Mapenzi ni mtihani

Mapenzi ni mtihani

Tony Yeyo

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2014
Posts
733
Reaction score
567
Nilikutana na huyu binti nikiwa nchi za nje nasoma. Baba yake alikuwa balozi wa nchi moja ya Africa Magharibi. Huyu binti nilikutana nae akiwa na umri wa miaka 18 mimi nina 23 yaani baada ya Miaka 6 mimi wazazi wake walihama nchi yaani toka Europe kurudi Africa mana muda wao wa kustaafu ulifika.

Mimi na huyu binti tulipendana sana lakini mimi nilikataa kumuoa kwa maana niliona atapata tabu kwenda kuishi Tanzania ila Kwa upande mwingine niliona kama uzuri wake unapungua kadri muda unavyokwenda ila yeye alizidisha mapenzi yake kwangu na kila siku anataka tuongee kuhusu masuala ya ndoa.

Basi nikamwambia wewe ukifika Africa mimi nitampigia simu babako nitamueleza kwa maana familia yake wote wananitambua.

Mimi bado nikabaki Europe, alipofika Africa mimi nikabadilika nikamwambi hatuwezi kuoana. Alijaribu sana kunibembeleza nikakataa.

Tatizo nililo nalo sasa muda mwingi hunijia katika mawazo yangu namuwaza yeye, niliishi nae muda mrefu na tulizoena na najiskia vibaya kwamba nilimgeuka ila nilikuwa sina jinsi.

Wiki iliyopita kanipigia simu na kuniambia anafunga ndoa basi mpaka leo namuwaza huyu binti.Naomba Mungu anisamehe maana nilitoa ahadi ya uongo na yeye aliniamini.

Naamini atapata mpenzi mwingine na ataishi maisha mazuri . Ila kwa upande wangu sijui kama nitapata tena msichana kama yule.

 
Ulaya ulikwenda kwa boti ukitokea Libya. mbona hunipi picha kam wewe umepitia shule ? au uko ulaya ndogo yaani Lushoto
 
Watu waongo kama nyie, ndo mnaponza wote tuonekane hamnazo.
Bora aolewe zake, we baki na usaliti wako labda utapata msaliti mwenzako.
 
jaribu kupitia halafu uone kuna mahali umesema anaolewa mara unamuombea apate mpenzi...
 
Ulipata dhahabu ya kweli ukaitupa jalalani,sasa tegemea kuokota ya bandia .
 
Tuseme sasa hvi una age 31+ kama ulimsaliti wakati unajua huwezi kupata mwingne ongea na dada zako umchomoe mmoja
 
Mbona unalialia!...kwani wewe si ulijipanga kwa kukataa.

Ulaya mbaya sana inaharibu hata uwezo wa kuandika Rugha yako ya Asili
 
Sidhani kama unajua maana ya neno kupenda...
 
Kama ulimuachia akaondoka haina haja ya kuendelea kumuwaza tena.
 
sasa unalalama nn akat uamz ulifanya mwenyew...tulia kijana golden chance never come twice

tafta mwingne na yy aje akuache uone uchungu wa kuachwa
 
Unajiskia sababu ulipendwa, ngoja uje ukutane na manyang'au ndo utatia akili.
 
BINADAMU NI MTIHANI, MAPENZI TUNAYASINGIZIA SABABU NI LAZIMA BINADAMU WAKUTANE. Fikiri juu ya marafiki walioanza pamoja biashara kisha baada ya mafanikio makubwa wakadhulumiana au hata mmoja kumuua mwingine, jumlisha na matukio mengi mchanganyiko, utanielewa. Napita.
 
Mbona unalialia!...kwani wewe si ulijipanga kwa kukataa.

Ulaya mbaya sana inaharibu hata uwezo wa kuandika Rugha yako ya Asili

Na wewe uliyebaki unaandika RUGHA nzuri
 
Back
Top Bottom