wetu mpya Azizi Ki na Clatous chota Chama Mwamba wa Lusaka, mtaalam wa locomotive faint.
Tangu ligi kuu Tanzania bara ianze pamoja na mechi za jana za kimataifa, mchezaji wetu Azizi Ki amekuwa sio bora sana hasa ukimlinganisha na Clatous Chama ambae amekuwa na mchango mkubwa katika klabu yake.
Niwaombe wananchi wenzangu tuache kumlinganisha Azizi Ki na Chama, Hii inampa presha kubwa mchezaji wetu. Kwa bongo Chama alishafanya Kila kitu Tena Kwa muda mrefu haliyakuwa Aziz Ki ndo kwanza anaanza kujitafuta.
Mimi ni mwananchi lakini Kwa Africa mashariki na kati Chama ni mchezaji wa daraja la juu Sanaa, hata aliyekuwa msemaji wetu Haji Manara alishawahi kukiri hili zaidi ya mara moja.
Kupata mchezaji mwenye brain ya Chama sio rahisi, pale unapodhani atakimbia na mpira yeye ndo anatembea, unapodhani atafinya yeye ndo atapiga, Wananchi sio rahisi kama tunavyodhani. Kwa sasa tangu ligi ianze ana takwimu bora sana ukimlinganisha na mchezaji wetu.
Azizi Ki ni mchezaji mzuri sana, Kila timu ingetamani kuwa nae lakini Chama ni nora zaidi. Tusimpe presha mchezaji wetu, tumuache acheze mpira, tuache kumlinganisha na Chama, Chama kamzidi mbali sana
Ni hayo tu wananchi
#Timu ya Wananchi
#Daima mbele, Nyuma mwiko
Ama baada ya salamu, nichukue fursa hii kuzipongeza timu za Simba na Yanga Kwa kufanikiwa kuanza kampeni zao vyema kwenye hatua ya awali ya mashindano ya klabu bingwa Afrika, Hongereni sana mashabiki wa mnyama na hongereni pia mashabiki wa wananchi.
Baada ya pongezi hizo, Mimi kama shabiki wa Yanga Africans nimekua nikikerwa sana na baadhi ya mashabiki wenzangu wa Young ambao wemekua wakitumia nguvu kubwa kujaribu kumlinganisha mchezaji wetu mpya Azizi Ki na Clatous chota Chama Mwamba wa Lusaka, mtaalam wa locomotive faint.
Tangu ligi kuu Tanzania bara ianze pamoja na mechi za jana za kimataifa, mchezaji wetu Azizi Ki amekuwa sio bora sana hasa ukimlinganisha na Clatous Chama ambae amekuwa na mchango mkubwa katika klabu yake.
Niwaombe wananchi wenzangu tuache kumlinganisha Azizi Ki na Chama, Hii inampa presha kubwa mchezaji wetu. Kwa bongo Chama alishafanya Kila kitu Tena Kwa muda mrefu haliyakuwa Aziz Ki ndo kwanza anaanza kujitafuta.
Mimi ni mwananchi lakini Kwa Africa mashariki na kati Chama ni mchezaji wa daraja la juu Sanaa, hata aliyekuwa msemaji wetu Haji Manara alishawahi kukiri hili zaidi ya mara moja.
Kupata mchezaji mwenye brain ya Chama sio rahisi, pale unapodhani atakimbia na mpira yeye ndo anatembea, unapodhani atafinya yeye ndo atapiga, Wananchi sio rahisi kama tunavyodhani. Kwa sasa tangu ligi ianze ana takwimu bora sana ukimlinganisha na mchezaji wetu.
Azizi Ki ni mchezaji mzuri sana, Kila timu ingetamani kuwa nae lakini Chama ni nora zaidi. Tusimpe presha mchezaji wetu, tumuache acheze mpira, tuache kumlinganisha na Chama, Chama kamzidi mbali sana
Ni hayo tu wananchi
#Timu ya Wananchi
#Daima mbele, Nyuma mwiko