Mwanakili90
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 1,568
- 246
Marekani imeanza kufanyia majaribio ndege zake
za kivita zisizo na rubani nchini Ethiopia katika
maandalizi ya kuanza mashambulio dhidi ya
ngome za wapiganaji wa Al Shabaab katika nchi
jirani ya Somalia. Ndege hizo ambazo zinaweza kubeba
makombora na mabomu yanayoelekezwa kwa
kutumia mtambo wa satelite zitaruka kutoka
kituo cha jeshi la Marekani katika mji wa kusini
mwa Ethiopia wa Arba Minch. Marekani hata hivyo imeihakikishia serikali ya
Ethiopia kwamba ndege hizo hazina silaha kwa
hivi sasa na zinatumika tu kuchunguza hali ya
usalama. Marekani imekuwa ikitumia ndege hizi nchini
Djibouti ambako majeshi yake yana ngome yake
ya kudumu ya kipekee barani Afrika.
Source:BBC
za kivita zisizo na rubani nchini Ethiopia katika
maandalizi ya kuanza mashambulio dhidi ya
ngome za wapiganaji wa Al Shabaab katika nchi
jirani ya Somalia. Ndege hizo ambazo zinaweza kubeba
makombora na mabomu yanayoelekezwa kwa
kutumia mtambo wa satelite zitaruka kutoka
kituo cha jeshi la Marekani katika mji wa kusini
mwa Ethiopia wa Arba Minch. Marekani hata hivyo imeihakikishia serikali ya
Ethiopia kwamba ndege hizo hazina silaha kwa
hivi sasa na zinatumika tu kuchunguza hali ya
usalama. Marekani imekuwa ikitumia ndege hizi nchini
Djibouti ambako majeshi yake yana ngome yake
ya kudumu ya kipekee barani Afrika.
Source:BBC