Mapungufu makubwa ya kuhamisha Walimu kutoka Sekondari kwenda kufundisha Shule za msingi

Kanyunyu

JF-Expert Member
May 2, 2012
335
495
Habari wana Jamvi

Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI Wiki iliyopita imeanza kuhamisha Walimu kutoka idara ya Sekondari kwenda kufundisha Shule za msingi ili kukabiliana na upungufu wa Walimu. Utaratibu huu wa kuhamisha Walimu Umekuwa ni wa kienyeji sana na usiozingatia taratibu na HAKI za mtumishi husika. Mapungufu makubwa ni kama ifuatavyo,

1. Mwalimu husika anakabidhiwa barua ya uhamisho na kuambiwa Nenda kuripoti haraka Shule ya msingi uliyopangwa na uanze Kazi Mara Moja , hapa hakuna utaratibu wa kuwaandaa Walimu kisaikolojia (semina) kwa ajili ya maandalizi ya kwenda kufundisha Shule za msingi.

2. Hakuna utaratibu wa kuwasafirisha Watumishi kutoka Kituo cha awali kwenda Kituo kipya (hakuna malipo ya nauli na Mizigo) mtumishi atajihamisha Kwa gharama Zake.

3. Hakuna malipo ya usubumbufu

4. Hakuna malipo ya Posho ya kujikimu

5. Hakuna nyumba za Watumishi, mtumishi atajua mwenyewe sehemu ya kukaa anakohamishiwa Kituo kipya. Mishahara kidogo afu nyumba upange Kwa mshahara huohuo mdogo. Huu ni uonevu wa kiwango cha juu sana.

Serikali hii ya awamu ya Tano haina huruma na Watumishi hawa ambao maslahi ya mishahara ni midogo sana na hawajapandishwa madaraja Kwa miaka 3 sasa kutokana na tamko la Rais Magufuli kuzuia Watumishi kupandishwa mishahara na madaraja.


Serikali hii ya wanyonge acheni kutesa Watumishi wa umma, HAKI na WAJIBU ndiyo msingi Mkuu wa Kazi.

Rais Magufuli amekuwa akisisitiza Watumishi wasikubali kuhamishwa bila kulipwa na ni marufuku kumhamisha mtumishi bila kuwa na bajeti ya kumlipa. Hivyo hawa Walimu wana HAKI ya kugomea uhamisho huu mpaka walipwe ?

Kazi kwenu wenye HAKI na nchi hii.
 
Huwa mnalipwa kipindi cha kusimamia uchaguzi. Mbona nasikia hata watakaolipwa mwezi huu madeni yenu hawafiki hata robo ya wanaodai kwa kila halmashauri. Malipo yote 2020 mkisimamia uchaguzi, mkijifanya viburi tunachukua manesi.
 
Ipo siku serikali itaingia hasara...maana huyo mwl unayemuhamisha kwenda msingi ukabakisha baadhi sec...sasa hao waliobaki, wakihama, wakistaafu, wakiacha kazi, wakihamisha vitengo vingine na kifo je, serikali hii itakuwa ina kazi ya kuzunguka mduara....mwisho miaka 10 ya Magu hamna walichofanya bali ni kucheza mduara tu utiao hasara nchi.
 
Huwa mnalipwa kipindi cha kusimamia uchaguzi. Mbona nasikia hata watakaolipwa mwezi huu madeni yenu hawafiki hata robo ya wanaodai kwa kila halmashauri. Malipo yote 2020 mkisimamia uchaguzi, mkijifanya viburi tunachukua manesi.

Tafakari kabla kuandika na kupost!!
 
Elimu na afya maeneo haya hayataki siasa nawashangaa wanaoleta siasa hapa akina jafo.
 
Waziri jafo wa TAMISEMI anapiga maneno tu, mambo yanaenda hovyo sana
 
Watumishi wa umma safari hii wamekutana na kichaa aliyepewa rungu! "watarimia meno"... Wanadhani wanawakomoa kumbe hawajui wanaangamiza Taifa, mbaya zaidi Kuna watu huko mitaani kazi yao kushangilia tuuuu kila linalotamkwa! Elimu buree, wao utasikia oyeeeeeee.... Ukienda mashuleni watoto wanakaa chini na wamejazana darasani kama uyoga halafu kati yao hao watoto hakuna hata mtoto wa mwalimu wa chekechea au afisa mtendaji wa kijiji maana na wao wamejinyima wamewapeleka watoto wao private maana wanajua elimu bora inapatikana mazingira gani!

Mara walimu wa sekondari, PUNGUENI MUENDE MSINGI! Hakuna semina, hakuna maandalizi inakuja kama demosheni ya kiani!!!! Huku wananchi unaskia, "na wakome walikuwa wanajidai sana! Awamu hii hakuna mchezo!!!!! huyu mwalimu anaenda kiunyonge lakini pamoja na unyonge huo anatambua mle darasani hakuna mtoto wake maana hizo senti anajibana kumpeleka mtoto wake sehemu anakojua walimu wanakuwa motivated hata kwa kauli tuu!!

Mwisho wa yote, nani anaumia kati ya watoa matamko na washangilia matamko!!!!!
 
Watumishi wa umma safari hii wamekutana na kichaa aliyepewa rungu! "watarimia meno"... Wanadhani wanawakomoa kumbe hawajui wanaangamiza Taifa, mbaya zaidi Kuna watu huko mitaani kazi yao kushangilia tuuuu kila linalotamkwa! Elimu buree, wao utasikia oyeeeeeee.... Ukienda mashuleni watoto wanakaa chini na wamejazana darasani kama uyoga halafu kati yao hao watoto hakuna hata mtoto wa mwalimu wa chekechea au afisa mtendaji wa kijiji maana na wao wamejinyima wamewapeleka watoto wao private maana wanajua elimu bora inapatikana mazingira gani!

Mara walimu wa sekondari, PUNGUENI MUENDE MSINGI! Hakuna semina, hakuna maandalizi inakuja kama demosheni ya kiani!!!! Huku wananchi unaskia, "na wakome walikuwa wanajidai sana! Awamu hii hakuna mchezo!!!!! huyu mwalimu anaenda kiunyonge lakini pamoja na unyonge huo anatambua mle darasani hakuna mtoto wake maana hizo senti anajibana kumpeleka mtoto wake sehemu anakojua walimu wanakuwa motivated hata kwa kauli tuu!!

Mwisho wa yote, nani anaumia kati ya watoa matamko na washangilia matamko!!!!!
Aisee nichangue kidogo. Serikali hii inaua kabisa elimu ya nchi kwa makusudi, wasomi,mawaziri, na maprofesa wote wapo kimya kutetea matumbo yao kwani wanajua awana watoto mashuleni. Wajue aya sisi walimu tunajibana na kupeleka watoto zetu mahala wanapopeleka wao ata wakitudemote tukafundishe chekechea tutaenda tu lkn watavuna mabua.
Aiwezekani Mimi Mwl nlie somea kufundisha MTU Wa kiwango cha sekondari ukanipeleke kufundisha vitito hii nifedhea kwa taaluma ya ualimu na kejeri.

Pia hii in janja ya serikali kuto taka kuajili kuaminisha watu wamejaa kwa hii kada.
 
Tujifunze kuwa tunatengeza taifa la wajinga na mbumbu wengi siku za usoni kutokuwa na utaratibu unaoeleweka wa elimu yetu katika mawaziri wote walio wahi kutumika hapo huyu ndiye kashindwa zaidi ya wote afadhari hata yule aliye unganisha fiziksi na kemia kuwa somo moja
 
Magufuli bhana, Ujumbe wako kusoma, tena ana fekero kama tatu humu Hahaha aisee kesho kwaresima!
 
Wananchi shangilieni lakin ipo siku mtaelewa kinachafanyika lakin itakuwa mmeshachelewa
 
Back
Top Bottom