Thomas Odera
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 673
- 155
Ni nini hasa kimesababisha hali kuwa hivo? Je ni kuporomoka kwa uchumi wa nchi hizo au ni wananchi wamechoka kuona utawala moja unakaa madarakani muda mrefu na pia bila chaguzi huru?
Hiyo ni sababu moja wapo, lakini kubwa ni utawala wa kislamu wa kiimla. Kwa sababu uislam si dini, kama dini nyingine ambazo huwa zinaeleza waumini wao kuwa hapa duniani tunapita tu, lakini uislam unakuwa hapa kama ndiyo mwisho, hamna maisha mengine. Ukiangalia ndiyo maana hakuna tofauti ya dini ya kiislamu na siasa. Hilo linapelekea kuwa na nchi zinazo tawaliwa kwa kutumia sheria za kiislamu. kama iran. Kwa upande mwingine biblia inapinga kujiingiza kwenye siasa za nchi. mathalan, Yesu Kristo alipokamatwa ili afanywe mfalme wa Wayahudi, alisema kuwa ufalme wake si wa hapa duniani hii. Akakimbia hakutaka awe mfalme. Hivyo ukristo hauingilii wala kupinga siasa (licha ya kuwa kuna wanadini wanoingia kwenye siasa kimakosa) lakini kwa uislam ni tofauti, unaingilia siasa.