Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,436
Akizungumza na vyombo vya habari mwanzilishi wa mtandao huo Mark Zuckerberg,, amewakosoa vikali wale ambao wanatoa wito kampuni hiyo ifungwe, akiongeza kuwa wanafanya kila wawezalo kukabiliana na changamoto zinazoibuka.
"Sidhani kama suluhisho ni kuifunga kampuni kwasababu tunashughulikia hili tayari na ni changamoto za kibiashara", amesema Zuckberg.
Karibia watumiaji 150,000 walifunguliwa akaunti zao baada ya kubainika kuwa hawakukiuka sheria kipindi hicho.
Facebook imesema ripoti hiyo imeangazia masuala hayo ili kuendesha huduma zake kwa njia ya uwazi na uwajibikaji ili kuufanya mtandao huo kuwa salama kwa wateja wake.