Mamndenyi
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 40,587
- 52,261
Na Musa Mataja
Muigizaji ‘brazameni' wa kundi la Orijino Komedi, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji' (pichani) Aprili 17 mwaka huu alibambwa nje ya Uwanja wa Karume, Ilala jijini Dar es Salaam akihubiri Injili laivu na Askofu wake Bruno Mwakibolwa, Risasi Mchanganyiko lina ripoti kamili.
Tukio hilo la aina yake lilinaswa na paparazi wetu pande hizo ambako kulikuwa na mahubiri ya kufikikisha ujumbe kwa waumini waliokuwa wakipita katika eneo hilo.
Msanii huyo alionekana akiwa mstari wa mbele na kuwafanya baadhi ya wapita njia kuacha shughuli zao na kusogea eneo hilo.