Tetesi: Marekani kuivamia Venezuela

Russia mtoe kwenye hiyo list, hadi vita inapiganwa kwake maana yake walishampima na wakamuona anaingilika walau tumseme North Korea anaweza akadinda mbele ya US ila sio Putin.

Putin alitoa tamka, yeyote atakayemsaidia Ukraine atakutana na mkono mzito. US akawa wa kwanza kabisa kutoa misaada kwa Ukraine, Putin akaufyata, leo hii ulaya nzima inatoa msaada kwa Ukraine na hakuna kitu amefanya. US sio nchi ya mzaha mzaha, jamaa wana watu vichwa haswa.
 
Kuchangiwa na Nchi kubwa zenye uwezo mkubwa wa kivita tena zaidi ya nne sio mchezo, so hata hivyo Russia anajitahidi sana, ila Marekani ikitangaza rasmi vita na Russia haitakuwa kama ilivyo na hata Nyuklia inaweza tumika

Russia ina wananchi wake wengi sana Ukraine kwahiyo Russia huwa inashambulia kwa umakini wakijua kuwa wana wananchi wake kule Ukraine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…