Mapishi ya nyama ya kuku

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,319
33,125
Mapishi ya nyama ya kuku na tangawizi

Mahitaji
20070515181326.jpg


Nyama ya kuku, tangawizi gramu 10, vitunguu maji gramu 5, siki kijiko kimoja, mchuzi wa sosi kijiko kimoja, mvinyo wa kupikia kijiko kimoja, maji ya wanga vijiko viwili.

Njia

1. kata nyama ya kuku iwe vipande vipande, washa moto, mimina mafuta kwenye sufuria, mpaka yawe joto la nyuzi 60, tia vipande vya nyama ya kuku na tangawizi korogakoroga, halafu tia chumvi, vitunguu maji, korogakoroga, tia mchuzi wa soya na maji.
2. baada ya dakika 5, tia vitunguu maji na mimina maji ya wanga, korogakoroga, mimina siki korogakoroga, baada ya maji ikukauka, ipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari.


Mapishi ya supu ya tufaha na nyama nofu


Mahitaji:
CI5473HAG74JH63E3J.jpg

Tufaha moja, nyama nofu gramu 50, karoti moja, tende gramu 10, uyoga mweupe gramu 10, chumvi kijiko kimoja

Njia:

1. kata nyama nofu iwe vipandevipande, ondoa punje ya tufaha na kata tufaha iwe vipande, kata karoti iwe vipande vipande.
2. washa moto, tia mafuta kidogo kwenye sufuria, halafu tia vipande vya nyama nofu, korogakoroga, vipakue.
3. washa moto tena, mimina maji bakuli 6 kwenye sufuria, tia vipande vya nyama nofu, tufaha, karoti na tende kwenye sufuria, korogakoroga, baada ya kuchemka punguza moto, iendelee kuchemka, baada ya dakika 10, tia uyoga mweupe, endelee kuchemsha kwa dakika 20. tia chumvi, halafu ipakue. Mpaka hapo supu hiyo iko tayari kuwakunywa.


Mapishi ya mseto wa kuku

Mahitaji
111_g37tq3OFnzzv.jpg

Pilipili mboga moja, nyama ya kuku gramu 50, yai moja, mboga gramu 20, vitunguu maji gramu 5, bakuli moja la wali, sosi ya kambamti gramu 5, chumvi gramu 5.
Njia
1. kata pilipili mboga na nyama ya kuku iwe vipande vipande na kasha livunje yai na vilikoroge yai.
2. washa mototia mafuta kwenye sufuria, halafu mimina yai lililokorogwa, likaange yai na lipakue
3. washa moto tena, tia vipande vya vitunguu maji, na korogakoroga kasha tia vipande vya nyama ya kuku, na vikoroga, halafu tia mboga na vipande vya pilipili mboga, sosi ya kambamti, na korogakoroga, halafu tia wali, na punguza moto, baada ya kupunguza moto korogakoroga kwa haraka, tia chumvi pamoja na chembechembe za kukoleza ladha, korogakoroga, kasha ipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom