Marekani: Rais Joe Biden aomba msamaha kwasababu ya wanajeshi kulala eneo la kuegesha magari

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
2,207
4,703
Rais Joe Biden wa Marekani ameomba msamaha baada ya baadhi ya wanajeshi waliokuwa wamewekwa kulinda eneo la Capitol kupigwa picha wakiwa wamelala katika eneo la kuegesha magari.

Zaidi ya wanajeshi 25,000 walipelekwa Washington DC kwa ajili ya kushughuli ya kuapishwa kwake mapema mwezi huu.

Picha walizopigwa maafisa hao zilianza kusambaa mtandaoni Alhamisi zikiwaonesha wakiwa wamepumzika katika eneo la karibu la kuegesha magari wabunge waliporejea.

Hali hiyo ilisababisha hasira miongoni mwa wanasiasa huku baadhi ya magavana wakawaondoa wanajeshi wao kwasababu ya utata huo.

Bwana Biden alizungumza na mkuu wa jeshi la kulinda usalama wa taifa Ijumaa, kuomba msamaha na kuuliza ni kipi ambacho kingekuwa kimefanywa kuweka mambo sawa, kulingana na vyombo vya habari vya Marekani.

Mama wa taifa Jill Biden pia naye alitembelea baadhi ya vikosi hivyo kuwashukuru akiwa amewabeba biskuti kutoka Ikulu kama zawadi.

"Leo hii nilitaka tu kuja na kuwashukuru kwa kutulinda mimi pamoja na familia yangu," alisema.

BBC
 
Aisee ingelikuwa bongo JWTZ wamelala... aisee sipati picha wangechambwa humu na kupondwa walakini kwa kuwa ni wamarekani .....basi mna watetea kwa nguvu zote...............mniwie radhi mipashow sitakii
Jeshi la Marekani wanatumia teknolojia, hakafu washapigana vita nyingi mnoooo.

Wakati JWTZ kaxi yao kupiga Raia wasio hata na wembe
 
Aisee ingelikuwa bongo JWTZ wamelala... aisee sipati picha wangechambwa humu na kupondwa walakini kwa kuwa ni wamarekani .....basi mna watetea kwa nguvu zote...............mniwie radhi mipashow sitakii
Usilinganishe USA armed forces na utopolo wa Jwtz,Hawa wakwetu wanaona ufahari kupiga Raia asiye hata na mafunzo ya uskauti,hao wa USA uliona jinsi walivyo enenda wakati wa kampeni ya "black lives matters"waliingia barabarani wakapiga na "goti"kusaport kampeni,ya huku kwetu haya yalioyoingia jeshi kuanzia 2000,ni usharobalo mtupu,hakuna kitu.
 
Hakukuwa na ulazima wa wanajeshi kulala karibu na maeneo yaliyotajwa kulinda usalama kulingana na hali ya kidemokrasia na siasa za nchi kama marekani ndio sababu Joe Biden amewakmba radhi wanajeshi.
 
Ujeshi ndio kazi yao!
Mnaenda lindoni kwa zamu!
Wasio zamu wanalala hadi muda wa zamu yao wanaamka kwenda kuwapoke walio maliza zamu!
Nisamehe sisi Wakurya kiswahili kwetu hakinyooki


Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
Hakukuwa na ulazima wa kupekleka wanajeshi wengi kiasi kile,Ni uoga wa kijinga tu hadi kupelekea wengine kulala hovyo..
 
Wanajeshi wa US hawapigi Raia, kwahiyo wanakuwa wengi ili kuweka ukuta
Nasemaje hakukuwa na ulazima wowote wa kupeleka 25k troops Washington.Ndio maana watu wamekasirika,kwa nini wanawajaza wanajeshi wenigi kiasi hivyo hadi wengine wanalala siku nzima bila kwenda doria??.Wali over react tuu..
 
Amefanya vizury kuomba msamaha lakini me naona biden bado ana unjuka wa uongozi kwasababu hiyo ndo kazi ya jeshi au walitaka wakalale lodge
 
Back
Top Bottom