Mapishi mbalimbali ya Karanga za kukaanga

Habari za mlo kwa wakati huu.

Jamani naomba kuelekezwa jinsi ya kutengeneza karanga za mayai..Napendaga sana tena saana tu ila naishiaga kununua tu supermarket nakwingineko.

Siku moja buana nkajifanya nazitengeneza mwenyewe kwa kuzipimia kisimpo simpo tu haaaaaa kilitoka kituko sijawahi ona sema nlikula hivohivo tu kwa kuonea huruma malighafi zangu especially mayai.

Roho inaniuma kununua nunua jamani wakati I think all materials needed for that are available at my place karanga za kumwaga mayai ndio usiseme tena ya kienyeji sh 250 tu.Anayejua anipe procedures jamani.

Bila kumsahau mwenyekiti wa kamati ya mapishi farkhina

Nawasilisha.

fuata hatua, zitatoka tamuu.
 
wanakula,hata maandazi ye anaweka chumvi siku akijisikia kula.

Mwambie aache hiyo tabiaa anajizuruuu atapata retention ya water mwilini aanze kuvimba maji mwili mzimaaa.aende akamuone daktari kwa ushauri mzuri jinsi ya kujitake care
 
Wanajamvi naomba kufundishwa kupika karanga za mayai na crips nahitaj kufanya biashara ndogo ndog maisha magum sana naomba mnifundishe kupika ivyo

=============
=============================

Mahitaji

Karanga mbichi 400gm
Chumvi pinch moja
Yai moja
Sukari vijiko viwili vya chakula
Unga wa ngano 1/3 cup

Jinsi ya kupika
Roweka karanga zako kwenye chumvi,(unaweza kuzikausha kidogo)
Changanya Yai na sukari changanya hadi uwe mweupe weka karanga hadi zote zienee mchanganyiko wa Yai weka ngano hadi uone inanata.
Weka mafuta jikoni yakichemka weka karanga zikiwa brown toa weka katika chujio zitoke mafuta.
 
Nimeona West Africans wanafanya crisps za ndizi mzuzu, ni tamu sana, una slice ndizi zilizoanza kuiva, unaanika zinakauka, unakaanga kwenye mafuta ya moto sana kwa dakika moja tu una toa na kuacha zipoe then una pack. Bishara ikiwa kubwa una kausha kwa umeme badala ya jua.
 
Wanajamvi naomba kufundishwa kupika karanga za mayai na crips nahitaj kufanya biashara ndogo ndog maisha magum sana naomba mnifundishe kupika ivyo
Asnte sana nipo tabora kupata ndiz mzuzu ni kazi ngoja nipambane asante sana
Nimeona West Africans wanafanya crisps za ndizi mzuzu, ni tamu sana, una slice ndizi zilizoanza kuiva, unaanika zinakauka, unakaanga kwenye mafuta ya moto sana kwa dakika moja tu una toa na kuacha zipoe then una pack. Bishara ikiwa kubwa una kausha kwa umeme badala ya jua.
 
Mahitaji

Karanga mbichi 400gm
Chumvi pinch moja
Yai moja
Sukari vijiko viwili vya chakula
Unga wa ngano 1/3 cup

Jinsi ya kupika
Roweka karanga zako kwenye chumvi,(unaweza kuzikausha kidogo)
Changanya Yai na sukari changanya hadi uwe mweupe weka karanga hadi zote zienee mchanganyiko wa Yai weka ngano hadi uone inanata.
Weka mafuta jikoni yakichemka weka karanga zikiwa brown toa weka katika chujio zitoke mafuta.
 
Nimeona West Africans wanafanya crisps za ndizi mzuzu, ni tamu sana, una slice ndizi zilizoanza kuiva, unaanika zinakauka, unakaanga kwenye mafuta ya moto sana kwa dakika moja tu una toa na kuacha zipoe then una pack. Bishara ikiwa kubwa una kausha kwa umeme badala ya jua.
Aisee hizo crisps ni tamuu.
 
Chumvi kijiko kimoja kidogo au kikubwa,pia kwa wewe sukari huwa unaweka kiasi gani kwa karanga kg1?
 
Hizo mnazoziita karanga za mayai mimi nazipika tofauti kidogo, situmii mayai natumia unga wa dengu:
Mahitaji:
-Karanga (zile ndogo nyeupe)1kg
-Unga wa dengu robo kilo (unaweza ongeza kidogo lkn isifike nusu kilo)
-Chumvi kijiko komoja kikubwa
.
.
Chambua karanga zioshe, weka unga wa dengu,chumvi na maji kiasi, maji yasisimame bali unga unate kwenye karanga.
Pasha mafuta moto (kama unavyopika maandazi). Weka karanga chache kwenye mafuta huku ukizichambuachambua ziachane, kaanga mpk utakaposikia zinapasuka kama popcorn zitoe haraka usiunguze.
.
Jaribuni hii mtaniambia.
Kama unafanya biashara ni vizuri kutumia unga wa dengu maana mayai ni gharama sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom