Kurunzi
Platinum Member
- Jul 31, 2009
- 10,196
- 11,623
Tangu niliposikia kusambaa video ‘chafu’ inayodaiwa kuwa ya Mchungaji Gwajima kwenye mitamdao mbalimbali ya kijamii nilifanya kila juhudi kuitafuta na kuiangalia, nikikereketwa na kujiuliza, kwa nini ‘Mtumishi’ kama huyu mwenye umaarufu kama alionao, aweza kujirekodi tena kwa picha ya video akafanya kitu kama hiki, huyo anayefanya naye kitendo hicho, mwanamke, naye akakubali kurekodiwa na kisha kuisambaza video hiyo kwenye mitandao ya kijamii?.
Baada ya kuiangalia kwa umakini niliishia kucheka peke yangu, huku nikishangazwa ma weledi wa watu wengi katika kuchungua mambo. Baada ya kujirizisha kwa hatua ya kwanza, nilipiga hatua ya pili ya kudodosa hapa na pale. Na kweli sasa tunaanza kunusa harufu sio tu ya nani na nani walifanya nini lakini pia nani yupo nyuma ya kadhia hii chafu.
Kwa nini nikalazimika kufanya hivi? Kutokana sasa na mwendelezo wa kuwachafua watumishi wa MUNGU, kwa sababu aidha ya uchu wa malengo kadha wa kadha ya kisiasa nk.
Ni ukweli usiopingika kuwa kwa mtu ambaye hana weledi wa kiuchunguzi wa IT, akiangalia kwa haraka lakini anachukizwa na picha hii, na akawa ni mmoja wa wanaochukizwa na kuzalilishwa kwa watumishi wa MUNGU, anakimbilia kusema picha hiyo sio ya gwajima. Kwamba sura ya watu hao ni sura za watu wawili tofauti wanaofanana. Hapa sio watu wawili tofauti ni mtu huyo huyo ila kwa umri tofauti.
Watengenezaji wa video hii, kuna kitu hawakuzingatia na hicho ni kile kilichotamkwa na rais wetu mpendwa Magufuli wakati fulani mbele za wasaidizi wake kuwa “ watanzania sio wajinga” , lakini pia watayashaji wa picha hii, walishindwa kuzingatia kuwa kumchafua ‘mtu’ kiwango cha Gwajima unalazimisha watu au taasisi ziwasiliane na wamiliki wa mitandao ya kijamii kufahamu video au picha fulani nani aliingiza kwenye mzunguko na kabla ya hapo alikuwa na mawasiliano ya aina gani na akina nani?
Lakini huko nisiende. Acha nichezee ‘viwanja vya nyumbani’. Kama nilivyotangulia kusema sura inayoonekana kwa kuonesha kuwa ni sura ya Gwajina ikiwa na kasoro kuashiria kuwa sio ya Mtumishi huyo kweli kabisa ni ya Gwajima.
Kipande hiki cha video ni sura halisi ya Gwajima ambacho alikirekodi mwaka 2008, akiwa kwenye ujenzi Kanisa lililouwa linajengwa, yeye mwenyewe akiwa kifua wazi.
Inasadikiwa ni Kijana mmoja ambaye nisimtaje jina lake linaanza na herufi C na binti jina lake likianza kwa herufi ile ile ya ya C, (na kwa ma paparadzzi wa kweli hebu acha mzaha, huyo binti si anaonekana sura yake? Nini sasa kusema asiyefahamika? Si wakati fulani alikuwa kwenye sobu house? Be serious.) waliporatibiwa kushawishiwa na hatimaye kucheza video hii, kwa masharti ya sura zao kutoonekana, ikichezewa kigamboni. Inasadikiwa wamelipwa kitita cha sh. Mil 15 za kitanzania.
Katika usanii huu ilipaswa ionekane mchungaji mwenyewe akijirekodi, na baada ya kukamilisha ‘mshindo’ aonekane aki stop simu isiendelee kurekodi. Lakini pia alipaswa kwa kiasi kikubwa aelekeze sura yake kwenye mchukua video.
Kilichotokea baada ya kuchukuliwa video hii ilipelekwa eneo la magomeni kufanyiwa editing na mtaalamu wa kazi hiyo mwenye jina linaloanza na A. hata hivyo nadhani aidha mtaalamu huyu hajakubuhu kwenye kazi hii, au ali under estimate uwezo wa watumiaji wa bidhaa yake.
Kwanza kwa kutumia program ya kusanifu picha ya video ya Light work na Blender MAC os alikata kichwa kutoka kipande cha picha halisi kutoka picha ya Gwajima ya mwaka 2008, akakipachika kwenye picha ya kijana ambaye kwa miaka mingi aliathiriwa na madawa ya kulevya ambaye amehudumiwa kwenye sobu house, sasa kazi ikaja namna ya kuoanisha maana watu hawa wawili wanatofautiana urefu, pia unene wa shingo. Katika kufanya hivi ikalazimika kichwa cha picha hii kirefuke kwa namna fulani tofauti na uhalisia wa kichwa halisi cha Gwajima cha sasa au cha picha halisi ya video ya mwaka 2008. Hili ni kosa la kwanza.
Kosa la pili akasahau kuwa rangi halisi ya wakati ule ya Gwajima alikuwa hajapigwa sana na ‘kiyoyozi’ ilikuwa bado nyeusi lakini rangi halisi ya kiongozi wa sasa ina ‘kaweupe fulani hivi na kamg’ao. Na bila shaka angetafuta weupe halisi pengine ingetoa mwanya wa kuonesha hitalafu zaidi. Na hii bila shaka mtaalamu wetu huyu angekuwa amepitia somo la Mag face asingethubutu kutuwekea kitu kama hiki ati atuaminishe uchafu wake huu.
Kosa la tatu la Bwana A, ingawa alijitahidi sana ku adopt sauti ya Gwajina inayosikika wakati wa ‘mshindo’ lakini napo akafanya kosa la kitaalamu kuwa baada ya adoption ile sauti ikawa mono, akajaribu kutafuta stereo, maana stereo inasikika katika ‘chakacha’. Kutoa sauti mono kuipeleka stereo inahitaji weredi mkubwa. Inapaswa utoke kwenye program ya Light work uingie Adobe audio ndipo unaweza alau ku crop, inaelekea alikuwa na haraka matokeo yake, stereo kwenye mshindo ikakataa badala yake inatoa mwangwi wa sauti.
Kosa la Nne ambalo japo yapo mengi namalizia na hili. Master mind wa kadhia hii alilenga kutuaminisha kuwa Gwajima kajirekodi tukio zima kwa kutumia simu yake ya mkononi au whatever. Hakujali tutatathmini vipi kijana huyo akiamsha mkono kama anazuia asionekane wakati mkono huo uliofanikiwa kwa sehemu kuzua asionekane ulikuwa urefu mkubwa kutoka ilipo simu, kwani mwishoni anaokuwa kama vile anazima simu mkono haupandi tena kwa urefu huo.
Hili ni moja ya matukio maovu kuwahi kufanywa kwenye taifa letu. Hii hali isiruhusiwe kuendelea. Ni uovu mkuu. Na hii ndio sababu ya watu kama mimi ambao kawaida hatujishughulishi na matukio yenu tunanyamaza kimya, kwa hili tumelazimika kuwaonesha kuwa, fanyeni mambo yenu lakini waache watumishi wa MUNGU wafanye kazi yao.
Tukumbuke kuwa Gwajina yeye ni binadamu kamili kama nilivyo mimi na wewe. Anaweza kufanya ‘kitu kama hiki’. Lakini sio kwa kujirekodi na video hii kuiingiza kwenye mitandao ya kijamii, ili aonekane.
Kwani yeye ni nani? Si ni Binadamu na mwanaume kamili lakini ambaye ameamua kumtumikia MUNGU? Ndio anaweza kukosea watumishi wakubwa kuliko yeye na waliozungumza na MUNGU moja kwa moja na akawataja kuwa wapenzi wake walifanya kosa hili na kuzidi, Gwajina ni nani hata imekuwa kwamba hawezi kukosea? Je nilazima tumpachike vitu ambavyo hakufanya? Tutumie kiasi kikubwa na pesa kama ‘mlichotumia’ kutayarisha uchafu huu?
Hii ni dhambi kubwa mnafanya wanasiasa . unatumia milioni taklibani 15, ambazo zingesaidia watu maskini, kwa ajiri ya kutayarisha video kama hii na kumpaka matole mchungaji. Kumbuka fanya yote haya lakini sote Duniani tu wapitaji na siku moja tutasimama mbele za MUNGU kujibu yale tunayofanya.
Uwe tajiri usitumie utajiri wako kuonea watu, bali wasaidie igeni kwa mzee wetu Mengi. Kama wewe ni mwanasiasa usitumie nafasi yako kuonea watu igeni kwa mzee wetu Nelson Mandela.
Habari hii
Copy & Paste
Baada ya kuiangalia kwa umakini niliishia kucheka peke yangu, huku nikishangazwa ma weledi wa watu wengi katika kuchungua mambo. Baada ya kujirizisha kwa hatua ya kwanza, nilipiga hatua ya pili ya kudodosa hapa na pale. Na kweli sasa tunaanza kunusa harufu sio tu ya nani na nani walifanya nini lakini pia nani yupo nyuma ya kadhia hii chafu.
Kwa nini nikalazimika kufanya hivi? Kutokana sasa na mwendelezo wa kuwachafua watumishi wa MUNGU, kwa sababu aidha ya uchu wa malengo kadha wa kadha ya kisiasa nk.
Ni ukweli usiopingika kuwa kwa mtu ambaye hana weledi wa kiuchunguzi wa IT, akiangalia kwa haraka lakini anachukizwa na picha hii, na akawa ni mmoja wa wanaochukizwa na kuzalilishwa kwa watumishi wa MUNGU, anakimbilia kusema picha hiyo sio ya gwajima. Kwamba sura ya watu hao ni sura za watu wawili tofauti wanaofanana. Hapa sio watu wawili tofauti ni mtu huyo huyo ila kwa umri tofauti.
Watengenezaji wa video hii, kuna kitu hawakuzingatia na hicho ni kile kilichotamkwa na rais wetu mpendwa Magufuli wakati fulani mbele za wasaidizi wake kuwa “ watanzania sio wajinga” , lakini pia watayashaji wa picha hii, walishindwa kuzingatia kuwa kumchafua ‘mtu’ kiwango cha Gwajima unalazimisha watu au taasisi ziwasiliane na wamiliki wa mitandao ya kijamii kufahamu video au picha fulani nani aliingiza kwenye mzunguko na kabla ya hapo alikuwa na mawasiliano ya aina gani na akina nani?
Lakini huko nisiende. Acha nichezee ‘viwanja vya nyumbani’. Kama nilivyotangulia kusema sura inayoonekana kwa kuonesha kuwa ni sura ya Gwajina ikiwa na kasoro kuashiria kuwa sio ya Mtumishi huyo kweli kabisa ni ya Gwajima.
Kipande hiki cha video ni sura halisi ya Gwajima ambacho alikirekodi mwaka 2008, akiwa kwenye ujenzi Kanisa lililouwa linajengwa, yeye mwenyewe akiwa kifua wazi.
Inasadikiwa ni Kijana mmoja ambaye nisimtaje jina lake linaanza na herufi C na binti jina lake likianza kwa herufi ile ile ya ya C, (na kwa ma paparadzzi wa kweli hebu acha mzaha, huyo binti si anaonekana sura yake? Nini sasa kusema asiyefahamika? Si wakati fulani alikuwa kwenye sobu house? Be serious.) waliporatibiwa kushawishiwa na hatimaye kucheza video hii, kwa masharti ya sura zao kutoonekana, ikichezewa kigamboni. Inasadikiwa wamelipwa kitita cha sh. Mil 15 za kitanzania.
Katika usanii huu ilipaswa ionekane mchungaji mwenyewe akijirekodi, na baada ya kukamilisha ‘mshindo’ aonekane aki stop simu isiendelee kurekodi. Lakini pia alipaswa kwa kiasi kikubwa aelekeze sura yake kwenye mchukua video.
Kilichotokea baada ya kuchukuliwa video hii ilipelekwa eneo la magomeni kufanyiwa editing na mtaalamu wa kazi hiyo mwenye jina linaloanza na A. hata hivyo nadhani aidha mtaalamu huyu hajakubuhu kwenye kazi hii, au ali under estimate uwezo wa watumiaji wa bidhaa yake.
Kwanza kwa kutumia program ya kusanifu picha ya video ya Light work na Blender MAC os alikata kichwa kutoka kipande cha picha halisi kutoka picha ya Gwajima ya mwaka 2008, akakipachika kwenye picha ya kijana ambaye kwa miaka mingi aliathiriwa na madawa ya kulevya ambaye amehudumiwa kwenye sobu house, sasa kazi ikaja namna ya kuoanisha maana watu hawa wawili wanatofautiana urefu, pia unene wa shingo. Katika kufanya hivi ikalazimika kichwa cha picha hii kirefuke kwa namna fulani tofauti na uhalisia wa kichwa halisi cha Gwajima cha sasa au cha picha halisi ya video ya mwaka 2008. Hili ni kosa la kwanza.
Kosa la pili akasahau kuwa rangi halisi ya wakati ule ya Gwajima alikuwa hajapigwa sana na ‘kiyoyozi’ ilikuwa bado nyeusi lakini rangi halisi ya kiongozi wa sasa ina ‘kaweupe fulani hivi na kamg’ao. Na bila shaka angetafuta weupe halisi pengine ingetoa mwanya wa kuonesha hitalafu zaidi. Na hii bila shaka mtaalamu wetu huyu angekuwa amepitia somo la Mag face asingethubutu kutuwekea kitu kama hiki ati atuaminishe uchafu wake huu.
Kosa la tatu la Bwana A, ingawa alijitahidi sana ku adopt sauti ya Gwajina inayosikika wakati wa ‘mshindo’ lakini napo akafanya kosa la kitaalamu kuwa baada ya adoption ile sauti ikawa mono, akajaribu kutafuta stereo, maana stereo inasikika katika ‘chakacha’. Kutoa sauti mono kuipeleka stereo inahitaji weredi mkubwa. Inapaswa utoke kwenye program ya Light work uingie Adobe audio ndipo unaweza alau ku crop, inaelekea alikuwa na haraka matokeo yake, stereo kwenye mshindo ikakataa badala yake inatoa mwangwi wa sauti.
Kosa la Nne ambalo japo yapo mengi namalizia na hili. Master mind wa kadhia hii alilenga kutuaminisha kuwa Gwajima kajirekodi tukio zima kwa kutumia simu yake ya mkononi au whatever. Hakujali tutatathmini vipi kijana huyo akiamsha mkono kama anazuia asionekane wakati mkono huo uliofanikiwa kwa sehemu kuzua asionekane ulikuwa urefu mkubwa kutoka ilipo simu, kwani mwishoni anaokuwa kama vile anazima simu mkono haupandi tena kwa urefu huo.
Hili ni moja ya matukio maovu kuwahi kufanywa kwenye taifa letu. Hii hali isiruhusiwe kuendelea. Ni uovu mkuu. Na hii ndio sababu ya watu kama mimi ambao kawaida hatujishughulishi na matukio yenu tunanyamaza kimya, kwa hili tumelazimika kuwaonesha kuwa, fanyeni mambo yenu lakini waache watumishi wa MUNGU wafanye kazi yao.
Tukumbuke kuwa Gwajina yeye ni binadamu kamili kama nilivyo mimi na wewe. Anaweza kufanya ‘kitu kama hiki’. Lakini sio kwa kujirekodi na video hii kuiingiza kwenye mitandao ya kijamii, ili aonekane.
Kwani yeye ni nani? Si ni Binadamu na mwanaume kamili lakini ambaye ameamua kumtumikia MUNGU? Ndio anaweza kukosea watumishi wakubwa kuliko yeye na waliozungumza na MUNGU moja kwa moja na akawataja kuwa wapenzi wake walifanya kosa hili na kuzidi, Gwajina ni nani hata imekuwa kwamba hawezi kukosea? Je nilazima tumpachike vitu ambavyo hakufanya? Tutumie kiasi kikubwa na pesa kama ‘mlichotumia’ kutayarisha uchafu huu?
Hii ni dhambi kubwa mnafanya wanasiasa . unatumia milioni taklibani 15, ambazo zingesaidia watu maskini, kwa ajiri ya kutayarisha video kama hii na kumpaka matole mchungaji. Kumbuka fanya yote haya lakini sote Duniani tu wapitaji na siku moja tutasimama mbele za MUNGU kujibu yale tunayofanya.
Uwe tajiri usitumie utajiri wako kuonea watu, bali wasaidie igeni kwa mzee wetu Mengi. Kama wewe ni mwanasiasa usitumie nafasi yako kuonea watu igeni kwa mzee wetu Nelson Mandela.
Habari hii
Copy & Paste