Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,207
- 4,703
Rais Joe Biden wa Marekani ameomba msamaha baada ya baadhi ya wanajeshi waliokuwa wamewekwa kulinda eneo la Capitol kupigwa picha wakiwa wamelala katika eneo la kuegesha magari.
Zaidi ya wanajeshi 25,000 walipelekwa Washington DC kwa ajili ya kushughuli ya kuapishwa kwake mapema mwezi huu.
Picha walizopigwa maafisa hao zilianza kusambaa mtandaoni Alhamisi zikiwaonesha wakiwa wamepumzika katika eneo la karibu la kuegesha magari wabunge waliporejea.
Hali hiyo ilisababisha hasira miongoni mwa wanasiasa huku baadhi ya magavana wakawaondoa wanajeshi wao kwasababu ya utata huo.
Bwana Biden alizungumza na mkuu wa jeshi la kulinda usalama wa taifa Ijumaa, kuomba msamaha na kuuliza ni kipi ambacho kingekuwa kimefanywa kuweka mambo sawa, kulingana na vyombo vya habari vya Marekani.
Mama wa taifa Jill Biden pia naye alitembelea baadhi ya vikosi hivyo kuwashukuru akiwa amewabeba biskuti kutoka Ikulu kama zawadi.
"Leo hii nilitaka tu kuja na kuwashukuru kwa kutulinda mimi pamoja na familia yangu," alisema.
BBC
Zaidi ya wanajeshi 25,000 walipelekwa Washington DC kwa ajili ya kushughuli ya kuapishwa kwake mapema mwezi huu.
Picha walizopigwa maafisa hao zilianza kusambaa mtandaoni Alhamisi zikiwaonesha wakiwa wamepumzika katika eneo la karibu la kuegesha magari wabunge waliporejea.
Hali hiyo ilisababisha hasira miongoni mwa wanasiasa huku baadhi ya magavana wakawaondoa wanajeshi wao kwasababu ya utata huo.
Bwana Biden alizungumza na mkuu wa jeshi la kulinda usalama wa taifa Ijumaa, kuomba msamaha na kuuliza ni kipi ambacho kingekuwa kimefanywa kuweka mambo sawa, kulingana na vyombo vya habari vya Marekani.
Mama wa taifa Jill Biden pia naye alitembelea baadhi ya vikosi hivyo kuwashukuru akiwa amewabeba biskuti kutoka Ikulu kama zawadi.
"Leo hii nilitaka tu kuja na kuwashukuru kwa kutulinda mimi pamoja na familia yangu," alisema.
BBC