Marekani yamuweka Magufuli njiapanda

Marekani yamuweka Magufuli njiapanda

Katika suala la misaada kutoka mataifa Tajiri kwa nchi za Africa alikwepeki.
Hata kama wakikitoza kodi hadi pesa zako zote zilizomo kwenye kibubu chako bado huna ujanja wa kutotegemea misaada ya nje.
Muulize Mugabe atakwambia

Kwa hiyo unashauri nini??!!!
 
Uhuru upi mlioingiliwa!.Au 'UHURU' wa bendera?

Jinga kabisa


unaonekana una mawazo ya kitumwa kabisa na kupenda kusaidiwasaidiwa, hivyo vi misaada vyao wala huwa havitusaidii chochote, kutafuta namna ya kutotegemea vijisenti vyao ni swala la lazima kama ww huoni hili lazima uwe na tatizo
 
Kama kwa mwezi tunaweza kukusanya trilioni moja. Dadeki wakae na milleniuma yao huko wapeleke sudani mattako yao
 
Kama kwa mwezi tunaweza kukusanya trilioni moja. Dadeki wakae na milleniuma yao huko wapeleke sudani mattako yao
Ni kweli mkuu..sasa inabidi isomeke hivi..JPM aiweka Marekani njiapanda
 
Maalim apishwe mara moja.

Ye ndio atapeleka umeme vijijini??!!!
Zinatakiwa njia endelevu za kuenedeleza nchi sio hizo "ransom" kwa jina la kunyimwa misaada sijui kuwekewa vikwazo. . . . . . .

Yaani maisha ya watu woote yasubiri kuapishwa mtu mmoja. . . . . . .
 
Namna nyingine tena?kuzoa taka tu shida zimezagaa kila mahali.Msaada ni muhimu panapohitajika angalia sasa hivi umeme vijijin unavyoenda sababu ni hiyo misaada tu.
 
Kwa hiyo tukose trillion moja na nusu kwa sababu CCM hawataki kushindwa? We ni juha nini?

Mambo yetu ya ndani tutayamaliza wenyewe na ya kwao hatuyangilii. Hao wazungu ni ndumilakuwili kule kwa Kagame na Museveni hakuna demokrasia na wananchi wao wana maisha mazuri lakini wameambiwa shut up kwa kuwa hawaombiombi. Wewe ni kati ya wale waliozoea kutembea na bakuli. Aibu yenu!
 
Ndiyo zao hao wana mind kuona Tz ina kiongozi anayeweza kujisimamia.Tukikomaa kusimamia ukusanyaji wa mapato na matumizi sahihi ya rasilimali hatuna haja ya misaada yao zaidi sana masisi tutakuwa doners
 
Marekani imeiweka njiapanda Serikali ya Rais Dk. John Magufuli, baada ya Bodi ya shirika lake la Changamoto za Milenia (MCC) kuamua kukutana kesho kujadili masuala kadhaa ya utoaji wa misaada kwa nchi zinazoendelea huku angalizo lake kwa serikali ya Tanzania kuhusiana na uchaguzi wa Zanzibar likiwa bado halijapatiwa ufumbuzi.


Tofauti na fedha zinazotolewa na wafadhili wengi duniani, fedha za MCC hazitakiwi kurudishwa na nchi inayopewa fedha hizo na pia nchi husika hupewa uhuru wa kuchagua aina ya miradi ya maendeleo ambayo inataka igharimiwe na fedha hizo.

Katika fedha za awamu ya kwanza za MCC, Tanzania ilipata dola za Marekani milioni 698 (Sh.trilioni 1.46), ambazo tayari zimesaidia kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwamo ya barabara na usambazaji wa umeme vijijini


CHANZO:
NIPASHE


Nadhani awamu ya Kwanza ya pesa hizi TZ itakuwa imeikosa!




 
Kwani mpaka leo bado hawajaisoma namba hao wamarekani na vipesa vyao uchwara? waendelee kutusubiri 2030 tutakwenda kuwatembelea na kuwasalimia lakini si kwa kuwaomba visenti vyao vya wizi na mizengwe
 
Hiyo trillion moja tumekwisha kuipata kwenye makontena yaliyotoroshwa. Na bado tukibana mianya yote ya ukwepaji kodi na ufisadi hatuhitaji misaada yenye masharti ya kipuuzi. Mbona Mugabe amewatolea nje na bado anadunda!

Ni kama kweli ila kumbuka Mugabe ni Mugabe na Magu ni Magu,
 
Trilioni moja tuna uwezo nayo kama vipi waende tu.Kama mizigo yenye Thamani ya 836bilioni iliingia sokoni bila kulipa kodi wafanyakazi wafanyaniashara wakidai ilikuwa iko on transit.

alokwambia serikali inaendesha miradi ya maendeleo nani,,tena ukae kimya kama huna cha kusema ,,nenda kijijini utaelewa,,,tunazitaka hizo hela kwa maendeleo ya mskini vijijini,,,tena zitafanya kazi vizuri maana usimamizi wa sasa mzuri nyuma zilikua zinaliwa sana
 
kodi ya trilioni moja kwa yale makontena labda kama yalikuwa yamebeba dhahabu! acheni kukuza mambo

Ukweli utatuweka huru kua TZ baado sana kukataa misaada ya wahisani. au siyo mkuu??? Kama kaokoa ziko wapi sasa?? Tujitahidini tu kumaliza migogoro ila tuendelee mbele kama Taifa
 
Magufuli asimamie kodi zaidi kuliko kutegemea miisaada. Kenya walifanyiwa hivyo miaka ya nyuma, wakaamua kukusanya kodi ya kutosha kuendesha serikali na kulipia miradi ya maendele, halfu wahisani hao wakarudi wenyewe
Hili ndio LA muhimu, kuendelea kutegemea misaada mpaka lini???
 
Naamini tunaweza bila misaada yao,

Pia ni muda sasa wa Tanganyika kuiachilia Zanzibar,
Kuipa uhuru wake.


Mstari wako wa kwanza naupinga kidogo ila wa pili naupendaaaaaaaa sana. Tuliungana nchi hizi zikiwa huru ila kwa sasa nikama zenji imekua kamkoa flani hivi kweli kanakopuuziwa haki yake ya msingi kisa uroho wa madaraka. Its time now.
 
Back
Top Bottom