MASAHIHISHO: Report ya mchanga ina maswali mengi ya kujibu

Ndugu yangu niseme tu kwa kifupi hili swala mkuu anadhani ndiyo sehemu utakayompa ujiko wa kisiasa lakini kwenye hili kuna possibilty kubwa tumeingia mkenge na hakuna haja kuwabatiza watu kuwa ni madalali au vyovyote vile, pia kwa bahati mbaya sana hayo ndiyo maono ya mkuu wetu.
Lakini lingine naona watu wengi wala hawataki kuhangaisha akili zao ili hata kujua gharama za uzalishaji wa huo mchanga zikoje utadhani huo mchanga ulikuwa kwenye government store kisha Accacia wamekuja na kuuiba tu bila kutumbukiza mtaji wowote wa kiuzalishaji.
Bado nashauri jambo hili linataka busara ya hali ya juu sana kudeal nalo kuliko mihemko iliyopo hivi sasa.
Hawa wazungu sio wajinga wabebe mikontena iliyojaa michanga wakajaze huko kwao!!
Kuna kitu tulifichwa na watawala wetu sasa Leo maovu yao yameanikwa hadharani
Muhongo ye kama pr na mtaalam wa miamba kwa muda aliokaa kwenye hii wizara kuwajibika ni halali kabisa
 
Nakubaliana na wewe kabisa kwa figures akizopewa raisi zinapotosha umma kabisa. Ndiyo maana nasema hata kama ni kwa takribani miaka ishirini tunaibiwa ni kiasi kidogo tu ambacho ni mharaba. Ukisoma vizuri nilichoandika utagundua kuwa mimi na wewe tunakubaliana hata kama hesabu nimekosea kiasi.
Ya ni kweli kabisa nimesoma tena post yako na ni sawa kabisa. Mpaka sasa hivi natafakari namna walivyoihandle issue nzima nashindwa kuwaelewa. Time will tell.
 
Mfumo wa uongozi aliouweka Mkuu wetu wa awamu hii ndio utakaoliingiza taifa hili pabaya. Mkuu amejitahidi na amefanikiwa kuweka mfumo wa watu kuwaona wote wanao-challenge mawazo yake ni wezi, wapiga deal, mafisadi, wala rushwa au wamepewa chochote kile wamkosoe. Huu utaratibu ni mbaya na naona taratibu unaanza kulitafuna taifa.

Sasa hivi ukiongea tofauti na mawazo ya Rais au Serikali yako basi wewe utaonekana ni moja ya watu hao niliowataja hapo juu. Kuna vitu vingi tu sasa hivi Mh. Mkuu anachemka lakini watu (wataalam) wanapiga kimya kwa kuogopa kuonekana hawaitaki mema nchi hii au wamepewa hela (wamehongwa). Hii ni mbaya sana kwa taifa. Ku-challenge (kuhoji) maamuzi au mawazo ya Rais (au Serikali) sio usaliti kwa nchi, ni njia nzuri ya kufanikisha mambo yaende, hatuwezi kufanana mawazo au mitazamo na akiona mnafanana kwenye kila jambo basi ujue anguko lenu limekaribia.

Kwenye taarifa ya jana kuna vitu vimepotoshwa/vimekuzwa lakini watu hawawezi kuviongelea kwa kuogopa kama nilivyosema hapo juu. Mkulu anaposema kwa makontena yale 277 serikali ilkuwa inapoteza mapato kati ya Bil 676 na Trilion 1.147 ya dhahabu sio sahihi.

Hizi ni true value (thamani halisi) ya dhahabu iliyopo kwenye makontena ambayo ikiuzwa, serikali kupitia TRA itachukua kodi/tozo/mrahaba wa 4% kwa sheria ya sasa hivi. Kwahiyo hiyo hela yote sio ya kwetu, sisi tuna % tu ya hela hiyo iliyotajwa. Tatizo lililopo ni kuwa kulingana na taarifa ya tume, thamani halisi ya dhahabu ni ndogo kuliko iliyotajwa hapo mwanzoni. Sasa hili tumelikuza na kuwaaminisha watanzania tumeibiwa kati ya Bil na Trilion wakati si kweli, chetu pale ni 4% ya true value (Bil 676 to Tril 1.147).

Ni kama kwenye biashara zingine tu za uzalishaji, utazalisha soda utauza zile soda, baada ya mauzo halisi ya soda zile kwa thamani sahihi ya soda, ile hela iliyopatikana (gross revenue) itapigwa % kadhaa kama kodi/tozo na mzalishaji atabaki na chake baada ya kodi/tozo (net revenue).

Sasa jana tumeaminishwa ile gross revenue baada ya kuuza zile dhahabu ni yetu yote. Hili tulikosea jana na kuleta taharuki kubwa ya kuonesha kuwa tunaibiwa sana. Ni kweli tunaibiwa lakini tuepuke kukuza mambo.
 
Funga migodi yote hakuna kuchimba chochote na hao wawekezaji waondoke wote!!

Hatuwezi kuchezea nchi na rasilimali zake kama mchezo wa paka na panya.

Hatuwezi kutawaliwa au koloni la wawekezaji kwasababu ya mikataba ya kinyonyaji ya madini!
 
Funga migodi yote hakuna kuchimba chochote na hao wawekezaji waondoke wote!!

Hatuwezi kuchezea nchi na rasilimali zake kama mchezo wa paka na panya.

Hatuwezi kutawaliwa au koloni la wawekezaji kwasababu ya mikataba ya kinyonyaji ya madini!
Haya yote chanzo MZEE BEN NKAPA
 
ukizingatia Dec buzwagi inafungwa.
Wacha tu mkuu migodi ifungwe tuone haya mataahira yatafanya nini? Juzi yamekabidhiwa mgodi wa TULAWAKA yamekula hasara mpaka yamefunga pamoja na kuachiwa mitambo na kila kitu, yameshindwa kuuendesha huo mgodi!!
 
Wacha tu mkuu migodi ifungwe tuone haya mataahira yatafanya nini? Juzi yamekabidhiwa mgodi wa TULAWAKA yamekula hasara mpaka yamefunga pamoja na kuachiwa mitambo na kila kitu, yameshindwa kuuendesha huo mgodi!!
Acha kuongopea serikali. Kwenye ukweli tuseme ukweli, kwenye uongo tukatae, lakini Tulawaka hawajala hasara,ni ishu tofauti. Fatilia ili ujue
 
Funga migodi yote hakuna kuchimba chochote na hao wawekezaji waondoke wote!!

Hatuwezi kuchezea nchi na rasilimali zake kama mchezo wa paka na panya.

Hatuwezi kutawaliwa au koloni la wawekezaji kwasababu ya mikataba ya kinyonyaji ya madini!
Hata ikifungwa sisi ni mataahira hatuwezi kuyachimba. Unakumbuka mgodi wa Tulawaka yaliachiwa kila kitu lakini yameshindwa kuuendesha. Pia wakiondoka wewe hiyo dhahabu yako utauzia wapi? Wenzetu ndo wameshika mpini sisi tumeng'ang'ania makali haki ya nani tutaacha vidole pale!! Hapa kikubwa na kinachotakiwa ni kurudi mezani na kujadili upya hii mikataba angalau iwe pasu kwa pasu!! Yote haya ni matokeo ya mataahira ya CCM tuliyoyapeleka bungeni!!
 
Acha kuongopea serikali. Kwenye ukweli tuseme ukweli, kwenye uongo tukatae, lakini Tulawaka hawajala hasara,ni ishu tofauti. Fatilia ili ujue
Unafikri unapoendesha mradi bila faida hiyo ni nini? Siyo kula hasara huko? Ndugu zako walikuwa wanatumia gharama kubwa kuzalisha kuliko mapato ndo maana wameamua kufunga, fuatilia uone ilikuwaje!!
 
Wacha tu mkuu migodi ifungwe tuone haya mataahira yatafanya nini? Juzi yamekabidhiwa mgodi wa TULAWAKA yamekula hasara mpaka yamefunga pamoja na kuachiwa mitambo na kila kitu, yameshindwa kuuendesha huo mgodi!!
Tulawaka/stamigold inasikitisha sana.
 
Ndugu yangu niseme tu kwa kifupi hili swala mkuu anadhani ndiyo sehemu utakayompa ujiko wa kisiasa lakini kwenye hili kuna possibilty kubwa tumeingia mkenge na hakuna haja kuwabatiza watu kuwa ni madalali au vyovyote vile, pia kwa bahati mbaya sana hayo ndiyo maono ya mkuu wetu.
Lakini lingine naona watu wengi wala hawataki kuhangaisha akili zao ili hata kujua gharama za uzalishaji wa huo mchanga zikoje utadhani huo mchanga ulikuwa kwenye government store kisha Accacia wamekuja na kuuiba tu bila kutumbukiza mtaji wowote wa kiuzalishaji.
Bado nashauri jambo hili linataka busara ya hali ya juu sana kudeal nalo kuliko mihemko iliyopo hivi sasa.
Umesema vema sana mkuu
 
Ilikuwa inalipwa % ya madini ambayo yalikuwa under estimated na baadhi yake hayakuhususishwa kwenye % hizo. Mfano wewe unalipa TRA kodi ya biashara ya unga wa sembe na mtaji wa laki mbili. Na katika biashara uliyokadiriwa unalipa % kwa biashara uliyoisajiri, lakini ukawa unauza unga, Mchele, Ngano, na Mafuta ya kula na biashara ni ya mtaji wa 5millions. Sasa ukishikwa na TRA unaweza ukauliza swali lako hilo la kuwa eti huwa silipi kodi!!?? Unalipa ila unacholipa sicho ulichotakiwa kukilipa.
Hayo madini mengine yapo ila yeye amejikita kwenye biashara moja ya gold na labda copper kidogo ndio maana mgodi unaitwa labda turawaka gold mine sio turawaka gold,uranium,polonium,nickel mine.ni sawasawa wewe uwe unauziwa chapati kwa shilingi mia mbili halafu baadae muuzaji akudai eti mbona kwenye chapati kuna unga wa ngano,mafuta,chumvi hujalipia?
 
Hawa wametuibia kupitia mikataba ya kipuuzi tuliosaini na hapa ndio watatubana.

Alafu taarifa ile ya kamati ilijikita kueleza tu thamani ya yale madini bila kueleza actual cost of production ambayo makampuni yanaingia katika uchimbaji,strorage, usafirsha na gharama ya ku-process mchanga huu uko nje ya nchi.
Mbona huo utetezi wenu bado haujaweza kuonesha kwanini waorodheshe kwa kiwango kidogo na kutooredhesha kabisa aina zingine za madini?yaani kwa hoja zenu sioni uhusiano gharama za uzalishaji na kuweka vielelezo vya kilaghai ,ina maana gharama zikiwa juu unacompesate kwa kufanya ghilba dhidi ya serikali?
Tupisheni tuendelee kuwachenjua hawa watu!
 
Augustine Moshi
Kamati ilifanya kazi yake ya kuonyesha true value ya dhahabu iliyoko ndani ya makinika, lkn ulisikia vizur JPM alovyokuwa anaongea baada ya kukabidhiwa report?? Yeye ndio aliyedanganya umma kwa kusema hiyo hela yote Bil 676 to Tril 1.147 tumeibiwa na hao wenye migodi kwa kushirikiana na wapiga deal na kuleta taharuki kwa kukuza figure tuliyotakiwa kulipwa. Sisi yetu pale ni 4% ya hiyo hela aliyoitaja kwa ujinga wetu wa kusign mikataba mibovu. Sasa jana et tumeaminishwa kwa yale makontena 277 tumeibiwa kati ya bil 676 na Tril 1.147

Ukipiga hesabu ya 4% (ujinga wetu wa mikataba hovyo) chetu pale ni kati ya Bil 19 na Bil 45. Umeona hiyo tofauti hapo??? Hiyo sasa ndio hela nying sana tunayopoteza kuliko hiyo difference between the actual value ya kamati na declared value kabla ya kamati. Sasa hapo mwenye akili ataona tatizo liko wap na waptunapoteza mapato mengi. Mapato mengi yanapotea kwa huu ujinga wa mikataba tuliyosainiana nao inayotupa 4%. Ndo mana tunalia kila siku na kusema turekebishe mikataba yetu (ingawa sio rahis km tunavyofkria, mana tulishasign ana nao kwa ujuha wetu) au tuweke utaratibu flan ambao uyawezesha tusign mikataba yenye tija kwa taifa. Tusipojirekebisha kwny mikataba yetu,,tutaendelea kusign mikatabaya hovyo mpk Yesu anarud. Tuweke itaratibu mzuri so that we can getthe best out of our signed contracts with those Investors (mabepari).

Point yangu ni kuhusu underdeclaration. Huo ndio wizi. Mkuu kataja thamani ya madini kwa fedha. Kwani amesema hiyo ndiyo asilimia yetu?

Uko sahihi unaposema tumeafiki mikataba mibovu. Namwombea Mungu mkuu ili apate nguvu ya kuwashughulikia akina Kafumu, Chenge na Kazirimagi. Wametuliza sana.

Ni ajabu kuna watu wanasema tusingefanya hivi eti kwa sababu ACACIA watakwenda mahakamani. Yaani ukamate mwizi kisha uogope kumthibiti kwa kuogopa mahakama?

Tunao ushahidi wa kisayansi kwamba ACACIA walivunja mkataba. Tuwashitaki kwa underdeclaration.

Siku nyingi tumekuwa tukijiuliza inawezekanaje nchi kama Tanzania na DRC ambazo zina utajiri mkubwa wa maliasili kuwa masikini hivyo? Magufuli katupatia aspect moja ya jibu. May he be blessed.
 
Ovyoooooooo.utafiti hupingwa kwa utafti.lete ba wewe utafti wako.usituletee ngonjera na maigizo hapa.na pia nakuomba usijifiche.jitokeze hadharani kw kupinga kinachafanywa na serikali.HAPA KUNA MAKUNDI MAWILI TUU.(1) KUNA WANAOPINGA UFISADI NA KUPIGANIA MASIRAHI YA NCHI.(2) KUNA MAFISADI NA VIBARAKA WA MAFISADI.WANAOTETEA UFISADI NA KUWAPINGA WANAOPINGA UFISADI.HIVYO JITOKEZE WEWE UKO UPANDE UPI!!!???SECOND JULY

Na wanaopinga ufisadi sasa ni hao hao walioasisi ufisadi na kusaini mikataba ya kifisadi ambayo wanaipinga! Hebu tusaidie kupinga kwa huo unaosema utafiti...Nyie nayi ndio walewale mbugila mbugila.......
 
Mbona huo utetezi wenu bado haujaweza kuonesha kwanini waorodheshe kwa kiwango kidogo na kutooredhesha kabisa aina zingine za madini?yaani kwa hoja zenu sioni uhusiano gharama za uzalishaji na kuweka vielelezo vya kilaghai ,ina maana gharama zikiwa juu unacompesate kwa kufanya ghilba dhidi ya serikali?
Tupisheni tuendelee kuwachenjua hawa watu!

Ndugu, nafikiri unajiandikia tu lakini hujui kwa undani unachoandika. Hivi unaposema vielelezo vya ulaghai, unamsema mwekezajji au unaisema TMAA?? (By the way TMAA ni kitengo cha serikali) unafikiri mwekezaji alikuwa anajikagua mwenyewe na kujiandikia thamani ya hayo madini yaliyokuwa kwenye makontena, kisha anajilipia kodi???? ndivyo unavyofikiri??? Tafadhali tusaidie kujielimisha zaidi ili uandike kitu ukiwa na mwanga wa kutosha kuhusu unachokiandika.
 
Point yangu ni kuhusu underdeclaration. Huo ndio wizi. Mkuu kataja thamani ya madini kwa fedha. Kwani amesema hiyo ndiyo asilimia yetu?

Uko sahihi unaposema tumeafiki mikataba mibovu. Namwombea Mungu mkuu ili apate nguvu ya kuwashughulikia akina Kafumu, Chenge na Kazirimagi. Wametuliza sana.

Ni ajabu kuna watu wanasema tusingefanya hivi eti kwa sababu ACACIA watakwenda mahakamani. Yaani ukamate mwizi kisha uogope kumthibiti kwa kuogopa mahakama?

Tunao ushahidi wa kisayansi kwamba ACACIA walivunja mkataba. Tuwashitaki kwa underdeclaration.

Siku nyingi tumekuwa tukijiuliza inawezekanaje nchi kama Tanzania na DRC ambazo zina utajiri mkubwa wa maliasili kuwa masikini hivyo? Magufuli katupatia aspect moja ya jibu. May he be blessed.

Augustine Moshi
Point # 1:Siku ile kwa masikio ya wote mkuu akitamka hizo Bil 676 mpk Trilion 1.147 ni mapato tuliyokuwa taifa tukipoteza, na zile figure zote za kwny copper, silver zote tulkuwa tukipoteza, kitu ambacho si kweli, tulkuwa tunapoteza 4% ya hizo figures. Na pia alienda mbal kwa kusema madin ya chuma na sulphir oia tumepoteza kias kile, ambaoo pia si kwel chuma na sulphir are not worth extracting so hakuna mrahaba tunaopata.

Point # 2: Sio kosa la ACACIA kwnye suala la under declaration ya kiasi cha madin kilichopo kwny makontena. Serikali kupitia taasisi yake TMAA ndio iliyofanya under declaration coz tulichikua sample, tukapima, tukatoa majib ya kuonyesha kiwango cha dhahabu kikichopo na thamani yake. So hapa unaweza kuona kama zile figure za kias cha dhahabu kilichotolewa na kamati ni sahihi basi kosa lipo kwa TMAA (ambao ndo ss serikali) na sio ACACIA.

Hawa jamaa wanatuibia kupitia kutokujua kwetu, kuwa na technolojia suni na kuwahobga wahusika, so unakuta makosa sio yao kiushahid na kiutetezi coz kila kitu kwa kinaonekana wamefanya sahhihi, haoo ndipo tutakaposhindwa mahakamani.
 
Back
Top Bottom