Maria Sarungi: Tofauti na wakoloni, watawala wetu hawana pa kwenda hawatambui kuwa ‘Kwao ni Kwetu’

Tangu mwingereza atawale mpaka anaondoka alikuwa na kesi moja tu ya Nyerere, hata hivyo hakuteswa na watu waliruhusiwa kuisikiliza na alishinda huku kukiwa hakuna maelekezo yoyote toka kwa Malkia au Gavana. Watanganyika walifanya siasa bila kubugudhiwa na polisi, na walikuwa huru kutoa maoni yao ndiyo sababu Nyerere akienda UNO aliweza kusindikizwa uwanja wa ndege na kupokelewa arudipo.
Zipo nchi zilizokataa uhuru na wanaishi kwa raha kuliko waliopata uhuru na kujikuta wanatawaliwa vibaya zaidi.
 
Huyo sio bright ni jasusi anayetumiwa na hao mabeberu. Kabla ya hayati Rais Magufuli kuingia madarakani huyu dada alikuwa akipiga sana fedha kutoka serikali lakini JPM alipoingia madarakani alikata mirija yote sasa ndio akaanza kujiita mwanaharakati mbona kabla 2015 hatuwahi kuona huo uharakati wake ?
 
Shingo yako imebeba dafu!
Hao kina maria uwa wanakua against na utawala ambao umewatupa wao wenyewe ama wazazi wao,huyo akirudishwa kwenye system ya kula keki ya taifa ataufyata kama alivyoufyata kigogo baada marope kurudi kwenye system
 
Huyu binti watu wampuuze wana damu na asili ya kuvuruga nchi..Baba yake akiwa waziri wa elimu alimsomesha nje ya nchi, huku halafu akaamua kuvuruga elimu ya nchi, akavuruga mitaala hasa hasa masomo ya sayansi aliunganisha masomo ya chemisty biology na phyisic likawa somo moja

Alifuta michezo na utamaduni mashuleni ndio sababj mpaka leo nchi imerudi nyuma sana kwenye michezo ya riadha, na ndondi ambayo tulikuwa tupo level moja na kenya na ethiopia wakati huo

Ndio aliosababisha michezo mimgine yote kama volleyball basketball imefutika na watu kuwa addicted na soka hasa simba yanga maana kuanzia mtoto anazaliwa haoni kiwanja wala tv inayotangaza mchezo mwingine zaidi ya soka hivyo hata kama angekuwa na kipaji kingine kinafutika anajilazimishia soka aliyoikuta na aliyoanza kununuliwa jezi zake tangu akiwa kinda
 
Hawawezi kukuelewa kama tulivyokua tunawaambia enzi za kigogo wakawa wanatutukana,kigogo now watu wake wamerudi kwenye system kawageuka,siku maria akiwa kwenye ulaji atawageuka na wataanza kumtukana kama wanavyomtukana kigogo now
 
Usimvhanganye na Makweta aliyevuruga elimu, huyu alikuwa waziri wa afya na ulinzi.
 
Hao kina maria uwa wanakua against na utawala ambao umewatupa wao wenyewe ama wazazi wao,huyo akirudishwa kwenye system ya kula keki ya taifa ataufyata kama alivyoufyata kigogo baada marope kurudi kwenye system
Wewe ni tatizo kweli...

Iweje uwe na fikra za namna hii wakati kilichopo mezani ni hoja?

Umeona taabu kujadili mantiki iliyo ktk hoja badala yake unaanza kumwangalia na kumjadili mtu...???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…