Mara yangu ya kwanza kumtia machoni Iddi Simba 1980s

..I dont feel like he is offering anything that is not known, or he is setting any record straight.

..sina uhakika kama kitakuwa kizuri kama kitabu cha Mzee Mtei au Conrad Mselle ambao ni watata kidogo na walikuwa na "makaburi ya kufukua."

Cc Kiranga
Wadogo zangu walikuja kunitembelea likizo, kama ilivyo ada kila mwaka miaka hii ya karibuni.

Basi wakaniuliza, kaka mkubwa tukuletee zawadi gani? Swali tata sana hili.

Nikaomba waniletee asali ya Tanzania na kitabu cha Mkapa.

Kitabu kilikuwa "out of print", zikapigwa simu mpaka kikapatikana, nikaletewa.

Nikakisoma kwa hamu, kwa kituo. Kwa jicho la mtu anayeijua familia ya Mkapa si kwa kupitia magazeti na siasa, bali kama mtu niliyekua na watoto wa familia Upanga.

Kusema kweli, Mzee Mkapa katupiga chenga tu na hiki kitabu. Ni muhimu kukisoma, lakini kwa caliber ya muandishi kama yeye, alichofanya kwenye kitabu hiki ni kutoa muhtasari wa mambo machache tu, na hata hayo kayaongelea kijuu juu tu.

Mfano, alivyoelezea jinsi alivyoingizwa kingi kwenye issue ya EPA, yani ukisoma unaona kabisa hapa mshua anatumia kitu kinaitwa "plausible deniability". Mkapa ni mtu meticulous sana, sana tu, na si mtu wa kudanganywa kitoto vile.

Ila, naona kaona afadhali apate fedheha ya kujifanya alikuwa mjinga, kuliko kupata lawama ya kwamba alikuwa "fisadi".

Ni kitabu kizuri kama unataka kujua historia ya maisha ya awali ya Mkapa, ingawa hata kwenye familia nako ameshindwa hata kumtaja Peter kama mtoto wake wa kufikia, ukisoma utafikiri Nick na Stephan ndio watoto pekee, lakini kama unataka kujua mambo kwa undani, Mkapa kabakisha maneno mengi sana kuliko aliyoandika. Kuanzia alivyokuwa anamwambia Nyerere kwamba Kambona anamsengenya, na Nyerere akiwa haamini anam dismiss Mkapa, mpaka ukweli kuhusu alivyokubali kupiga dili la EPA.

Kabla ya kusoma kitabu cha Mkapa, nilikuwa nasoma kitabu cha balozi wa serikali ya Marekani chini ya Obama hapo UN, Samantha Power, kinaitwa "The Education of An Idealist: A Memoir". Ukisoma wenzetu wanavyozama katika kueleza maisha yao na maamuzi waliyochukua wakiwa madarakani, halafu ukasoma kitabu cha Mkapa, utaona kitabu cha Mkapa kimejaa habari za "danganya toto, kula kunde, nyama mbichiii".

The book is full of plausible deniability, omissions,obfuscation, conveniently late conversions to being a democrat, the list goes on.

In short, the book is an insults to our collective intelligence.
 
Wadogo zangu walikuja kunitembelea likizo, kama ilivyo ada kila mwaka miaka hii ya karibuni.

Basi wakaniuliza, kaka mkubwa tukuletee zawadi gani? Swali tata sana hili.

Nikaomba waniletee asali ya Tanzania na kitabu cha Mkapa.

Kitabu kilikuwa "out of print", zikapigwa simu mpaka kikapatikana, nikaletewa.

Nikakisoma kwa hamu, kwa kituo. Kwa jicho la mtu anayeijua familia ya Mkapa si kwa kupitia magazeti na siasa, bali kama mtu niliyekua na watoto wa familia Upanga.

Kusema kweli, Mzee Mkapa katupiga chenga tu na hiki kitabu. Ni muhimu kukisoma, lakini kwa caliber ya muandishi kama yeye, alichofanya kwenye kitabu hiki ni kutoa muhtasari wa mambo machache tu, na hata hayo kayaongelea kijuu juu tu.

Mfano, alivyoelezea jinsi alivyoingizwa kingi kwenye issue ya EPA, yani ukisoma unaona kabisa hapa mshua anatumia kitu kinaitwa "plausible deniability". Mkapa ni mtu meticulous sana, sana tu, na si mtu wa kudanganywa kitoto vile.

Ila, naona kaona afadhali apate fedheha ya kujifanya alikuwa mjinga, kuliko kupata lawama ya kwamba alikuwa "fisadi".

Ni kitabu kizuri kama unataka kujua historia ya maisha ya awali ya Mkapa, ingawa hata kwenye familia nako ameshindwa hata kumtaja Peter kama mtoto wake wa kufikia, ukisoma utafikiri Nick na Stephan ndio watoto pekee, lakini kama unataka kujua mambo kwa undani, Mkapa kabakisha maneno mengi sana kuliko aliyoandika. Kuanzia alivyokuwa anamwambia Nyerere kwamba Kambona anamsengenya, na Nyerere akiwa haamini anam dismiss Mkapa, mpaka ukweli kuhusu alivyokubali kupiga dili la EPA.

Kabla ya kusoma kitabu cha Mkapa, nilikuwa nasoma kitabu cha balozi wa serikali ya Marekani chini ya Obama hapo UN, Samantha Powers, kinaitwa "The Education of An Idealist: A Memoir". Ukisoma wenzetu wanavyozama katika kueleza maisha yao na maamuzi waliyochukua wakiwa madarakani, halafu ukasoma kitabu cha Mkapa, utaona kitabu cha Mkapa kimejaa habari za "danganya toto, kula kunde, nyama mbichiii".

The book is full of plausible deniability, omissions,obfuscation, conveniently late conversions to being a democrat, the list goes on.

In short, the book is an insults to our collective intelligence.

..siku ya uzinduzi nilimuona Mzee Mramba.

..Je,Mzee Mkapa amezungumzia lolote kuhusu kesi ya Mramba na Yona?

..amezungumzia kuhusu kesi ya Prof.Mahalu ambaye alilazimika kwenda kumtetea?

..vipi kuhusu lawama za muda mrefu kuhusu mikataba ya madini? ametoa neno kuhusu masuala hayo?
 
..siku ya uzinduzi nilimuona Mzee Mramba.

..Je,Mzee Mkapa amezungumzia lolote kuhusu kesi ya Mramba na Yona?

..amezungumzia kuhusu kesi ya Prof.Mahalu ambaye alilazimika kwenda kumtetea?

..vipi kuhusu lawama za muda mrefu kuhusu mikataba ya madini? ametoa neno kuhusu masuala hayo?
Kitabu kizima sikumbuki kuona Mramba katajwa.

Amemtetea sana sana tu Dr. Mahalu, ukikisoma kitabu ndiyo utajua kuwa Mkapa na Mahalu ni maswahiba wakubwa sana, nilikuwa najua ni marafiki, lakini kusoma kitabu kumenifungua macho kujua kwamba wanapatana sana.

Hayo mambo ya madini kaongelea in passing juu juu tu. Unasoma unaona boilerplate tu.

Nilitaka kuandika full review hapa, lakini nikataka kusubiri muda kidogo labda watu wengine watapata kukisoma niweze kujadiliana na watu wengine waliokisoma pengine nakosea, huwa najipa nafasi ya kuweza kukosea siku zote.
 
Kitabu kizima sikumbuki kuona Mramba katajwa.

Amemtetea sana sana tu Dr. Mahalu, ukikisoma kitabu ndiyo utajua kuwa Mkapa na Mahalu ni maswahiba wakubwa sana, nilikuwa najua ni marafiki, lakini kusoma kitabu kumenifungua macho kujua kwamba wanapatana sana.

Hayo mambo ya madini kaongelea in passing juu juu tu. Unasoma unaona boilerplate tu.

Nilitaka kuandika full review hapa, lakini nikataka kusubiri muda kidogo labda watu wengine watapata kukisoma niweze kujadiliana na watu wengine waliokisoma pengine nakosea, huwa najipa nafasi ya kuweza kukosea siku zote.

..kama Mkapa anajivunia kwa ku-turn around the economy lazima awaseme vizuri mawaziri wake wa fedha ambao ni yona na mramba.
 
MARA YANGU YA KWANZA KUMTIA MACHONI IDDI SIMBA 1980s

Ilikuwa miaka ya 1980 tuko nyumbani kwa marehemu Bi. Mruguru bint Mussa, mama yake Ally Sykes Mtaa wa Lindi.

Pametokea msiba Bi. Mariamu, shangazi yake Bwana Ally Sykes amefariki.

Watu wamejazana mtaa umefungwa wanasubiri muda wa mazishi.

Bwana Ally mwenyewe kakaa jamvini kazungukwa na jamaa zake wa Gerezani, wamekukuja kuungananae katika msiba wa shangazi yake.

Watu ni wengi sana.

Bwana Ally yeye mwenyewe ni mzishi sasa leo limemfika ndugu zake wamemwitika kwa wingi sana, wamekuja kumzika.

Bwana Ally kuniona ananita nende nikakae nae mbele.

Basi nanyanyuka pale nyuma nilipokuwa kwa unyonge maana umma mzima unaniangalia watu wanajiuliza huyu anaeitwa mbele pale ana umuhimu gani?

Katika lile jamvi alokuwa Bwana Ally ni “nani aliye nani katika mji wa Dar es Salaam,” Waingereza wanasema “Who is Who,” wenyewe watoto wa Gerezani na Dar es Salaam wametanda.

Iddi Simba alikuwa amekaa jirani ya Ally Sykes.

Amevaa nguo zilizomkaa vyema kapendenza na miwani yake.

Sasa Bwana Ally anawanadia watu, “Nyie mnamjua huyu? Mtoto wa Said pale Kipata mwandishi hodari sana…”

Utambulisho umekwisha nakaa pembeni Ally Sykes na Zuberi Mtemvu wanashambuliana kwa maneno.

Bwana Ally kalalamika kuhusu hali ya nchi mambo hayendi vyema.

Zuberi Mtemvu kadakia anawashahidisha watu, “Jamani mnasikia Ally analalamika ati mambo hayendi sawa…”

Mtemvu anaangua kicheko cha kejeli huku akitingisha kichwa.

Watu sasa weshakuwa hadhir wanasubiri Mtemvu atasema kitu gani?

“Huyu Ally na marehemu kaka yake Abdul (Mungu amrehemu) walikuwa wanashirikiana na Nyerere kukipiga vita chama changu kife, leo Ally huyu huyu keshageuka ati nchi imeharibika…”

Wasikizaji wanacheka wengine wanamuunga mkono Bwana Ally wengine Zuberi Mtemvu.

Bwana Ally hakubali kushindwa anarudisha kombora, “Ala kumbe Congress bado mko hadi leo nilidhania tulishakumalizeni.”

Vicheko.

Mzee mmoja kwa mbali anaita, “Ally sikiza bwana, Congress tupo sana. Congress ni mwamba usiovunjika.”

Vicheko vinaendelea.

Hii “Congress ni mwamba usiovunjika,” ni maneno yaliyokuwa katika nyimbo ya Congress wakati wa harakati za kudai uhuru.

Watu wametulia Bwana Ally akafahamu kuwa Mtemvu alikuwa hamjui Iddi Simba na pale akawatambulisha.

Nilishangaa sana vipi miamba hii yote ya Gerezani isifahamiane.

Hapo nami ndipo nikamfahamu Iddi Simba ingawa jina lake lilikuwa maarufu katika vyombo vya habari kila inapotajwa East African Development Bank iliyokuwa na makao makuu yake Kampala Uganda.

Kuanzia hapo Mzee Iddi Simba kila tutakapokutana atakuwa na la kunieleza.

Mzee Iddi Simba alikuwa na kawaida kila akimaliza kusali Dhuhr Msikiti wa Manyema hatoki atakenda kukaa nyuma ya msikiti na jamaa zake watamfuata pale.

Nami hii ndiyo ilikuwa fursa yangu ya kusalimiananae kila nikiswali Msikiti wa Manyema na hapo utamkuta kakaa na rafiki yake kipenzi Muharam Kocha.

Napenda kuhitimisha kwa kueleza kisa kimoja.

Anur Suleiman alipata kuwa Mkuu wa Mkoa Mwanza katika miaka ya 1970/80.

Huyu bwana alikuwa anajenga msikiti sikumbuki kama ni kwao Bukoba au Mwanza.

Akaleta vitabu vya risiti kwa ajili ya kuchangisha nami nikapewa kimoja nichangishe hapa Dar es Salaam.

Basi siku hiyo nikamkuta Mzee Iddi Simba kakaa kwa Daddy huyu alikuwa fundi cherehani maarufu Kariakoo karibu na Saigon ya zamani, Mtaa wa Sikukuu.

Katika maisha yangu hadi hii leo sijawahi kuchangisha kitu chochote nikapata fedha nyingi kama nilizopata katika mchango huu kiasi hata yule aliyenipa kitabu kile alipigwa na butwaa.

Nikamfuata Mzee Iddi Simba kakaa pale kwenye benchi na vijana wa Saigon mtu akikwambia ukubwa wa mtu huyu na hadhi yake utakataa utajiuliza pale anafanya nini?

Mzee Iddi Simba akanisikiliza kisha akabaki kimya hakunambia chochote nami nikaondoka.

Nilidhani hakutaka kunipa mchango.

Baadae kidogo akanifanyia ishara nimfuate.

Fedha alizonipa kama mchango wake wa msikiti zilinishtua na naamini wale waliokuwa wakitaka kuchanga wanataka kwanza waangalie nani na nani washachanga bila shaka mchango ule uliwatia motisha angalau na wao watoe kingi wamkaribie Iddi Simba.

Allah amfanyie wepesi mzee wetu safari yake na amsamehe.

Amin.

View attachment 1356331

PICHA: Mzee Iddi Simba na Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu katika futari ya Saigon mwaka wa 2010
Asilimia kubwa la hili jukwaa la HISTORIA ni kama watu wamekuachia ww (mo saidi)...hongera lakini kwanini na katika maisha yako hujawahi kukutana na MKRISTO aliyefanya jambo nzuri kijamii ya tanganyika/Tanzania uje usimulie humu...maana naona wote isipokuwa nyerere ni waislamu tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asilimia kubwa la hili jukwaa la HISTORIA ni kama watu wamekuachia ww (mo saidi)...hongera lakini kwanini na katika maisha yako hujawahi kukutana na MKRISTO aliyefanya jambo nzuri kijamii ya tanganyika/Tanzania uje usimulie humu...maana naona wote isipokuwa nyerere ni waislamu tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Emanuel...
Niruhusu kujibu swali lako kwa kukuuliza swali.

Mbona hawa unaowasoma hapa hawakupata kutajwa katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Emanuel...
Niruhusu kujibu swali lako kwa kukuuliza swali.

Mbona hawa unaowasoma hapa hawakupata kutajwa katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa maana hiyo, jee hakuna Wapigania Uhuru wenye imani ya Kikristo ambao hawakutajwa? Wewe ukubali tu ni mdini. Hilo ni jambo lisilopingika na usilete kauli zako za kijanja kukwepa.
 
MARA YANGU YA KWANZA KUMTIA MACHONI IDDI SIMBA 1980s

Ilikuwa miaka ya 1980 tuko nyumbani kwa marehemu Bi. Mruguru bint Mussa, mama yake Ally Sykes Mtaa wa Lindi.

Pametokea msiba Bi. Mariamu, shangazi yake Bwana Ally Sykes amefariki.

Watu wamejazana mtaa umefungwa wanasubiri muda wa mazishi.

Bwana Ally mwenyewe kakaa jamvini kazungukwa na jamaa zake wa Gerezani, wamekukuja kuungananae katika msiba wa shangazi yake.

Watu ni wengi sana.

Bwana Ally yeye mwenyewe ni mzishi sasa leo limemfika ndugu zake wamemwitika kwa wingi sana, wamekuja kumzika.

Bwana Ally kuniona ananita nende nikakae nae mbele.

Basi nanyanyuka pale nyuma nilipokuwa kwa unyonge maana umma mzima unaniangalia watu wanajiuliza huyu anaeitwa mbele pale ana umuhimu gani?

Katika lile jamvi alokuwa Bwana Ally ni “nani aliye nani katika mji wa Dar es Salaam,” Waingereza wanasema “Who is Who,” wenyewe watoto wa Gerezani na Dar es Salaam wametanda.

Iddi Simba alikuwa amekaa jirani ya Ally Sykes.

Amevaa nguo zilizomkaa vyema kapendenza na miwani yake.

Sasa Bwana Ally anawanadia watu, “Nyie mnamjua huyu? Mtoto wa Said pale Kipata mwandishi hodari sana…”

Utambulisho umekwisha nakaa pembeni Ally Sykes na Zuberi Mtemvu wanashambuliana kwa maneno.

Bwana Ally kalalamika kuhusu hali ya nchi mambo hayendi vyema.

Zuberi Mtemvu kadakia anawashahidisha watu, “Jamani mnasikia Ally analalamika ati mambo hayendi sawa…”

Mtemvu anaangua kicheko cha kejeli huku akitingisha kichwa.

Watu sasa weshakuwa hadhir wanasubiri Mtemvu atasema kitu gani?

“Huyu Ally na marehemu kaka yake Abdul (Mungu amrehemu) walikuwa wanashirikiana na Nyerere kukipiga vita chama changu kife, leo Ally huyu huyu keshageuka ati nchi imeharibika…”

Wasikizaji wanacheka wengine wanamuunga mkono Bwana Ally wengine Zuberi Mtemvu.

Bwana Ally hakubali kushindwa anarudisha kombora, “Ala kumbe Congress bado mko hadi leo nilidhania tulishakumalizeni.”

Vicheko.

Mzee mmoja kwa mbali anaita, “Ally sikiza bwana, Congress tupo sana. Congress ni mwamba usiovunjika.”

Vicheko vinaendelea.

Hii “Congress ni mwamba usiovunjika,” ni maneno yaliyokuwa katika nyimbo ya Congress wakati wa harakati za kudai uhuru.

Watu wametulia Bwana Ally akafahamu kuwa Mtemvu alikuwa hamjui Iddi Simba na pale akawatambulisha.

Nilishangaa sana vipi miamba hii yote ya Gerezani isifahamiane.

Hapo nami ndipo nikamfahamu Iddi Simba ingawa jina lake lilikuwa maarufu katika vyombo vya habari kila inapotajwa East African Development Bank iliyokuwa na makao makuu yake Kampala Uganda.

Kuanzia hapo Mzee Iddi Simba kila tutakapokutana atakuwa na la kunieleza.

Mzee Iddi Simba alikuwa na kawaida kila akimaliza kusali Dhuhr Msikiti wa Manyema hatoki atakenda kukaa nyuma ya msikiti na jamaa zake watamfuata pale.

Nami hii ndiyo ilikuwa fursa yangu ya kusalimiananae kila nikiswali Msikiti wa Manyema na hapo utamkuta kakaa na rafiki yake kipenzi Muharam Kocha.

Napenda kuhitimisha kwa kueleza kisa kimoja.

Anur Suleiman alipata kuwa Mkuu wa Mkoa Mwanza katika miaka ya 1970/80.

Huyu bwana alikuwa anajenga msikiti sikumbuki kama ni kwao Bukoba au Mwanza.

Akaleta vitabu vya risiti kwa ajili ya kuchangisha nami nikapewa kimoja nichangishe hapa Dar es Salaam.

Basi siku hiyo nikamkuta Mzee Iddi Simba kakaa kwa Daddy huyu alikuwa fundi cherehani maarufu Kariakoo karibu na Saigon ya zamani, Mtaa wa Sikukuu.

Katika maisha yangu hadi hii leo sijawahi kuchangisha kitu chochote nikapata fedha nyingi kama nilizopata katika mchango huu kiasi hata yule aliyenipa kitabu kile alipigwa na butwaa.

Nikamfuata Mzee Iddi Simba kakaa pale kwenye benchi na vijana wa Saigon mtu akikwambia ukubwa wa mtu huyu na hadhi yake utakataa utajiuliza pale anafanya nini?

Mzee Iddi Simba akanisikiliza kisha akabaki kimya hakunambia chochote nami nikaondoka.

Nilidhani hakutaka kunipa mchango.

Baadae kidogo akanifanyia ishara nimfuate.

Fedha alizonipa kama mchango wake wa msikiti zilinishtua na naamini wale waliokuwa wakitaka kuchanga wanataka kwanza waangalie nani na nani washachanga bila shaka mchango ule uliwatia motisha angalau na wao watoe kingi wamkaribie Iddi Simba.

Allah amfanyie wepesi mzee wetu safari yake na amsamehe.

Amin.

View attachment 1356331

PICHA: Mzee Iddi Simba na Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu katika futari ya Saigon mwaka wa 2010
Hapa alikuwa ameisha acha kupiga masanga?
 
Kwa maana hiyo, jee hakuna Wapigania Uhuru wenye imani ya Kikristo ambao hawakutajwa? Wewe ukubali tu ni mdini. Hilo ni jambo lisilopingika na usilete kauli zako za kijanja kukwepa.
Ndjabu...
Sina tatizo mtu ananiitaje.

Wala sina "kauli ya ujana," wengi wananisoma kwa yale ninayoandika yanayovutia usomaji na huu si, "ujanja."

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kitabu kizima sikumbuki kuona Mramba katajwa.

Amemtetea sana sana tu Dr. Mahalu, ukikisoma kitabu ndiyo utajua kuwa Mkapa na Mahalu ni maswahiba wakubwa sana, nilikuwa najua ni marafiki, lakini kusoma kitabu kumenifungua macho kujua kwamba wanapatana sana.

Hayo mambo ya madini kaongelea in passing juu juu tu. Unasoma unaona boilerplate tu.

Nilitaka kuandika full review hapa, lakini nikataka kusubiri muda kidogo labda watu wengine watapata kukisoma niweze kujadiliana na watu wengine waliokisoma pengine nakosea, huwa najipa nafasi ya kuweza kukosea siku zote.
Chief Kiranga

Upo makini sana Mkuu
Ila jambo moja tu
Kukataa uwepo wa Muumba wako
Hili linakuzamisha topeni kabisa Chief
Barikiwa sana
Mola atuongoze njia ya sawa
Ila upo makini Bro

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chief Kiranga

Upo makini sana Mkuu
Ila jambo moja tu
Kukataa uwepo wa Muumba wako
Hili linakuzamisha topeni kabisa Chief
Barikiwa sana
Mola atuongoze njia ya sawa
Ila upo makini Bro

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijakataa kuwepo kwa muumba wangu.

Siku zote nimekuwa nikisisitiza muumba wangu kuwepo.

Mmoja ni Baba yangu mzazi, mwingine ni Mama yangu mzazi.

Kama unaweza kuthibitisha mwingine yupo, thibitisha.

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Back
Top Bottom