Mapenzi hayathaminiwi kabisa siku hizi

Mapenzi hayathaminiwi kabisa siku hizi

RingaRinga

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2015
Posts
1,052
Reaction score
529
Nadhani ni ile misemo ya watoto wa mjini, siku hizi wanasema mapenzi pesa sjui mapenz kitu gani! Kwamba maua mpelekee kipepeo sjui, romance mpelekee njiwa!

Lakini nnachotaka kusema hapa ni kuwa ile role ya mapenzi kwishney kabisa, if still exists it's very rare and to very few human beings, men to women utulivu ziro hata kwa usiowafikiria unaowaona wametulia ubinafsi mwiingi!

Hakuna shukrani! hakuna fadhila.

Unakutana na mdada unampenda,unaanza nae mahusiano, unamwonyesha total love, very responsible love, highly committed! Unamjali kuanzia yeye hadi ndugu zake, humpi kupumua kwa kumwonyesha mapenzi mfululizo.

Inapokuja wewe unauhitaji hata wa faraja tu kutokana na matatizo ya kidunia labda unauguliwa na mama au mwanafamilia yeyote pale ulipozaliwa, unategemea atakuwa na wewe bega kwa bega, ndipo unakutana na vituko.

Inakatisha tamaa sana, kwani mapenzi tuyaonayo kwenye tamithilia hatujifunzi? Au hayawezekani? Kinachoshindikana ni nini hadi tuweke slogan ya kuvumiliana?

Unaweza hata ukamkuta mtu katika matatizo makubwa ukampenda kwa huruma na dhati, ukamtoa katika shida zake, sasa mwenzio hapo anahesabu ameukata, akishakaa sawa hapo hajishughulishi tena, hata kwenda kununua nyanya chungu sokoni nusu km atachukua bodaboda, hafanyi chochote kusave currance ila kutumia.

Amekuwa bize kufanya mambo ambayo hayana tija, kutafta marafiki wapya wa ile anayoiona kuwa ni hadhi yake ya sasa ambao hupoteza muda kufuatiliana maisha badala ya kufanya mambo binafsi. Hata mkizaa hajishughulishi na watoto utadhani amekuzalia wewe yeye hawamhusu.

NIMECHOKA!

Sasa ndugu zangu nitaftieni mke wa kuoa, tena napenda aliepitia shida za mapenzi ili nimfariji astawi, awe mzuri wa wastani tu hata akiwa na watoto angalau wasizidi wawili na tukiongeza mmoja wakutuunganisha tunapeta.

Nishaurini wanajamvi
 
kama hakuna upendo maana yake hakuna maisha
hebu tafuta watu na mapenzi yao
 
kama hakuna upendo maana yake hakuna maisha
hebu tafuta watu na mapenzi yao

Kuna haja ya kuanza kupitapita maeneo yenye ajira za vibarua vinavohusisha wanawake labda ntapata, ni raha sana kumpata alietokea chini mkafaulu kumake, mtaheshimiana, kuthaminiana ba kupendana sana, shida ni namna ya kumfaham kuwa huyu ni yule nnayemhitaji.
 
Sasa tukutafutie huku tulipo au wapi,au kama wapo tuku connect nao kwa njia gani.

Uko mkoa gani miss rose? mi niko mwanza nisaidie daangu ntatoa mahari kwa wazazi wa mwenzi na kwako km utanifanikishia wa kiwango mamaangu
 
Pole sana brother.... Huenda unatafuta wanawake wa kileo...madada duu...hawa hawajui kitu zaid ya kuangalia status na kutumia peza zako unazopata kwa jasho na mateso...

Kimsingi mwanamke yeyote atakuumiza tuu kwa namna moja au nyingine...jambo la muhimu ni kutafuta yule ambae ana thamani ya chozi lako.... Tuliza akili potezea na soon utamuona yule ambae mungu amekutafutia maana maandiko yanasema mungu hukupa yule unaefanana nae...
 
nenda pale kwa kimboka buguruni utawakuta kibao ukimtoa pale barabarani ukaweka ndani unaanza nae maisha na kila kitu kinakuwa fresh kabisa no stress
 
Kwa miaka hii inatakiwa uombe Mungu sana akusaidie kumpata msichana unaemtaka kuishi nae. Kuna jamaa juzi alikuwa analalamika kampata binti wakakubaliana kuwa marafiki na hatimaye waje kuishi wote. Binti alikuwa na simu ya kawaida. Jamaa akajaribu kumpandisha hadhi akampa smartphone. Yule binti akaingia mitandao ya kijamii akapata marafiki wengi wa kiume. Sasa hivi hata maelewano hakuna tena. Hayo ndio mambo ya kisasa. Kwa hiyo inatakiwa uvumilivu na kumuomba Mungu akuongoze kutafuta mwenza wa maisha.
 
Nadhani ni ile misemo ya watoto wa mjini, siku hizi wanasema mapenzi pesa sjui mapenz kitu gani! Kwamba maua mpelekee kipepeo sjui, romance mpelekee njiwa!

Lakini nnachotaka kusema hapa no kuwa ile role ya mapenzi kwishney kabisa, if still exists very rare and to very few human beings, men to women utulivu ziro hata kwa usiowafikiria unaowaona wametulia ubinafsi mwingi!

Hakuna shukrani! hakuna fadhila.

Unakutana na mdada unampenda,unaanza nae mahusiano, unamwonyesha total love, vety responsible love, highly committed! Unamjali kuanzia yeye hadi ndugu zake, humpi kupumua kwa kumwonyesha mapenzi mfululizo.

Inapokuja wewe unauhitaji hata wa faraja tu kutokana na matatizo ya kidunia labda unauguliwa na mama au mwanafamilia yeyote pale ulipozaliwa, unategemea atakuwa na wewe bega kwa bega, ndipo unakutana na vituko.

Inakatisha tamaa sana, kwani mapenzi tuyaonayo kwenye tamithilia hatujifunzi? Au hayawezekani? Kinachoshindikana ni nini hadi tuweke slogan ya kuvumiliana?

Unaweza hata ukamkuta mtu katika matatizo makubwa ukampenda kwa huruma na dhati, ukamtoa katika shida zake, sasa mwenzio hapo anahesabu ameukata, akishakaa sawa hapo hajishughulishi tena, hata kwenda kununua nyanya chungu sokoni atachukua bodaboda, hafanyi chochote kusave currance ila kutumia.

Amekuwa bize kufanya mambo ambayo hayana tija, kutafta marafiki wapya wa hadhi yake ambao hupoteza muda kufuatiliana maisha badala ya kufanya mambo binafsi. Hata mlizaa hajishughulishi ma watoto utadhani amekuzalia wewe yeye hawamhusu.

NIMECHOKA!

Sasa ndugu zangu nitaftieni mke wa kuoa, tena napenda aliepitia shida za mapenzi ili nimfariji astawi, awe mzuri wa wastani tu hata akiwa na watoto angalau wasizidi wawili na tukiongeza mmoja wakutuunganisha tunapeta.

Nishaurini wanajamvi

Nitafutee mkuuu!
 
Pole xana mkuu,ila inavyoenekana we ndio ulimpenda shemeji ila shemeji alikukubal kutokana na misaada yako.
 
Pesa unazo lakini au?
Maana sie tunajijua, bila pesa sawa na kusubiri daladala la Mbagala Bagamoyo
 
Back
Top Bottom