Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana UVCCM Mkoa wa Mara, Mary Joseph amewataka vijana kuacha kujihusisha na vitendo vinavyochafua picha ya umoja huo, badala yake wawe sehemu ya ulinzi wa amani na mshikamano.
Mary ametoa kauli hiyo leo Machi 24, 2025 alipokuwa akizungumza na vijana katika Wilaya ya Tarime mkoani Mara, baada ya kuhitimisha ziara yake ya kusikiliza za na kuzitafutia ufumbuzi kero za mbalimbali zilizopo mkoani humo.
“Hatuna sababu ya kudanganya kutiana moyo na kukichafua chama kuwa vijana wa Chama Cha Mapinduzi haitupi upendeleo wowote wa kuvunja sheria, kwenda kinyume na taratibu.
“Muhimu tuwe na utaratibu wa kuzingatia sheria bila shuruti kama umeonewa hapo tunaweza kusimama pamoja na kutafuta ufafanuzi, tofauti na hapo tufuate sheria,”amesema Mary.
.
Amefafanua kuwa inawezekana kuna jambo kijana wa CCM anafanya kwa nia njema au kwa kutojua, mwingine akalifanya kwa nia ovu akasingizia ni vijana wa chama hicho kwa sababu walishawahi kulifanya hakuna pa kukwepea.