Mashabiki wa Simba wasingiziwa!!

Mashabiki wa Simba wasingiziwa!!

M.E.M.A

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2013
Posts
1,373
Reaction score
472
Sijui kwa nini vurugu za mechi ya jana kati ya Yanga na Al Ahly zinawaendea moja kwa moja mashabiki wa Simba. Kwa maelezo haya ni wazi wenye vurugu ni mashabiki wa Yanga wakilazimisha kushangiliwa:

" Mashabiki wa Simba na Yanga wakirushiana viti Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo wakati wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga SC na Al Ahly ya Misri. Yanga ilishinda 1-0 na chanzo cha vurugu hizo ni mashabiki wa Simba kuishangilia Ahly. Leo mashabiki wa Yanga waliruhusiwa kwenda kukaa upande wa Simba SC, jambo ambalo lilisababisha vurugu hizo na uharibifu wa viti vilivyong'olewa.".
Source: bin Zubeiry.
 
Sijui kwa nini vurugu za mechi ya jana kati ya Yanga na Al Ahly zinawaendea moja kwa moja mashabiki wa Simba. Kwa maelezo haya ni wazi wenye vurugu ni mashabiki wa Yanga wakilazimisha kushangiliwa:

" Mashabiki wa Simba na Yanga wakirushiana viti Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo wakati wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga SC na Al Ahly ya Misri. Yanga ilishinda 1-0 na chanzo cha vurugu hizo ni mashabiki wa Simba kuishangilia Ahly. Leo mashabiki wa Yanga waliruhusiwa kwenda kukaa upande wa Simba SC, jambo ambalo lilisababisha vurugu hizo na uharibifu wa viti vilivyong'olewa.".
Source: bin Zubeiry.

Acheni kupotosha watu shabiki gani wa Yanga aingie Taifa amevaa jezi ya Simba na akakae jukwaa la Simba, kwa lengo gani hasa.?
 
Leo mashabiki wa Yanga waliruhusiwa kwenda kukaa upande wa Simba SC, jambo ambalo lilisababisha vurugu hizo na uharibifu wa viti vilivyong'olewa.".
Source: bin Zubeiry.
Kwani huo uwanja umejengwa na Yanga au Simba hadi kusiwe na uhuru wa kila mtu kukaa anapohitaji kukaa?

Kwanza kama ungelikuwepo uwanjani ungeliweza kuona uchache wa mashabiki wa Simba kwa siku ile...

Yale majukwaa ambayo huzoeleka kukaa mashabiki wa Yanga kulikuwa kumejaa hadi wengine kusimama...

Sasa kwa mtazamo wako ulitaka wenye timu wasimame nje wakati ndani ya uwanja kuna viti wazi vinavyosemekana ni vya mashabiki wa Simba?
 
Acheni kupotosha watu shabiki gani wa Yanga aingie Taifa amevaa jezi ya Simba na akakae jukwaa la Simba, kwa lengo gani hasa.?

CC: watu8
 
Last edited by a moderator:
Kwani huo uwanja umejengwa na Yanga au Simba hadi kusiwe na uhuru wa kila mtu kukaa anapohitaji kukaa?

Kwanza kama ungelikuwepo uwanjani ungeliweza kuona uchache wa mashabiki wa Simba kwa siku ile...

Yale majukwaa ambayo huzoeleka kukaa mashabiki wa Yanga kulikuwa kumejaa hadi wengine kusimama...

Sasa kwa mtazamo wako ulitaka wenye timu wasimame nje wakati ndani ya uwanja kuna viti wazi vinavyosemekana ni vya mashabiki wa Simba?

Mkuu hebu dadavua point kwanza. Chanzo cha vurugu kwa mujibu wa taarifa hii ni kipi?
 
Mkuu hebu dadavua point kwanza. Chanzo cha vurugu kwa mujibu wa taarifa hii ni kipi?

Sijajua kwa sababu gani umeni cc

Ila kwa tuliokuwepo uwanjani, mashabiki wa Yanga tena tawi maarufu la UBT "Wakali wa Terminal" wakiwa wamevalia mavazi yao nadhifu yenye rangi ya njano na kijani pamoja na bendera yao kubwa, walipiga kambi upande wa kaskazini wa uwanja jukwaa la Orange.

Kitendo hicho kiliwapa hasira mashabiki wa Simba ambao kwa uchache wao wakiwa na jezi nyekundu na nyeupe, walijaza sehemu ya mzunguko viti vya Orange lakini upande wa magharibi ya uwanja.

Mwanzoni kulikuwa na figisu figisu za hapa na pale lakini ni zile za ushabiki wa kawaida tu wa miaka yote.
Mambo yalipadilika baada ya Yanga kupata goli na upande ambao goli lilifungwa ndio huo upande walipokuwa wanazi hao wa timu zote mbili.

Huenda shangilia ya Wakali wa Terminal iliwakera mashabiki wa Simba, maana ghafla walianza kurusha viti hadi pale askari wa FFU waliposogea eneo hilo ndio wakaacha hizo fujo.
 
ahly.jpg
Nafikiri mashabiki wa timu hii ndio waling'oa viti uwanja wa Taifa
 
Sijajua kwa sababu gani umeni cc

Ila kwa tuliokuwepo uwanjani, mashabiki wa Yanga tena tawi maarufu la UBT "Wakali wa Terminal" wakiwa wamevalia mavazi yao nadhifu yenye rangi ya njano na kijani pamoja na bendera yao kubwa, walipiga kambi upande wa kaskazini wa uwanja jukwaa la Orange.

Kitendo hicho kiliwapa hasira mashabiki wa Simba ambao kwa uchache wao wakiwa na jezi nyekundu na nyeupe, walijaza sehemu ya mzunguko viti vya Orange lakini upande wa magharibi ya uwanja.

Mwanzoni kulikuwa na figisu figisu za hapa na pale lakini ni zile za ushabiki wa kawaida tu wa miaka yote.
Mambo yalipadilika baada ya Yanga kupata goli na upande ambao goli lilifungwa ndio huo upande walipokuwa wanazi hao wa timu zote mbili.

Huenda shangilia ya Wakali wa Terminal iliwakera mashabiki wa Simba, maana ghafla walianza kurusha viti hadi pale askari wa FFU waliposogea eneo hilo ndio wakaacha hizo fujo.

Ila taarifa inasema "kurushiana" sio "kurusha". Huoni unakuwa biased mkuu?

Nimeku cc uone hoja ya shabiki mwenzio.
 
Ila taarifa inasema "kurushiana" sio "kurusha". Huoni unakuwa biased mkuu?

Mkuu kwa nini nitegemee taarifa ilihali nilikuwepo uwanjani na kila kitu kilikuwa kinaonekana wazi?
 
Mkuu kwa nini nitegemee taarifa ilihali nilikuwepo uwanjani na kila kitu kilikuwa kinaonekana wazi?

Hahaa..kwa hiyo watani mlikuwa kama 'Yesu'..hamkurudisha?
 
Hahaa..kwa hiyo watani mlikuwa kama 'Yesu'..hamkurudisha?

Kama si busara za mashabiki wa Yanga basi tungelikuwa tunazungumza habari nyingine, hata hivyo haikuwa vurugu kubwa sana maana kuna polisi walifika haraka pale jukwaani na wakaweka ulinzi hadi mwisho wa mchezo...
 
Ila taarifa inasema "kurushiana" sio "kurusha". Huoni unakuwa biased mkuu?

Nimeku cc uone hoja ya shabiki mwenzio.
bado haujadadavua hoja. Suala ni mashabiki gani walin,goa viti? Kwa mfano wewe shabiki wa Simba ukingoa kiti ukamrushia wa yanga,kisha yeye akakiokota na kukurushia. Ni nani hapo aliengoa viti. After all mashabiki wa simba wana CV na rekodi ya kungoa viti kila wakikasirika.
 
bado haujadadavua hoja. Suala ni mashabiki gani walin,goa viti? Kwa mfano wewe shabiki wa Simba ukingoa kiti ukamrushia wa yanga,kisha yeye akakiokota na kukurushia. Ni nani hapo aliengoa viti. After all mashabiki wa simba wana CV na rekodi ya kungoa viti kila wakikasirika.

Kumbe ni habari za rekodi!! Hoja inaanza hivi
1. Mashabiki wa Simba kuishangilia Al Ahyl
2. Mashabiki wa Yanga wananza vurugu
3. Viti vinarushwa.
Kama ni bakora hapa utawachapa wa kundi gani na kuacha lipi?
 
bado haujadadavua hoja. Suala ni mashabiki gani walin,goa viti? Kwa mfano wewe shabiki wa Simba ukingoa kiti ukamrushia wa yanga,kisha yeye akakiokota na kukurushia. Ni nani hapo aliengoa viti. After all mashabiki wa simba wana CV na rekodi ya kungoa viti kila wakikasirika.

Busara hamna hapo mkuu. Yanga na mashabiki wao ni watu wa vurugu na hamna staha ya mchezo. Ninyi mechi na Simba hamkutokea uwanjani kuogopa kipigo ambacho kiliwakuta pia, ninyi mlimtwanga refa makonde. Team yenye busara inakuwa hivi kweli?
 
Kumbe ni habari za rekodi!! Hoja inaanza hivi
1. Mashabiki wa Simba kuishangilia Al Ahyl
2. Mashabiki wa Yanga wananza vurugu
3. Viti vinarushwa.
Kama ni bakora hapa utawachapa wa kundi gani na kuacha lipi?
Umewacha hatua moja muhimu. Naomba uiweke panapostahiki ndipo uulize swala lako. Hatua yenyewe ni ' Yanga wanafunga goli'.
 
Umewacha hatua moja muhimu. Naomba uiweke panapostahiki ndipo uulize swala lako. Hatua yenyewe ni ' Yanga wanafunga goli'.



Kumbe ni habari za rekodi!! Hoja inaanza hivi
1. Mashabiki wa Simba kuishangilia Al Ahyl
2. Mashabiki wa Yanga wananza vurugu
3. Yanga wanafunga goli
4. Viti vinarushwa.
Kama ni bakora hapa utawachapa wa kundi gani na kuacha lipi?

Haya nimetii. Japo kabla yagoli unaona waziwazi waliokuwa wanafanya vurugu ni akina nani.
 
Kumbe ni habari za rekodi!! Hoja inaanza hivi
1. Mashabiki wa Simba kuishangilia Al Ahyl
2. Mashabiki wa Yanga wananza vurugu
3. Yanga wanafunga goli
4. Viti vinarushwa.
Kama ni bakora hapa utawachapa wa kundi gani na kuacha lipi?

Haya nimetii. Japo kabla yagoli unaona waziwazi waliokuwa wanafanya vurugu ni akina nani.
ina maana Yanga walianza vurugu kabla hawajafunga goli. Sawa. Lakini vurugu hizo hazikufikia viti kun'golewa. Sawa. Yanga wanafunga goli. Viti vina'golewa. Huoni kama hiyo inathibitisha unachojaribu kukikataa?
 
ina maana Yanga walianza vurugu kabla hawajafunga goli. Sawa. Lakini vurugu hizo hazikufikia viti kun'golewa. Sawa. Yanga wanafunga goli. Viti vina'golewa. Huoni kama hiyo inathibitisha unachojaribu kukikataa?

Sasa mkuu kinachosababisha hatua hiyo ni goli au mwendelezo wa vurugu wana yanga walizoanzisha!!?
 
Sasa mkuu kinachosababisha hatua hiyo ni goli au mwendelezo wa vurugu wana yanga walizoanzisha!!?
kinachokosekana kwenye hoja yako ni mshikamano ya mitiririko uliyoinukuu. Kama Yanga walianzisha vurugu kabla hata ya kupata goli. Hawakuwa na sababu ya kusubiri hadi goli liingie ndiyo waanze kun'goa viti. Goli pekee haliwezi kuwa kichocheo cha kun'goa viti. Lazima kuna kitu chengine kilichochochewa na kuingia goli, nacho kikachochea kin'golewa viti. Mtiririko wako wa maelezo umevinyamazia vichocheo hivyo. Kwa hivyo maelezo yako yameshindwa kuthibitisha hoja yako, hata kama Yanga wangekuwa ndio walion'goa viti hivyo.
 
Kumbe ni habari za rekodi!! Hoja inaanza hivi
1. Mashabiki wa Simba kuishangilia Al Ahyl
2. Mashabiki wa Yanga wananza vurugu
3. Yanga wanafunga goli
4. Viti vinarushwa.
Kama ni bakora hapa utawachapa wa kundi gani na kuacha lipi?

Haya nimetii. Japo kabla yagoli unaona waziwazi waliokuwa wanafanya vurugu ni akina nani.

Mkuu usiongee nahharia. Kama kweli wewe ni mwanamichezo na ulikuwapo uwanjani basi unapaswa kukemea ushenzi uliofanyika.

Asili ya vurugu: Mashabiki wa UBT walipoamua kukaa nyuma ya goli upande wa screen. Lengo kuu lilikuwa kuumiliki uwanja dhidi ya waarabu ili kuzima kelele zao za ushangiliaji. Hii pia ilikuwa sahihi kwa vile eneo hilo lilikuwa wazi tu. Hizi ni mbinu za kimchezo.

Wahuni wa soka (soccer hooligans) waliovalia sare nyekundu na nyeupe hawakuipenda hali hiyo. Hivyo rabsha zikaanza hata kabla ya mechi kwa wahuni hao kujaribu kuwaondoa mashabiki wa Yanga kwa madai kuwa hilo ni eneo lao la kukaa. Yanga wakagoma, viti vikaanza kurushwa hata kabla mechi haijaanza (timu zilikuwa zikipiga jalamba). Ukweli ni kuwa viti viling'olewa upande wa jukwaa la wekundu na kurushwa kwa mashabiki wa Yanga. Katika hatua ya kushangaza, FFU waliingilia kati na kuanza kuwatandika virungu mashabiki wa Yanga, wakiwataka warudi mpaka eneo lao (nusu ya uwanja). Hali hii ilisababisha manung'uniko kwa vile hii haikuwa mechi baina ya Simba na Yanga. Pia kitendo hiki kilitafsiriwa kuwa ni njama za polisi wetu kuwasaidia wageni ambao huzinyanyasa timu zetuziwapo huko.

Kufuatia malalamiko mengi, Luis Sendeu alimvaa Wambura Boniphace kutaka ufafanuzi kisa cha mwenyeji kunyanyasika nyumbani, na kama hi imechi ni baina ya Yanga na Simba. Ndipo afisa wa juu wa polisi alipowaamuru polisi wasio na uzalendo wawaruhusu yYanga kukaa kwenye viti vilivyo wazi bila vurugu. Yanga wakarudi tena na kuweka bendera zao kwa amani.

Mashabiki wa upande wa pili hawakuridhika na hatua hio, lakini polisi walisimama imara kudhibiti rabsha zoa.

Kasheshe kubwa lilikuja pale goli lilopofungwa. Wakali wa UBT waliokjwa jirani kabisa na wamisri koko wllishangilia kwa furaaaha. hii iliwakera makoko hao, ndipo wakaanza ile tabia chafu walioizoea ya kurusha viti. Hali ilkkuwa mbaya kiasi kwamba wekundu wenye busara aalianza kuwadhibiti wenzao wasiendelee na ushenzi huo.

Maoni:

Yanga akiwa mwenyeji alikuwa na haki zote za kujipangia mbinu za ushindi. Hii hutokea hata kwa timu zingine ambapo wageni hupewa idadi fulani tu ya tiketi.

Pia huu haukuwa mchezo baina ya Simba na Yanga, hivyo hakuna timu yenye hati miliki ya eeeo la kukaa uwanjani. ni upuuzi mkubwa. kuthibitisha hilo, benchi la akiba la Yanga lilikuwa upande unaofahamika kutumiwa na Simba, wala wamisrikoko hawakulalamika.

Kifupi Simba mmetia aibu sana.
 
Back
Top Bottom