Albedo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 5,559
- 1,452
Yaani kila inachofanya CCM bwana Marmo anakibariki na kuwa ni Sehemu ya Maisha au Kanuni za Uchaguzi, kaaazi Kweli kweli
Marmo aruhusu vyama vya siasa kampeni ya nyumba kwa nyumba
Na Muhibu Said
19th June 2010
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Philip Marmo.
Serikali imesema vyama vya siasa vinaruhusiwa kufanya kampeni nyumba hadi nyumba na kuorodhesha majina ya watu walioandikishwa, lakini haviruhusiwi kuchukua kadi za wapigakura.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Philip Marmo, alisema hayo wakati akijibu hoja za wabunge waliochangia mjadala wa hotuba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuhusu mapitio na mwelekeo wa kazi za serikali na makadirio ya matumizi ya fedha ya ofisi ya Waziri Mkuu na ofisi ya Bunge ya mwaka 2010/11, bungeni jana.
Wabunge waliochangia eneo hilo, ni pamoja na Dk. Willibrod Slaa (Karatu-Chadema), Mgana Msindai (Iramba Mashariki-CCM), Masoud Abdallah Salim (Mtambile-CUF), Lucy Owenya (Viti Maalum-Chadema) na Ismail Jussa Ladhu (Kuteuliwa na Rais-CUF), ambao baadhi yao waliitaka serikali itoe tamko kukemea viongozi wa CCM kuwafuata wananchi majumbani na kuorodhesha kadi za wapigakura na kuandika namba zake kwenye fomu maalum.
Waziri Marmo alisema wajumbe wa vyama vyote vya siasa wanaruhusiwa kuwafuata wananchi na kuwahamasisha katika kuwashawishi ili wawapigie kura na kufanya kampeni nyumba hadi nyumba.
Alisema sheria za uchaguzi hazikatazi vyama kuorodhesha majina ya watu walioandikishwa na kwamba, kinachokatazwa ni kuchukua kadi za wapigakura.
Kutokana na hali hiyo, alisema iwapo kuna vyama vinavyochukua kadi za wapigakura, taarifa ya suala hilo itolewe ili hatua zinazostahili zichukuliwe.
Kuhusu madai katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Biharamulo, mkoani Kagera na ule wa Busanda, mkoani Mwanza, uliofanyika mwaka jana, kwamba kadi za wapigakura zilichukuliwa kwa nguvu, alisema taarifa zilipelekwa polisi na baada ya uchunguzi, walibaini kuwa waliolalamikiwa walikuwa wameorodhesha majina tu ya wanachama wao na hawakuchukua kadi yoyote ya mpigakura na kwamba, kwa kuwa kuorodhesha majina siyo kosa, watu hao waliachiwa.
Alivitaka vyama vya siasa vyenye wajibu wa kuteua wagombea, kuteua wanawake wengi na kwamba serikali itaendelea kuvishauri kuwa kwa sasa lengo la serikali ni kwamba, asilimia 40 ya watakaokuwa wabunge katika Bunge lijalo, ni wanawake.
Kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa kuondolewa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na kuwekwa chini ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Marmo alisema jambo hilo kwa sasa haliwezekani.
Alisema Katiba ya nchi imeipa NEC mamlaka ya kusimamia uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani Tanzania Bara, hivyo haina mamlaka ya kusimamia uchaguzi kwa serikali za mitaa.
Alisema uchaguzi huo unasimamiwa na Halmashauri husika chini ya Tamisemi kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za mitaa namba 7 na 8 za Mwaka 1982 na kwamba, serikali inaamini utaratibu huo unakidhi haja na utaendelea kutumika.
Kuhusu NEC kutoa taarifa zaidi ili kuepusha ubambikiaji wa kesi kwa viongozi wa vyama vya siasa wakati wa uchaguzi, alisema kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi sura ya 343, imepewa mamlaka ya kuandaa maadili ya uchaguzi baada ya kushauriana na vyama vya siasa na serikali.
Waziri Marmo alisema hivi sasa NEC iko katika mchakato wa kuandaa maadili hayo na kwamba, pamoja na mambo mengine, maadili yanakataza ubambikiaji wa kesi wakati wa uchaguzi.
Alisema maadili hayo yakishakamilika, itatangazwa kwa wadau wote ili yaweze kufahamika na kwamba, vyama vyote vya siasa, serikali ikiwamo, vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na NEC, watawajibika kutekeleza maadili hayo kwa baadaye.
Kuhusu serikali kukemea lugha chafu wakati wa uchaguzi, alisema inakatazwa na sheria za uchaguzi na kwamba, serikali itachukua hatua kwa atakayekiuka maadili hayo.
CHANZO: NIPASHE
Marmo aruhusu vyama vya siasa kampeni ya nyumba kwa nyumba
Na Muhibu Said
19th June 2010
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Philip Marmo.
Serikali imesema vyama vya siasa vinaruhusiwa kufanya kampeni nyumba hadi nyumba na kuorodhesha majina ya watu walioandikishwa, lakini haviruhusiwi kuchukua kadi za wapigakura.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Philip Marmo, alisema hayo wakati akijibu hoja za wabunge waliochangia mjadala wa hotuba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuhusu mapitio na mwelekeo wa kazi za serikali na makadirio ya matumizi ya fedha ya ofisi ya Waziri Mkuu na ofisi ya Bunge ya mwaka 2010/11, bungeni jana.
Wabunge waliochangia eneo hilo, ni pamoja na Dk. Willibrod Slaa (Karatu-Chadema), Mgana Msindai (Iramba Mashariki-CCM), Masoud Abdallah Salim (Mtambile-CUF), Lucy Owenya (Viti Maalum-Chadema) na Ismail Jussa Ladhu (Kuteuliwa na Rais-CUF), ambao baadhi yao waliitaka serikali itoe tamko kukemea viongozi wa CCM kuwafuata wananchi majumbani na kuorodhesha kadi za wapigakura na kuandika namba zake kwenye fomu maalum.
Waziri Marmo alisema wajumbe wa vyama vyote vya siasa wanaruhusiwa kuwafuata wananchi na kuwahamasisha katika kuwashawishi ili wawapigie kura na kufanya kampeni nyumba hadi nyumba.
Alisema sheria za uchaguzi hazikatazi vyama kuorodhesha majina ya watu walioandikishwa na kwamba, kinachokatazwa ni kuchukua kadi za wapigakura.
Kutokana na hali hiyo, alisema iwapo kuna vyama vinavyochukua kadi za wapigakura, taarifa ya suala hilo itolewe ili hatua zinazostahili zichukuliwe.
Kuhusu madai katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Biharamulo, mkoani Kagera na ule wa Busanda, mkoani Mwanza, uliofanyika mwaka jana, kwamba kadi za wapigakura zilichukuliwa kwa nguvu, alisema taarifa zilipelekwa polisi na baada ya uchunguzi, walibaini kuwa waliolalamikiwa walikuwa wameorodhesha majina tu ya wanachama wao na hawakuchukua kadi yoyote ya mpigakura na kwamba, kwa kuwa kuorodhesha majina siyo kosa, watu hao waliachiwa.
Alivitaka vyama vya siasa vyenye wajibu wa kuteua wagombea, kuteua wanawake wengi na kwamba serikali itaendelea kuvishauri kuwa kwa sasa lengo la serikali ni kwamba, asilimia 40 ya watakaokuwa wabunge katika Bunge lijalo, ni wanawake.
Kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa kuondolewa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na kuwekwa chini ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Marmo alisema jambo hilo kwa sasa haliwezekani.
Alisema Katiba ya nchi imeipa NEC mamlaka ya kusimamia uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani Tanzania Bara, hivyo haina mamlaka ya kusimamia uchaguzi kwa serikali za mitaa.
Alisema uchaguzi huo unasimamiwa na Halmashauri husika chini ya Tamisemi kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za mitaa namba 7 na 8 za Mwaka 1982 na kwamba, serikali inaamini utaratibu huo unakidhi haja na utaendelea kutumika.
Kuhusu NEC kutoa taarifa zaidi ili kuepusha ubambikiaji wa kesi kwa viongozi wa vyama vya siasa wakati wa uchaguzi, alisema kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi sura ya 343, imepewa mamlaka ya kuandaa maadili ya uchaguzi baada ya kushauriana na vyama vya siasa na serikali.
Waziri Marmo alisema hivi sasa NEC iko katika mchakato wa kuandaa maadili hayo na kwamba, pamoja na mambo mengine, maadili yanakataza ubambikiaji wa kesi wakati wa uchaguzi.
Alisema maadili hayo yakishakamilika, itatangazwa kwa wadau wote ili yaweze kufahamika na kwamba, vyama vyote vya siasa, serikali ikiwamo, vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na NEC, watawajibika kutekeleza maadili hayo kwa baadaye.
Kuhusu serikali kukemea lugha chafu wakati wa uchaguzi, alisema inakatazwa na sheria za uchaguzi na kwamba, serikali itachukua hatua kwa atakayekiuka maadili hayo.
CHANZO: NIPASHE