Marando Kuhamia CHADEMA

Nyunyu

JF-Expert Member
Mar 9, 2009
4,354
1,010
Wakuu,

Toka nilivyosikia kuwa mwanasiasa na mwanasheria mkongwe nchini Mabere Marando kahamia CHADEMA, nimekuwa katika upembuzi yakinifu kutokana na historia yan nyuma ya mheshimiwa huyu.

Mabere Marando; kama wote tufahamuvyo aliwahi kuajiriwa serikalini kule kwa wale wanaojiita "Usalama wa Taifa" Wakati wa vugu vugu la vyama vingi, pamoja na wengine ikiwamo Mrema, ni mmoja wa watu walioutangazia umma kuhama CCM na kujiunga upinzani. Wakati huo NCCR-Mageuzi ilikuwa juu. Wakahamia huko na Mrema. Wakahamasisha watu wote tukaamini mageuzi yanakuja TZ katika uchaguzi huo wa 1995. Wote tunajua yaliyotokea. Marando baada ya kuivuruga NCCR-M akahama chama na kutokomea anakokujua; he stayed low profiled.

Iweje leo CHADEMA, "chuma kimeshika kasi" anatangaza tena kutoka huko anakokujua na kujiunga nacho? Maswali yanayonitatiza ni haya;

Je haiwezi kuwa, kutokana na historia ya kazi yake Mabere Marando "yuko kazini" CHADEMA?

Kuwavuruga na kisha aondoke akilalamika wakati amekimaliza chama chetu?

Ndugu zangu, naomba luwakilisha hoja yangu.

Go Dr. Slaa go...
 
Sote twajua kama Marando anawatetea mafisadi katika kesi zao mahakamani -- Jitu Tapeli na Basil Mramba among them na hili Chadema wanalijua fika. Lakini nilivyoambiwa (msiniulize na nani) ni kwamba alikubali kuwatetea ili kupata ushaidi wa ndani kabisa wa utapeli wao -- kama vile vile 'vimemo' baina ya viongozi wa CCM na hao wezi wa EPA ili auanike hadharani.

Ameshaupata huo ushahidi wa ndani na alikuwa anangojea mtu wa kuumwaga hadharani. Sasa kisha ampata mtu muafaka na credible kwa kazi hiyo -- Dr W. Slaa na tutegemee makombora yake, kasema tayari anayo 20.

Safari hii CCM WATAJIBEBAAAAAA!!!!
 
Sote twajua kama Marando anawatetea mafisadi katika kesi zao mahakamani -- Jitu Tapeli na Basil Mramba among them na hili Chadema wanalijua fika. Lakini nilivyoambiwa (msiniulize na nani) ni kwamba alikubali kuwatetea ili kupata ushaidi wa ndani kabisa wa utapeli wao -- kama vile vile 'vimemo' baina ya viongozi wa CCM na hao wezi wa EPA ili auanike hadharani.

Ameshaupata huo ushahidi wa ndani na alikuwa anangojea mtu wa kuumwaga hadharani. Sasa kisha ampata mtu muafaka na credible kwa kazi hiyo -- Dr W. Slaa na tutegemee makombora yake, kasema tayari anayo 20.

Safari hii CCM WATAJIBEBAAAAAA!!!!

We better be sure he is for real!!!
 
.

Ameshaupata huo ushahidi wa ndani na alikuwa anangojea mtu wa kuumwaga hadharani. Sasa kisha ampata mtu muafaka na credible kwa kazi hiyo -- Dr W. Slaa na tutegemee makombora yake, kasema tayari anayo 20.

!

Nadhani makombora yan[paswa kwenda sambamba na ilani inayoeleza wakiingia watafanya nini? Kwa mfano wanaweza sema yote waliyonayo na.... watabadili katiba. Just an example!
 
Mimi nadhani wana mageuzi tuache woga. Kwani Marando ni raia wa wapi? hivi mnafikiri huko usalama wa taifa wana mageuzi hawapo? Ilimradi tu Marando hatugeuki majukwaani na kuisifia ccm kama Mrema. Endelea Marando, songa mbele, tangaza habari za ukombozi wa mtanzania, achana na waoga na wakatishaji tamaa, na hakika tutashinda kwani Mungu yupo upande wetu.
 
Wakuu,
Mabere Marando; kama wote tufahamuvyo aliwahi kuajiriwa serikalini kule kwa wale wanaojiita "Usalama wa Taifa" Wakati wa vugu vugu la vyama vingi, pamoja na wengine ikiwamo Mrema, ni mmoja wa watu walioutangazia umma kuhama CCM na kujiunga upinzani. Wakati huo NCCR-Mageuzi ilikuwa juu. Wakahamia huko na Mrema. Wakahamasisha watu wote tukaamini mageuzi yanakuja TZ katika uchaguzi huo wa 1995. Wote tunajua yaliyotokea. Marando baada ya kuivuruga NCCR-M akahama chama na kutokomea anakokujua; he stayed low profiled.

Iweje leo CHADEMA, "chuma kimeshika kasi" anatangaza tena kutoka huko anakokujua na kujiunga nacho? Maswali yanayonitatiza ni haya;

Go Dr. Slaa go...

Masikini Nyunyu ama umetumwa au una lako jambo ! Yaani hata hujui vugu vugu la mageuzi lilivyoanza au hata NCCR-Mageuzi ilianza vipi hadi kwa akili yako unathubutu kuropoka kwa madai ya uwongo - eti Mabere Marando pamoja na Mrema ni mmoja wa watu walioutangazia umma kuhama CCM na kujiunga NCCR-Mageuzi ambayo wakati huo ilikuwa juu ! Pole Nyunyu, Watanzania wameamka na hawako tayari kudanganyika kwa jambo la kipuuzi na kijinga kama hili lako.

Unajidai ni shabiki wa Dr. Slaa na hapo hapo unamponda moja wa askari wake, mwanzilishi na shujaa wa mageuzi nchini aliyeonja joto la jiwe mikononi mwa pandikizi la CCM kwa jina Augustino Lyatonga Mrema ! Hapana, Nyunyu, rudi huko huko shimoni ulikotoka na umwache mkombozi wetu Dr, Slaa na jeshi lake lililokamilika liendeleze libeneke tuling'oe hili dude lililotuadhiri na kutudumaza kwa miaka karibia hamsini. Kama unamkubali Dr. Slaa, uwe tayari kuwakubali na maluteni wake.
 
Wakuu,

Toka nilivyosikia kuwa mwanasiasa na mwanasheria mkongwe nchini Mabere Marando kahamia CHADEMA, nimekuwa katika upembuzi yakinifu kutokana na historia yan nyuma ya mheshimiwa huyu.

Mabere Marando; kama wote tufahamuvyo aliwahi kuajiriwa serikalini kule kwa wale wanaojiita "Usalama wa Taifa" Wakati wa vugu vugu la vyama vingi, pamoja na wengine ikiwamo Mrema, ni mmoja wa watu walioutangazia umma kuhama CCM na kujiunga upinzani. Wakati huo NCCR-Mageuzi ilikuwa juu. Wakahamia huko na Mrema. Wakahamasisha watu wote tukaamini mageuzi yanakuja TZ katika uchaguzi huo wa 1995. Wote tunajua yaliyotokea. Marando baada ya kuivuruga NCCR-M akahama chama na kutokomea anakokujua; he stayed low profiled.

Iweje leo CHADEMA, "chuma kimeshika kasi" anatangaza tena kutoka huko anakokujua na kujiunga nacho? Maswali yanayonitatiza ni haya;

Je haiwezi kuwa, kutokana na historia ya kazi yake Mabere Marando "yuko kazini" CHADEMA?

Kuwavuruga na kisha aondoke akilalamika wakati amekimaliza chama chetu?

Ndugu zangu, naomba luwakilisha hoja yangu.

Go Dr. Slaa go...

Mkuu Nyunyu,

Huyo Mh. Marando naona amejieleza mwenyewe kwenye hiyo mikutano ya kumtambulisha Dr. Slaa. Nimesoma kwenye gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa. Naomba nivute yale aliyoyasema kwenye huo mkutano mjini Morogoro, para za mwisho kabisa kwenye hii quote:

MWANASIASA wa siku nyingi na wakili wa kujitegemea, Mabere Marando, ameituhumu serikali kwa kuhusika moja kwa moja katika wizi wa fedha za Malipo kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje kupitia Benki Kuu ya Tanzania (EPA), ambapo kiasi cha sh bilioni 133 zilikwapuliwa.

Marando, ambaye ni miongoni mwa mawakili wanaowatetea baadhi ya watuhumiwa wa kesi za EPA ambazo hivi sasa zipo mahakamani, alisema kuwa yupo tayari kutoa nyaraka zinazothibitisha kuhusika kwa serikali katika ukwapuaji huo unaofikia shilingi bilioni 133.

Kauli hiyo aliitoa jana mjini hapa, uwanja wa Shule ya Msingi Keindege, wakati akiwahutubia wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara wa kuomba udhamini kwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa.

Marando ambaye alijiunga na CHADEMA hivi karibuni akitokea NCCR - Mageuzi, alisema wananchi kamwe wasitarajie kuwa serikali ya CCM inaweza kupambana na rushwa, kwa sababu yenyewe ndiyo iliyoipanda na hivi sasa inafurahia mavuno yake.

Alisema kuwa fedha za EPA ni wizi uliotiwa baraka na serikali ya CCM na ndiyo uliomsaidia Rais Jakaya Kikwete kuingia madarakani katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.

Aliongeza kuwa amegundua kuhusika huko kwa serikali kutoka kwenye baadhi ya kesi anazozisimamia, akiwa ni wakili, ikiwamo ile inayomkabili mfanyabiashara maarufu, Jeetu Patel, ambaye ni mteja wake.

“Ninaahidi kuzionyesha hadharani nyaraka za wizi wa EPA na namna serikali ilivyobariki, kwa sababu ilizihitaji fedha hizo ili zimsaidie Kikwete kuingia madarakani,” alisema Marando.

Alisema wananchi wanapaswa kujua kwamba serikali ya CCM haina uwezo wa kuondoa ufisadi na umaskini, kwa kuwa inanufaika na matatizo ya wananchi.

Katika mkutano huo, Marando alikiri mbele ya umati wa wananchi kuwa yeye kitaaluma ni mwana usalama na kwamba miongoni mwa kazi alizopata kuzifanya ni ile ya kubaini mitego ya majeshi ya aliyekuwa kiongozi wa Uganda, Iddi Amini, aliyeingia vitani na Tanzania, akiwa Mtanzania wa kwanza kuweka miguu yake Kampala.

Marando alisema hajajiunga na CHADEMA kwa lengo la kuibomoa, bali amefanya hivyo ili kuhakikisha wanaiondoa CCM madarakani, ili wananchi wakomboke kwenye minyororo ya kuonewa, kudhalilishwa na kuibiwa.

Mwenye kutaka habari kamili aende kwenye gazeti husika:

Marando apasua bomu

Wakati mwingine ni rahisi kumtuhumu mtu kwa hisia, lakini mpeni nafasi muone kama kweli ana malengo ya kukibomoa chama. Kwa sasa hapo alipo hana nafasi yoyote inayogusa maamuzi magumu ya chama, labda aalikwe kwenye vikao ambako hana nafasi hata ya kupiga kura zaidi ya kuchangia tu. Mpeni benefit of doubt.
 
Ninavyokumbuka mimi ni kwamba Marando hakuwa chanzo cha vurugu NCCR Mageuzi wakati ule, Mrema ndiye aliyekuwa chanzo. Marando alijitahidi sana kukipigania Chama ili kirudi mikononi kwake baada ya kubaini hila za Mrema, bahati mbaya alishindwa. kama mchangiaji hapo juu, naweza kusema Marando alikutana na Ajali ya Kisiasa, lakini ukweli utabakia kwamba Marando ni mmoja wa Waasisi wa Mageuzi nchini.
 
Marando ambaye alijiunga na CHADEMA hivi karibuni akitokea NCCR - Mageuzi, alisema wananchi kamwe wasitarajie kuwa serikali ya CCM inaweza kupambana na rushwa, kwa sababu yenyewe ndiyo iliyoipanda na hivi sasa inafurahia mavuno yake.
Alisema kuwa fedha za EPA ni wizi uliotiwa baraka na serikali ya CCM na ndiyo uliomsaidia Rais Jakaya Kikwete kuingia madarakani katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.
Aliongeza kuwa amegundua kuhusika huko kwa serikali kutoka kwenye baadhi ya kesi anazozisimamia, akiwa ni wakili, ikiwamo ile inayomkabili mfanyabiashara maarufu, Jeetu Patel, ambaye ni mteja wake.
"Ninaahidi kuzionyesha hadharani nyaraka za wizi wa EPA na namna serikali ilivyobariki, kwa sababu ilizihitaji fedha hizo ili zimsaidie Kikwete kuingia madarakani," alisema Marando.
Alisema wananchi wanapaswa kujua kwamba serikali ya CCM haina uwezo wa kuondoa ufisadi na umaskini, kwa kuwa inanufaika na matatizo ya wananchi.
Katika mkutano huo, Marando alikiri mbele ya umati wa wananchi kuwa yeye kitaaluma ni mwana usalama na kwamba miongoni mwa kazi alizopata kuzifanya ni ile ya kubaini mitego ya majeshi ya aliyekuwa kiongozi wa Uganda, Iddi Amini, aliyeingia vitani na Tanzania, akiwa Mtanzania wa kwanza kuweka miguu yake Kampala.

Marando ni moto wa kuotea mbali, NCCR iliharibiwa na mrema ikawa basi tena. Ninafurahia mtu anapoongea akiwa na ushahid mikononi kama huyu jamaa ambaye anajua sana maana ya ushahidi. Wizi wa EPA ndio uliompeleka Kikwete Ikulu, ndiyo maana serikali haiweiz kufanya lolote kuhusiana na wizi huo.
 
Back
Top Bottom