Richie the1
New Member
- Aug 25, 2014
- 3
- 6
Hawa jamaa walichotufanyia leo tarehe 28 nov 2019...gari ya kwanza kutoka arusha sio cha kufanya gari za kisasa. Yaani tumekuja na gari tukiwa tunaelekea dar ikaharibika msata (hilo ni jambo la kawaida) sasa namna walivyo handle the situation ndio tatizo linapoanza wametufaulisha kwenye coaster mizigo wakaweka kwenye gari ya pili iliyokua nyuma yetu na hii coaster kumbe tunajilipia na isitoshe inaishia makumbusho huku mizigo yetu tukitakiwa kwenda kuichukua shekilango...nauli ya dar tumetoa 33k nayli ya msata-makumbusho 5k,majibu yao kutoka kwenye ofisi zao zote dar,moshi na arusha ni mabovu na wanakukatia simu mteja. Kwa hali hii mimi binafsi kupanda hii gari pale nitakapo kosa kabisa gari ya kupanda jambo ambalo ni gumu sana kwa karne hii option zimekua nyingi biashara huria huwezi ku treat mteja kipuuzi kiasi hiki na ukategemea kukutangaza vizuri kurecommend wengine, mimi nimepanda kwa recommendation ya mtu ambae hajawahi panda alisikia tuu kwa mtu, na yeye baada ya kusikia hivi hana mpango wa kupanda tena sasa hapo tuu ni wateja w3. Wabadilike laa sivyo wateja tunahitaji huduma siku hizi sio enzi za Mwalimu hizi.