Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,621
- 46,268
Mapigano yameripotiwa kati ya mamluki wa Wagner group na Jeshi rasmi la Urusi, wapiganaji kadhaa wa Wagner wanaripotiwa kuuawa katika shambulizi liliofanywa na Jeshi la Urusi.
Baadhi ya vyanzo vya taarifa vinadai Wagner wanafanya jaribio la mapinduzi na wanataka kuanza kwa kuuondoa uongozi wa Jeshi la Urusi. Prighozin ametoa kauli kwamba viongozi wa vyombo vya usalama na jeshi la Urusi walimdanganya Putin kuivamia Ukraine na kwamba vita hiyo haikuwa na ulazima, ilikuwa inaepukika!
Rais wa Putin ametoa kauli kwamba anaelewa kinachoendelea katika kundi la Wagner group.
Taarifa zaidi kwa kina zitaendelea kuletwa kadri zinavyopatikana.
Baadhi ya vyanzo vya taarifa vinadai Wagner wanafanya jaribio la mapinduzi na wanataka kuanza kwa kuuondoa uongozi wa Jeshi la Urusi. Prighozin ametoa kauli kwamba viongozi wa vyombo vya usalama na jeshi la Urusi walimdanganya Putin kuivamia Ukraine na kwamba vita hiyo haikuwa na ulazima, ilikuwa inaepukika!
Rais wa Putin ametoa kauli kwamba anaelewa kinachoendelea katika kundi la Wagner group.
Taarifa zaidi kwa kina zitaendelea kuletwa kadri zinavyopatikana.