Hazard CFC
JF-Expert Member
- Apr 7, 2015
- 16,615
- 38,589
Hivi kwani nimeandika nini 😆😆😆Haaaa! Kumbe wa kwetueee
Aya bwana!Hivi kwani nimeandika nini
Mimi wa Tanzania yote
Naomba kirikiri hapo ninywe mbege.kwa ulivyoelezea naona ipo tayari kwa ajili ya kunywewa.
Arifu Hama huko tutakupoteza.kijana mzuri kama wewe kutengeneza mbege hapana kwakweli
Kuna mti unaitwa msesewe unachonga magome yake unaanika then unasaga...unapatikana sana uchagani kuleBosi maelezo yako hayajitosjelezi mkuu, huo uliouita msesewe Ninini, na ukakatika product gani unga,maji,mbegu ama Ninini? Na niwapi unapopatikana? Na kazi yake Ninini? Na nisipoweka athari zake ninni kwenye mbege.
Kati ya ulezi na ndizi zinazotajikana kuwahi kuandaliwa ninini?
Mbona umesahau kutenga samboHatua kwa hatua mapishi ya mbege.
Mahitaji kimjini mjini
1. Ndizi mbivu
2.ulezi
3.msesewe
4.mkaaa
5.ndoo walau 4
5. Maji
Chukua ndizi mbivu zilizoivaa kabisa na kulainika sana,zimenyee kwenye chombo kisafi uziponde ponde( hii inasaidia ziive mapema)..zitie kwennye sufuria zichemshe bila maji mpaka pale zitakapobadilika rangi kabisa na kua na rangi kama kahawi,wakati wakuchemsha zikiwa zinaanza kubadilika rangi weka msesewe husaidia baadae pombe yako kua na ukali..ziepua ndizi zako weka kwenye vikontena usijaze hadi juu na ziache kwa siku saba ndizi zichachuke(zikatike).
Chukua ulezi wako uoshe vizurii na kisha weka kwenye viroba(mifuko iliosha sukari au unga) ziache kwenye mifuko zichujike maji hadi kesho yake, zimimine kwenye sakafu safi zitandaze kwa muda kama masaa 12, sikusanye kwa pamoja zinyunyuzie maji yakutosha kisha changanya hakikisha zote zinapata maji yakutosha,zitandaze tena kisha funika kwa siku moja hadi mbili zianze kuota...baada ya kuota siku mbili zifunue na kuziachanisha kisha kazianike zikaule hapo utakua umepata kimea safii kabisaa...
Baada ya siku saba chukua ndizi zako zile changanya kwenye chombo kimoja kikubwa kisha zitie maji inategemea na vipimo vya ndizi zako,kama ulipika ndoo moja tia maji ndoo mbili, ziache kwa masaa kadhaa kisha tafuta chujio locally unaweza tumia viroba hivi vya kuwekea mchelee kuzichuja ndizi zako ili upate ile juice nyekundu kabisaa..
Kasage ulezi wako(kimea) kisha weka maji ya moto mimina unga wako koroga hakikisha unaiva kabisa na kupata uji zitoo uache upoe..
Chukua ile juice yako ya ndizi kwenye chombo safi pipa au jaba mimina humo kisha chukua ule uji wa ulezi changanya pamojaa...hapo unapata togwa safi kabisaa tenga togwa yako kwa wale wasiotumia kilevi wanaweza kunywa..baada ya hatua hiyo weka msesewe wa kutosha uliosagwa koroga kisha funika....
Subiri kwa siku moja pombe yako itakua tayarii.... wingi wa alcohol kwenye pombe yetu inategemea na ndizi zilizotumika,mda ndizi zilivyokaa kwenye uchachushaji,ulezi n.k
December ndio hiyo wadau twendenii zetu moshi tukapate darasa kwa vitendoo,mimi sio mwelezeaji mzuri sana kwa anaetika kujifunza kwa vitendo asisite kunitafuta
Imeletwa kwenu na hazardihoo
Ndizi za siku Saba sio kwa dar es laam hii mkuu!Kuna mti unaitwa msesewe unachonga magome yake unaanika then unasaga...unapatikana sana uchagani kule
Ulezi unaweza kuaandaa siku yoyote ila ndizi ni ndani ya siku saba
Msesewe baada ya kuchanganya ukezi ulopikwa kwenye ndizi ulokamua (hiyo siku ya pombe kamili sasa)kama sukari inakhwa imezidi ndio unatia huo msesewe kama vijiko 2 hivi ili kuongeza uchungu fulaniBosi maelezo yako hayajitosjelezi mkuu, huo uliouita msesewe Ninini, na ukakatika product gani unga,maji,mbegu ama Ninini? Na niwapi unapopatikana? Na kazi yake Ninini? Na nisipoweka athari zake ninni kwenye mbege.
Kati ya ulezi na ndizi zinazotajikana kuwahi kuandaliwa ninini?
Najua kupika dadiii,gongo,wanzuki,mbege japo kwa tabu sana(kuinywa najua vizuri mno)nini tena nimesahau😅😅😅eheee ndo hivyoUnajua kuipika ama utaishia kuunguza tu.
😅😅😅😅tunawapenda hivyo hivyo mangi..hivi na wewe si ulikuwa wa daa eebakini na wanaume wenu wa dar
Msesewe Ni mti mchungu mno ukiukata unatoa maziwa maziwa unatoa vitunda vya kijani size ya zabibu!Bosi maelezo yako hayajitosjelezi mkuu, huo uliouita msesewe Ninini, na ukakatika product gani unga,maji,mbegu ama Ninini? Na niwapi unapopatikana? Na kazi yake Ninini? Na nisipoweka athari zake ninni kwenye mbege.
Kati ya ulezi na ndizi zinazotajikana kuwahi kuandaliwa ninini?
Naufaham mkuu, nilikua nataka mleta mada aende ndani kidogo, nijuavyo Mimi sio kiungo Cha lazima kwenye maandalizi ya mbege.Msesewe Ni mti mchungu mno ukiukata unatoa maziwa maziwa unatoa vitunda vya kijani size ya zabibu!
Jina la kisayansi unaitwa rauvoflia caffra ingia Google utauona
Zamaniitunawapenda hivyo hivyo mangi..hivi na wewe si ulikuwa wa daa ee
Ni subiria mapishi ya gongo nipate kulewa vizuriZamanii
Soon nawaletea mapishi ya gongoo