Mapenzi si pesa

kwisha

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2021
Posts
1,788
Reaction score
5,027
Kuna watu wanatudanganya kuwa mapenzi pesa lakini siyo kweli. Kuna mwanamke nipo naye kwenye mahusiano, nilimkuta hana simu kubwa nikamnunulia simu kubwa ili kuepusha matatizo ya salio kila siku. Pia nilimkuta hana mavazi mazuri nikatoa pesa zangu kumnunulia mavazi.

Lakini naona moyo wake kwangu haupo kabisa, najaribu kufosi kumpa vijizawadi lakini wapi. Kweli anasema ananipenda, lakini siyo ile mapenzi ya asili.

Nilichojifunza pesa siyo mapenzi. Mpaka leo nimeongea naye, nikampa tu ukweli kuwa hana mapenzi ya kweli kwangu ila anafosi tu kuwa na mimi. Kwahiyo basi nimemwambia tuachane, lakini tubaki kuwa marafiki ili nimpe uhuru wa kutafuta atakaye mfurahisha.
 
mkuu wa kukupenda kiukweli ni mother home,huko kwingine siku hizi tunafuata kukojoa,hilo mwanangu chimbo lako muda wowote ukijisikia tu unaamsha
 
Ni kweli kabisa mapenzi si pesa. Ila pesa muhimu katika mapenzi.

Huyo dada hajakupenda na hana elements za udangaji.
 
Mtoa mada mbona unajikanyaga kanyaga mwenyewe kwenye Uzi wako?

So umesema mapenzi si pesa sasa mbona unamnunua Simu janja na mavazi?
 
Mtoa mada mbona unajikanyaga kanyaga mwenyewe kwenye Uzi wako?

So umesema mapenzi si pesa sasa mbona unamnunua Simu janja na mavazi?
Kasema hivo baada ya kutumia pesa zake kwa uyo bidada nakuona kwamba hazijamsaidia kupata mapenzi yake ya kweli.
 
Ukweli mchungu ni kwamba wanawake ndio wanafaidika sana na mapenzi kuliko wanaume.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…