Mapendekezo ya 'Ruti' mpya Dar

Mapendekezo ya 'Ruti' mpya Dar

Habari,

Jiji la Dar es salaam linakuwa na kutanuka kwa kasi sana. Lakini kuna maeneo yamefikiwa na barabara lakini hakuna huduma za usafiri wa Umma kuyafikia maeneo hayo.

Nimewahi kupendekeza ruti kadhaa huko awali na zikafanyiwa kazi hivyo napata hamasa ya kupendekeza nyingine kwa imani kuwa zitakuwa msaada kwa wakazi wa maeneo hayo.
1. Bunju-Kariakoo(Magari Makubwa)
2. Bunju-Posta(Magari Makubwa)
3. Madale-Makumbusho(kupitia makongo juu)
4. Kawe-Kimara(kupitia njia nne, matosa)
5. Mawasiliano-Kinyerezi/Segerea( kupitia Kimara, Bonyokwa)
6.Madele-Makumbusho(kupitia Tegeta kibaoni) hii ilikuwepo lakini sijajua kilichoiua.

Kwasababu kuna kituo kipya Mwenge kikianza baadhi ya ruti zinaweza kuanzia hapo pia. Hii itapunguza usumbufu na gharama kwa wananchi.

Mbezi bunju kwa kupitia mpigi magoe,mbezi mbunju kupitia kibamba njia panda ya shule,mbezi mapinga kupitia kibaha tamko,
 
NINAPENDEKEZA ROUTE YA MBEZI LOIS magufuli terminal kwenda SEGEREA Kupitia Temboni Kupitia Saranga via Kinyerezi Mwisho/Shule/njia mahakamani hadi SEGEREA.

HII ROUTE NI MUHIMU SANA KUCHUKUA ABIRIA WA SARANGA,GOLAN N, KINYEREZI

(NAWASILISHA)
 
1.Watu wa bunju vita yenu kwa sasa haipaswi kuwa daladala za bunju-kariakoo/kivukoni bali vita na mapambano yenu kwa sasa yanapaswa kuhakikisha miundombinu ya mwendokasi inafika hadi bunju mwisho badala ya ilivyopangwa sasa kuishia tegeta hii ndio solution ya kudumu maana very soon,hizo route zote za daladala kuelekea mjini zitakufa mwendokasi ikikamilika ujenzi wake.

2.hali kadhalika kwa watu wa chanika mnapaswa kupigia kelele miundombinu ya mwendokasi isiishie gongo la mboto bali ifike hadi chanika mwisho hyo ndio suluhu ya kudumu kuwaunganisha na city center.

3.kwa swala la ruti mpya za daladala mimi maoni yangu ni serikali kubadili mfumo wa wao kuwa ndo wenye mamlaka ya kuanzisha route mpya bali waweke utaratibu wa mtu yeyote atakaetaka kuoperate kwenye route fulani apeleke maombi afanyiwe assessment ya nauli kisha apewe kibali cha kuoperate kwenye hyo route sambamba na kupangiwa kiwango cha nauli nakisha route kusajiliwa rasmi, kwa kufanya hivi tutaibua ruti nyingi mno nzuri na zenye tija hivo kuboresha usafiri wa umma na maisha ya wakazi wa jiji la dar es salaam kwa ujumla.
 
Buza-kawe via Mandela road

Bunju - kawe via Ununio

Mbagala- g/mboto via Buza

etc

Zipo route nyingi hazina usafiri ila nasikia unaweza kubuni route yako ukapewa TLB as long as inakidhi vigezo vya LATRA
 
Msisahau kuwa magari ya abilia hayo mnaita daladala nyingi hazitafika katikati ya mji as kariakoo, posta au kivukoni Sababu mfumo mpya ni UDART.

Daladala zinaishia eneo la malishio as pale mwenge, mbezi, Morocco nk, hayo ni maeneo ambayo tayari UDART wana access.
 
Kuna route mpya ya Mbezi kimara korogwe maji chumvi - mnazi mmoja kupitia buguruni au kigogo, ipo poa sana , inawasaidia hadi baadhi ya wakazi wa tabata kimanga kwenda mbezi kwa urahisi
 
Back
Top Bottom