Mapenzi yanaua ubongo wa wanaume.

Tabutupu

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2010
Posts
13,262
Reaction score
18,711
Mapenzi yanahusisha 100% ubongo. Umewahi jiuliza kwanini baada ya kufanya mapenzi unapata usingizi wa ajabu ?

Hii ni kwa sababu ubongo unakua umetumika sana kiasi kutokua na uwezo wa kuuhudumia mwili.

Wanaume ambao hawafanyi mapenzi huwa wanakua na nguvu kiakili kuliko wanao fanya mapenzi

Kutokana na hivyo wanaume wanao fanya mapenzi huzeeka mapema kutokana na ubongo wao kupunguza uwezo wa kuhudumia mwili.

Mapenzi yanachosha akili kuliko mwili.
 
Uongo ni dhambi ndugu,maana hapa haijulikani umetoa elimu isiyo na ushahidi au unahubili
 
Huo ndio ukweli
Unge-ambatisha na reference juu ya hii Topic yako inge leta mantiki sana ---

Hiki unacho kisema kwa upande fulani kina ukweli -ndio maana tunaona ma -Padre wakiwa Wanaishi miaka mingi sana --kwa sababu hawaoi -so hata kama huwa wanafanya ngono huwa ni kwa kificho sana --hali hiyo hupelekea kwa wao kujikuta wa kifanya ngono Mara chache tofauti na mtu mwingine ambaye anaishi maisha ya kawaida
 
Nachoweza kusema ni kwamba binafsi sijawahi kuoa na sina mpango kwa sasa kulingana na mazingira yangu yalivyo unachosema kina weza sema ni kweli na kinahusishwa na watu ya jamii mbili nayo ni walevi na wenye lishe duni kama mimi binafsi nina karibu miaka miwili sijawahi kulala na mwanamke au dada poa sio sifa ila mazingira yamenibidi niwe hivyo kwa hali hiyo inapelekea hata nikichelewa kulala najikuta nimewahi kuamka itaendelea...... ...
 

Si kweli.Hili suala si dogo kama unavyolielezea. Huwezi kumpima padre kwa kigezo hiki cha kufanya mapenzi pekee.Kwanza ni jambo linalohitaji utafiti wa kina,maana maisha ya binadamu hutawaliwa na mambo mengi. Unajua changamoto anazokutana nazo mtu mwenye mke/familia ukilinganisha na asiyekuwa na mke? Kuanza kufikiria familia itakula nini,wamevaa nini,wamesoma wapi n.k.,jumlisha aina ya maisha unayoishi na mwanamke wako,huenda maisha ni full stress.Hii ni mifano tu, kuna maelfu ya vitu vinavyoweza kuingilia mfumo wa akili na kuathiri maisha ya mtu na pengine hata kufupisha maisha.

Zingatia

Kama nilivyosema,suala hili ni tata, halina majibu ya moja kwa moja.Kutokuwa na mke se guarantee ya mtu kuishi muda mrefu,bado itategemea unaishi vip.Yawezekana huna mke au familia na bado ukawa na majukumu mengi kuliko hata mwenye mke na watoto.Au kama wewe ni mlevi kupindukia,huna uhakika wa kula na pa kulala,bado itakuwa ni tatizo.Hapa aliyeoa na kuwa na maisha bora atakuwa vizuri kushinda wewe usiyeoa.

Kwa kifupi tusiongee mambo yanayohitaji utafiti kirahisi hivi wandugu.Mambo haya ni tata,hayana jibu moja.
 
Huo mfano wa Padre kuto shiriki ngono Mara kwa mara nilioutoa ulikuwa ni mfano 1 wapo'' Ambao una base kwenye hii Topic. ..Nikweli kwamba Kuna sababu nyingi ambazo Zina changia life span ya wanaume kuwa ndogo uki - compare na wanawake -..Moja wapo ikiwa ni stress changamoto mbali mbali za kazi --kama unavyo jua kazi nyingi hatarishi huwa zinafanywa na wanaume ''etc ...

Lakini licha ya sababu hizo nilizo zitaja hauwezi kuu-ondoa ufanyaji wa ngono uliopitiliza budi kuwa ni moja ya vyanzo vinavyo changia kwa mwanaume kuwa na life span ndogo ....haswaa sisi wanaume tunao ishi Africa ---kwa sababu ni wachache sana kati yetu wanaopata Lishe bora
 


Kuna kaukweli fulani kwa mbali.

Ngoja nitafanya kautafiti juu ya Jogoo kwa sababu yeye katika mambo hayo hajambo kwani kila akiona "demu" mpya anaye.
 
Kuna kaukweli fulani kwa mbali.

Ngoja nitafanya kautafiti juu ya Jogoo kwa sababu yeye katika mambo hayo hajambo kwani kila akiona "demu" mpya anaye.

Sasa yeye,jogoo, huwa anachinjwa.Hahaahaa
 


Ni kweli ubongo hufa kwa sababu ya kufanya mapenzi, na ubongo ukifa hata fikra zinakufa, mfano mdogo chukua jogoo akitoka bandani asubuhi badala ya yeye kula chakula ili ashibe utamuona kwanza anamuita jike ale--- huo ni ugonjwa wa akili kutokana na kufanya mapenzi nadhani hata kwa binadamu ni hivyo hivyo.
 
Naweza kuamini kwa sababu nelson Mandela alifungwa miaka 27.it means papuchi alikua haipat Mara kwa Mara na ndio maana ameish miaka ming sana( 95+)
 

Acha tu nizeeke yan niachekujilia mema Ya Nchi kwa kuogopa kuzeeka,na Hamna kazi nyengine iliyotuleta hapa duniani zaidi Ya mapenzi dini yenyewe imesema tupendane na imesisitiza tuujaze ulimwengu.
 
Mbona mnatuchanganya jameni nilishawai kusoma makala moja hivi kuhusiana na kufanya mapenzi, kwa mujibu wa iyo makala kufanya mapenzi ni tiba kiafya
 
Asante kwa mawazo,ila wacha tu tuzeeke mapema...
 
Mithali 6:32
[32]Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa;
Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…