Marubani wachunguzwa Uchina

MasterMind

Senior Member
Aug 26, 2010
102
0
Marubani wachunguzwa Uchina

Uchina imeanza kuwachunguza marubani wake wote wanaohusika katika safari za ndege za abiria, kufuatia madai kwamba zaidi ya marubani mia mbili walitumia vyeti vyenye maelezo ya uwongo, kuhusiana na ujuzi na maarifa yao ya urubani.

Idara ya safari za ndege iligundua kwamba zaidi ya marubani mia moja waliotoa maelezo ya uwongo walikuwa ni wafanyikazi wa shirika la ndege la Shenzhen, kampuni kuu iliyosimamia shirika la ndege la Henan, ambalo ndege yake ilianguka mwezi uliopita, na kusababisha vifo vya watu arubaini na wawili.

Zaidi ya watu 54 walinusurika baada ya ndege hiyo kukosea njia.
Kati ya mwaka 2008 hadi 2009, inaelekea maelezo kuhusiana na historia ya kikazi ya zaidi ya marubani 200 wanaohusika na ndege za abiria ni ya uwongo, na wengi wakitia chumvi juu ya maarifa yao.

Ripoti hiyo inaelezea kwamba kati ya marubani wanaohusika ni wale waliokuwa wakiendesha ndege za kijeshi, na baadaye kuanza kuendesha ndege za abiria.
Baada ya kugunduliwa, marubani hao wanakatazwa kufanya kazi, hadi watakapokaguliwa na kutahiniwa tena.

Sekta ya safari za ndege nchini Uchina imekuwa ikiimarika kwa kasi mno, na kila mwaka mamia ya marubani uhitajika.


Source: BBC Swahili
 
Hivi rubani akiwa ametumia cheti cha kughushi halafu akawa na rekodi bora maradufu ya kurusha ndege zaidi ya rubani mwenye cheti halali, kuna umuhimu wa kumuandama?

Nafikiri waongeze uangalifu katika kuwapa urubani marubani wapya, na marubani waliopitisha uzoefu fulani waachiwe. Experience is the best teacher, no certificate can make up for hands on experience. Ukifikia uzoefu fulani kazi yako haipimwi kwa cheti chako, inapimwa kwa matokeo ya kazi.
 
Marubani wachunguzwa Uchina

Uchina imeanza kuwachunguza marubani wake wote wanaohusika katika safari za ndege za abiria, kufuatia madai kwamba zaidi ya marubani mia mbili walitumia vyeti vyenye maelezo ya uwongo, kuhusiana na ujuzi na maarifa yao ya urubani.

Idara ya safari za ndege iligundua kwamba zaidi ya marubani mia moja waliotoa maelezo ya uwongo walikuwa ni wafanyikazi wa shirika la ndege la Shenzhen, kampuni kuu iliyosimamia shirika la ndege la Henan, ambalo ndege yake ilianguka mwezi uliopita, na kusababisha vifo vya watu arubaini na wawili.

Zaidi ya watu 54 walinusurika baada ya ndege hiyo kukosea njia.
Kati ya mwaka 2008 hadi 2009, inaelekea maelezo kuhusiana na historia ya kikazi ya zaidi ya marubani 200 wanaohusika na ndege za abiria ni ya uwongo, na wengi wakitia chumvi juu ya maarifa yao.

Ripoti hiyo inaelezea kwamba kati ya marubani wanaohusika ni wale waliokuwa wakiendesha ndege za kijeshi, na baadaye kuanza kuendesha ndege za abiria.
Baada ya kugunduliwa, marubani hao wanakatazwa kufanya kazi, hadi watakapokaguliwa na kutahiniwa tena.

Sekta ya safari za ndege nchini Uchina imekuwa ikiimarika kwa kasi mno, na kila mwaka mamia ya marubani uhitajika.


Source: BBC Swahili

Kumbe makanjanja wapo kila nchi!..huh!...
Ingekuwa ni Tanzania tungeongea hadi kwa lugha za malaika kulaani hii maneno!
All in all, rubani wa ndege ya Abiria anatakiwa kuwa na kiwango cha juu kabisa cha uelewa katika ngazi za urubani ili apate leseni ya commercial, jambo ambalo wengi linawatesa, na hivyo kutafuta njia za mkato!
 
Hivi rubani akiwa ametumia cheti cha kughushi halafu akawa na rekodi bora maradufu ya kurusha ndege zaidi ya rubani mwenye cheti halali, kuna umuhimu wa kumuandama?

Nafikiri waongeze uangalifu katika kuwapa urubani marubani wapya, na marubani waliopitisha uzoefu fulani waachiwe. Experience is the best teacher, no certificate can make up for hands on experience. Ukifikia uzoefu fulani kazi yako haipimwi kwa cheti chako, inapimwa kwa matokeo ya kazi.


Kiranga: experience might be the best teacher, lakini kama mtu anaweza akawa na ujuzi mzuri ambao ni kwa faida ya wengi, kwanini asifuate normal procedures ili kuhakikisha usalama wake na wale anaowabeba, kwa maana kitu chochote ambacho kinahusisha maisha ya wengi ni bora kufuata taratibu halali.

Credibility ya mtu haiji tu kwa uzuri wa kazi anayofanya, lakini pia to the level of honesty or loyalty to his/her profession.
 
China, China

Marubani makanjanja, maziwa ya watoto feki, bidhaa substandard madukani tele, nk, nk - Tujihadhari na wachina!
 
PakaJimmy: Ni kweli, lakini pia mi naona kinacho sababisha pia ni watu kutokuwa wavumilivu.
Wingi wa procedures ama urefu wa procedures unamfanya mtu afikirie kwamba ili kurahisisha mambo basi
afate njia za mkato.....lakini hili si sahihi! mtu lazimwa apimwe kihalali ili ajulikane uwezo wake wa kufaya kazi....si ndio?
 
Naweza uliza swali bei ya mafuta ya ndege na tofauti ya ptrol au diesel?
 
Hivi rubani akiwa ametumia cheti cha kughushi halafu akawa na rekodi bora maradufu ya kurusha ndege zaidi ya rubani mwenye cheti halali, kuna umuhimu wa kumuandama?

Nafikiri waongeze uangalifu katika kuwapa urubani marubani wapya, na marubani waliopitisha uzoefu fulani waachiwe. Experience is the best teacher, no certificate can make up for hands on experience. Ukifikia uzoefu fulani kazi yako haipimwi kwa cheti chako, inapimwa kwa matokeo ya kazi.
Na hapo ndo huwa watu wengi wanakosea sana..
 
Back
Top Bottom