Mnhhh inawezekana?
Iran unaamini angeweza kununua silaha kwa Marekani?
Inawezekana sana tu, kabla ya Iranian Revolution Shah of Iran alikuwa ni rafiki mzuri sana wa America na silaha zote alinunua huko. Baada ya mapinduzi Iran ikawekewa embargo pamoja na PACIFIC BLOCKADE. Hii ndiyo chanzo cha Iraq- Iran War ambapo Raegan alimpa SCUD Missile na Strategic weapons nyingi Sadam ili awatwange Iran bali Sadam naye akawageuka.
Kinachoendelea Iran ni suala zima la Big power politics. Inasemekana Iran akifanikiwa kutengeneza Nuclear Grade Weapons basi kuna likelihood ya nchi nyingi pamoja na makundi kama Hezbollah yanaweza kuwa radicalized zaidi ya hapa.
Hii ni hatari kwa Usalama wa Israel na Saudi Arabia.
Ikumbukwe Iran ni mdau mkubwa sana wa kibiashara wa Urusi na Uchina. China anategemea mafuta ya Iran, sasa kwa kipindi hiki ubabe hauwezi kufanya kazi kwasababu kutakuwa na Nuclear Proliferation ambayo ni Unprecedented. For now the world doesn't need a new North Korea.
Urusi na Marekani wamesaini mikataba Mingi sana ya kuzuiana wao kwa wao wasisambaze silaha za Kinyuklia kwa mataifa wadau wao. Endapo ubabe ukitumika na Marekani asijali Maslahi ya Uchina na Urusi unadhani ni nini kitawazuia Warusi kuwasaidia Iranians kuzalisha Nuclear Grade Weapons?
Hili hata Henry kissinger , Brehzinsk , Ash Carter, Clinton na wengine wengi wanalijua.
Kama una kumbukumbu nzuri Republicans wao wenyewe walishawahi kutumia mkakati kama huu mwaka 1972. Nixon baada ya kuona Uchina inakuwa na nguvu na inatengeneza silaha za Kinyuklia na inatishia sana mataifa rafiki wa Marekani kama South Korea, Japan, Philippines na India. Akaamua kwenda kuwafuata huko huko kwao akisingizia anaenda kutembelea THE GREAT WALL OF CHINA.
Kule Uchina Nixon aliwaahidi Wachina kwamba Sera ya Marekani ya mambo ya nije itabadilika na atamfungulia masoko ya kibiashara endapo tu Uchina itabadilisha mtazamo wake juu ya mataifa jirani. Nuclear Proliferation iliishia pale pale.
Mwaka 1972 kama una kumbukumbu nzuri Uchina Walirudishwa UN na wakapewa na VETO huku TAIWAN alifukuzwa. Hujiulizi kwanini Marekani aliamua kuwa mpole???
Mwisho kabisa hivi hujajiuliza kwanini Ronald Raegan na ubabe wake wote hakuwahi vamia CUBA ambao ni majirani zake kabisa???
Au unadhani European Refugee crisis imetokea tu out of thin Air?? Vita nyingine ikitokea middle east unadhani Ulaya itakaa salama ndugu yangu??
Hivi unadhani Wazungu watamsapoti Marekani kwenye vita ambayo moja kwa moja itahatarisha Usalama na uchumi wao kama ilivyo sasa????
Now the answers are simple..
1) Big power politics
2) Threat of Nuclear Proliferation
3) Escalation of World terrorism
4) European Security Concerns
"EVALUATE YOUR BATTLES CAREFULLY SOMETIMES PEACE IS MORE IMPORTANT THAN BEING RIGHT"
Marekani ni taifa kubwa sana na maamuzi yake yanaathiri dunia nzima.
Hebu tusipende kufurahia vita sana nimekaa hapo Sudan Kusini sijapenda kabisa mazingira ya vita hata kidogo.
Nakushauri usipende kushabikia machafuko.