umenikumbusha mbaaaaali!!!miaka hiyoo nilipatwa na mkasa kama wako!!nikayachukia malovee na sikutaka kuanzisha mahusiano mengine tena!ikapita 2years kama wewe vile,nilikuwa namuota na kuwaza kila dakika!roho iliuma mfano hakuna!!ndugu na marafiki wote walishindwa kuturudisha pamoja!ahahaha.
Mwisho nikakata tamaa ikawa sipokei zake wala sms sijibu,nikawa na hasira kwelikweli juu yake mwishowe nikahamia kwa sister wangu mkoa mwingineee!
Wiki tatu baada ya kuhama nikashangaa bwana mkubwa huyu hapa mlangoni na am sorry kibao!blah blah zikaendelea miezi miwili mbele tukafunga ndoa.
Mpaka leo namuuliza ilikuaje ukarudi tena hanijibu zaidi ya kua mkali kama pilipili ili usimuulize tena maswali ya namna hiyo.
Unaweza ukatokewa na miujiza kama wa kwangu,usikate tamaa dada penzi la kweli halifi.