Maporomoka Uganda yahofiwa kuuwa watu 300

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125


Chama cha Msalaba Mwekundu nchini Ugabda kimesema watu zaidi ya mia tatu wanahofiwa kufariki dunia kufuatia maporomoko ya ardhi yaliyotokea ...
mashariki mwa nchi hiyo.
Maporomoka hayo yaliyotokana na mvua kubwa, yamesababisha uharibifu mkubwa katika eneo kubwa lenye milima la Bududa, huku vijiji vitatu vikiarifiwa kufukiwa na udongo.

Shirika la Msalaba Mwekundu linaarifu kuwa makundi ya uokoaji yanatumia vifaa vya mkononi kuchimba tope kwa lengo la kuitoa miili ya watu.

Hata hivyo waokoaji wamepata miili hamsini pekee, huku wakiendelea kuwatafuta manusura.
Jeshi la taifa la Uganda nalo linatarajiwa kujiunga na juhudi za uokoaji.

Waziri anayehusika na kukabiliana na majanga nchini Uganda, amesema mazishi ya watu waliofariki dunia yanatarajiwa kufanyika leo.
 
Back
Top Bottom