Mapendekezo: Serikali ipitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa na TISS iundwe upya kwa maslahi ya taifa

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
Katika miezi ya hivi karibuni kumekuwepo na mijadala mbalimbali inayohusu idara ya usalama Tanzania ijulikanayo kama TISS.

Mijadala hiyo imeelekezwa zaidi kwenye kuishutumu idara hiyo kwa kujishughulisha zaidi ya ukandamizaji wa haki za binadamu na kuwadhibiti wapinzani wa serikali inayoongozwa na chama tawala cha CCM.

Mimi, binafsi lazima niseme ukweli, nimependezwa sana na kasi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali na sekta mbalimbali nchini mwetu.

Pia nimependezwa na juhudi za raisi John Magufuli kuisimamisha Tanzania kwenye ramani yake halisi barani Afrika na kwingineko.

Nimekuwa namuunga mkono raisi Magufuli katika michango mingi humu JF na kila mara nimekumbana na kasi kubwa ya mashambulizi kutoka kwa wanachama wenzangu ambao (kwa mtazamo) wao wanaona raisi John Magufuli anakosea kwenye baadhi ya mambo hususani uendeshaji wa idara ya usalama wa taifa ya TISS.

Ni juzi tu raisi Magufuli amemteua bwana Diwani Athumani kuwa mkurugenzi mkuu wa TISS uteuzi ambao si tu umenistua bali pia umeiacha na masuali mengi.

Masuali hayo pamoja na mengine ndo yamenisukuma kuandika haya maoni khasa kwenye eneo la uteuzi na kwamba kuna haja ya TISS kuundwa upya na pia uteuzi wa mkurugenzi mkuu kuwepo na nafasi ya Bunge letu tukufu kupitia sifa za mteule mpya wa TISS na kumthibitisha kabla ya kuapishwa rasmi na raisi.

Mimi pia ni mdau tu hivyo maoni haya yasichukuliwe kuwa ni kuingilia shughuli za idara hiyo bali ni kupeana ushauri na mapendekezo yanayolenga kuilinda nchi yetu katika masuala yote yanayohusu maslahi yake, uchumi wake na nyanja zingine muhimu.

Update: 12/04/2021

Raisi Magufuli RIP hatunae tena, alitangazwa kufariki tarehe 17 March 2021.

Sasa hivi tunae raisi Samia Suluhu Hassan ambae alikuwa ndie ataongoza serikali ya awamu ya tano kumalizia miaka minne ya mwisho ndani ya awamu mbil hadi 2025.

Twende kazi.

Mpaka sasa sheria ya usalama wa taifa ni ile ya mwaka 1996 ambayo inaelezea muundo wa TISS kama idara chini ya ofisi ya raisi.

Ushauri ni kwamba sheria inayounda TISS ipitiwe upya na ikiwezekana kuwe na sheria mpya kabisa ya kuundwa kwa idara hii na vitengo vingine ndani yake vitakavyokuwa na majukumu tofauti ya TISS.

Sheria hiyo mpya itakuwa inafafanua wazi kwamba TISS ipo kwa ajili ya maslahi ya taifa na usalama wake, uchumi wake na raia wake. na ipo kuzuia hujuma dhidi ya taifa letu, ugaidi, na vitendo voyote vinavyohatarisha usalama wa nchi na shughuli za kimaendelao na demoktasia kwa ujumla.

Hivyo basi, TISS haitaonekana kwamba ipo kwa ajili ya chama taala pekee bali ni kwa kila mtanzania.

Yaani: TISS ni Usalama wa taiifa chini ya mkurugenzi wake mkuu na mitandao yake yote nchi nzima.

Mkurugenzi wake mkuu ateuliwe na raisi lakini aidhinishwe na Bunge kwa sababu katika nchi zingine huyu bosi ana level moja na waziri yoyote yule yaani anakaa kwenye kikao cha BLM.

Akiidhinishwa Bunge anakuwa amepitia chujio.

Huyu DG anakuwa kama inavyojulikana anatoa PDB (taarifa za kila siku) kwa raisi kila usubuhi na hii PDB huwa inatoka kwenye idara zote nchi nzima na hata nje.

Hivyo, DG wa TISS aiongoza na kuielekeza TISS kwenye masuala na mpango mzima wa Usalama wa Taifa na pia ni mshauri wa raisi kama nilivyosema hapo juu kuhusu PDB.

Itaendelea, ntaongelea mapendekezo ya TISS mpya na vitengo vyake kikiwemo kitengo cha ujasusi wa nje ya Tanzania , maana suala la kuzuiwa ndege yetu ya ATCL kule Afrika Kusini limetutia aibu sana.

Pia ntaongelea tofauti yake na polisi lakini uwiano wake wa kazi na JWTZ.

Pia ntaongelea nini maana ya jumuiya ya wanausalama na umuhimu kwake kwa taifa la Tanzania linaloelekea kwenye hatua ya kila mwananchi kupata maziwa na asali.
 
Naendelea. Sehemu ya Pili.

Baada ya kupitia upya sheria ya usalama wa taifa.

Sheria itafanyiwa marekebisho na ufahamike wazi kwamba TISS ipo kwa ajili ya kulinda demokrasia ya bunge ikiwemo haki ya wabunge kupinga uteuzi wa mkurugenzi mkuu endapo itaonekana hana sifa.

Pia TISS inalinda maslahi ya taifa kiuchumi, kiutamaduni na kisiasa pamoja na kukabiliana na vitendo cha kigaisi, ujasusi wa kimataifa na uhujumu uchumi.

Mapendekezo ya Muundo mpya wa TISS na idara zake muhimu chini yake.

Kama nilivyosema hapo awali TISS ni Usalama wa taifa yaani National Security Organization/ Agency ambayo inaongozwa na mkurugenzi mkuu.

Naibu mkurgenzi yeye atashughulikia idara zingine khasa ya nje kwenye mabalozi, upelelezi wa ndani yaani domestic Surveillance na kuhudhuria vikao vya kamati za usalama zote za wilaya na mikoa.

Idara ya usalama wa ndai na usalama wa nje yaani "counter intelligence and counter espionage" zitakuwa na wakurugenzi wadogo ambao wanawajibika kwa naibu mkurugenzi mkuu.

TISS iwe inasimamiwa shughuli zake kwa ukaribu na kamati ya bunge la JMT ya Ulinzi na Usalama na iwe inaangaliwa kwa jicho kali kwenye bajeti yake, shughuli zake na hata utaratibu wake wa kuajiri watumishi wake.

Kwenye miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na tuhuma za TISS kuajiri vijana wa CCM na hivyo kuingilia shughuli zake ambazo msingi wake ni kulinda usalama wa taifa na maslahi yake popote pale iwe ndani au nje ya nchi.

Kwa kuwa kamati ya Bunge inajumuisha wabunge kutoka vyama vyote hapo tayari ushiriki wao kuikosoa TISS unakuwa umekamilika yaani "accomplished".

Itaendelea.
 
Kama vyombo mahsusi havitatekeleza kaa ukijua unampigia mbuzi gitaa.. hata bungeni nape alishawahi lalamika lkn Nini ni nini.. hili Jambo ni kubwa Sana Kama Kuna mkono wa mtu kwenye hio idara Basi jua kazi itakuwa kazi kubwa! Lkn Tena kunaweza kufanyika mchezo bandia wa kuvunja na kurudisha nguvu mpya ambayo si kwamba tu itatekeleza Yale ya zamani ila master mind yake itakuwa pana zaidi!!! Hivyo kelele zitakuwa zimeongeza ugumu wa tatizo!,hapa kunahitajika data ambayo si ya kiwango Cha kitoto. Na waliostafu kwenye hio idara wanafahamu matatizo yake na faida zake hapo inahitajika kamati zalendo yenye Siri na weledi mpana kabla ya kuvunjwa.
 
SEHEMU YA TATU.

Naendelea- uundwaji na mfumo wa Usalama Tanzania au TISS na chombo kamili kama taasisi au organization.


Lakini pia hii ni mashine au "Intelligence machine" ambayo inaundwa kuendesha shughuli zake nchi nzima na nje ya mipaka.

Hivyo basi, mashine yoyote ina vipuri kadha wa kadha ili iweze kuwa imara na itekeleze majukumu yake kikamilifu.

Hivyo mashine hii ya TISS yaunda TISS 7 Domestic ya ndani na TISS 8 Foreign ya nje, idara ya mawasiliano.idara ya usalama JWTZ, jumuiya ya makachero au intelligence community, baraza la usalama na kamati maalum ya usalama.

Hivyo basi muundo wake taasisi hii na idara zake nikama ifuatavyo:

1.Usalama wa taifa na inaongozwa na Mkurugenzi mkuu na naibu mkurugenzi mkuu.


2. Idara ya intelligentsia ya ndani au "TISS 7 domestic" na mkurugenzi wake

3. Idara ya intelligentsia ya nje "TISS 8 Foreign" na mkurugenzi wake.

Wakurugenzi wa TISS 7 na TISS 8 Foreign wanawajibika kwa mKurugenzi mkuu wa Usalama wa Taifa yaani Tanzania National Security Agency.


TISS na idara na hivyo vitengo vingine vinakuwa vinasimamiwa kwa pamoja na sheria mpya ya usalama wa taifa ya mwaka 2020 (ikiwa sheria inaafikiwa ijadiliwe, na ipitishwe)

Naomba nifafanue hapa, kwamba TISS haihusiani na wala haiwezi kuchanganywa na jeshi la polisi isipokuwa katika utekelezaji wa majukumu yao kama taasisi tofauti.

Kwa mfano TISS inazibua shughuli na mipango ya kigaidi basi kunakuwa na opereshini maalum inayoitwa joint operation ya kumalizana na hao watuhumiwa ila ni polisi ndo wanaoshughulika kwa mwongozo wa TISS.

Hivyo basi, polisi wana chuo chao cha Poilisi CCP Moshi na TISS wana vyuo vyao tofauti.

Ukitaka kuwa ofisa wa TISS kutoka polisi inabidi uanze upya maombi na ufanyiwe usaili na mitihani

Yaani hapa uteuzi, ajira na upandishaji vyeo unatakiwa uwe tofauti na usiingiliane na hata kama mtu ana sifa mbalimbali bado anatakiwa kupita kwenye chujio maalum.

Kwa mfano vyombo vingine vya nchi za mbali huwa wanawanyia maofisa watarajiwa mitihani unaojulikana kama polygraph ambapo ofisi mtarajiwa anapimwa uaminifu kulingana na masuali anayojibu.

Mfumo unaopendekezwa wa TISS - Idara za ndani kabisa.

Hapa tunaondoa idara ya PSU ambayo inajitegemea.

Idara za ndani

Idara ya Uchambuzi, Idaya ya ubunifu na utafiti, idara ya operesheni, idara ya usaidizi na ugavi na idara ya sayansi na teknolojia.

Idara zote hizi ziongozwe na watu walosoma masuala hayo na wawe wanaisaidia TISS kuchambua taarifa ambazo zingine ni dhahiri tunaweza kuzishughulikia kwa uharaka na umakini mkubwa.

Kwa kuwa nchi yetu ni kubwa basi kilamkoa unapata fursa ya kuwa na maofisa ambao wanafanya shughuli zao kutoka kwenye wilaya na mikoa yote chini ya mwamvuli wa mama yso TISS.

Kwa mfano idara ya sayansi na teknolojia inaweza kuwa inajishughulisha na kuandaa vijana mbalimbali wenye vipaji khasa wale wa kutoka kwenye shule maalum na kuwaandaa kupitia chuo kikuu au vyuo vya TISS.

Idara ya ubunifu na utafiti.

Idara hii ni moja ya idara maalumu kabisa na kazi yake ya msingi ni kuijenga taswira ya TISS kitaifa na kimataifa kulingana na mahitaji.

Idara hii itashughulika na masuala ya mitandao, kampeni mbalimbali kwenye vyombo vya habari, kuelimisha jamii, kupambana na propaganda za mitandanoni na kujibu mapigo pale serikali au taasisi zake zinaposhambuliwa ama mitandaoni kwenye magazeti au hata nyombo vya habari vya nje.

Ikitumia mtindo uitwao "friendly approach", idara hii itaandaa semina mbalimbali kwa ajili ya kufanya brain storming kwa maofisa watarajiwa na hata kutoa taarifa za kiinteligensia kwa vyombo vingine vya ulinzi na usalama.

Idara hii pia itajihusisha na kutengeneza historia na kumbukumbu ya TISS kwa ajili ya vizazi vijavyo jambo litakalosaidia kuelimisha zaidi maofisa wapya.

Hivyo kutakuwa na jumba la makumbusho la TISS na maktaba kabisa ambapo maofisa wataweza kusoma historia kama ile ya vita vya Kagera na matukio mengine muhimu.

Watu wa idara hii wanatarajiwa kuwa ni wasomi wa shahada za kwanza na za pili kwenye masuala mbalimbali kama habari, teknolojia, usalama wa habari na mahusiano ya umma.

Ikumbukwe kwamba hiki chombo si adui wa wananchi au wanasiasa wa pande zozote zile bali ni kama kiunganishi kwa wananchi hao ambao wakikielewa wanaweza kuwa msaada mkubwa kwa kutoa taarifa zinazohusiana na kutishia usalama wa nchi.


itaendelea..
 
TISS za wenzetu zipo kwa ajili ya vita kuu mbili yaani UCHUMI NA USALAMA WA NCHI TISS yetu iachane na kuwa biased kwa kufuata maelekezo ya kulinda chama tawala.Waachane na mambo ya kubana praizi wakosoaji wa serikali na badala yake wajipange kubuni mikakati ya kuisaidia nchi na utawala kupunguza wimbi la umasikini ambalo linazalisha wakosoaji na waponda serikali wengi.
 
Sasa ateuliwe na raisi ila athibitishwe na bunge( bunge butu) watu wote wanasema ndioooo hakuna mawazo mbadala unategemea itakua na tija gani? Mara mia ungesema hio post ua uDG iombwe kama nafasi zingine mwenye sifa aongoze kwa weledi
 
Katika miezi ya hivi karibuni kumekuwepo na mijadala mbalimbali inayohusu idara ya usalama Tanzania ijulikanayo kama TISS.
Mijadala hiyo imeelekezwa zaidi kwenye kuishutumu idara hiyo kwa kujishughulisha zaidi ya ukandamizaji wa haki za binadamu na kuwadhibiti wapinzani wa serikali inayoongozwa na chama tawala cha CCM.
Mimi, binafsi lazima niseme ukweli, nimependezwa sana na kasi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali na sekta mbalimbali nchini mwetu.
Pia nimependezwa na juhudi za raisi John Magufuli kuisimamisha Tanzania kwenye ramani yake halisi barani Afrika na kwingineko.
Nimekuwa namuunga mkono raisi Magufuli katika michango mingi humu JF na kila mara nimekumbana na kasi kubwa ya mashambulizi kutoka kwa wanachama wenzangu ambao (kwa mtazamo) wao wanaona raisi John Magufuli anakosea kwenye baadhi ya mambo hususani uendeshaji wa idara ya usalama wa taifa ya TISS.
Ni juzi tu raisi Magufuli amemteua bwana Diwani Athumani kuwa mkurugenzi mkuu wa TISS uteuzi ambao si tu umenistua bali pia umeiacha na masuali mengi.
Masuali hayo pamoja na mengine ndo yamenisukuma kuandika haya maoni khasa kwenye eneo la uteuzi na kwamba kuna haja ya TISS kuundwa upya na pia uteuzi wa mkurugenzi mkuu kuwepo na nafasi ya Bunge letu tukufu kupitia sifa za mteule mpya wa TISS na kumthibitisha kabla ya kuapishwa rasmi na raisi.
Mimi pia ni mdau tu hivyo maoni haya yasichukuliwe kuwa ni kuingilia shughuli za idara hiyo bali ni kupeana ushauri na mapendekezo yanayolenga kuilinda nchi yetu katika masuala yote yanayohusu maslahi yake, uchumi wake na nyanja zingine muhimu.
Twende kazi.
Mpaka sasa sheria ya usalama wa taifa ni ile ya mwaka 1996 ambayo inaelezea muundo wa TISS kama idara chini ya ofisi ya raisi.
Ushauri ni kwamba sheria inayounda TISS ipitiwe upya na ikiwezekana kuwe na sheria mpya kabisa ya kuundwa kwa idara hii na vitengo vingine ndani yake vitakavyokuwa na majukumu tofauti ya TISS.
Yaani: TISS ni Usalama wa taiifa chini ya mkurugenzi wake mkuu na mitandao yake yote nchi nzima.
Mkurugenzi wake mkuu ateuliwe na raisi lakini aidhinishwe na Bunge kwa sababu katika nchi zingine huyu bosi ana level moja na waziri yoyote yule yaani anakaa kwenye kikao cha BLM.
Akiidhinishwa Bunge anakuwa amepitia chujio.
Huyu DG anakuwa kama inavyojulikana anatoa PDB (taarifa za kila siku) kwa raisi kila usubuhi na hii PDB huwa inatoka kwenye idara zote nchi nzima na hata nje.
Hivyo DG wa TISS anaiongoza na kuielekeza TISS kwenye masuala na mpango mzima wa Usalama wa Taifa na pia ni mshauri wa raisi kama nilivyosema hapo juu kuhusu PDB.
Itaendelea, ntaongelea mapendekezo ya TISS mpya na vitengo vyake kikiwemo kitengo cha ujasusi wa nje ya Tanzania , maana suala la kuzuiwa ndege yetu ya ATCL kule Afrika Kusini limetutia aibu sana.
Pia ntaongelea tofauti yake na polisi lakini uwiano wake wa kazi na JWTZ.
Pia ntaongelea nini maana ya jumuiya ya wanausalama na umuhimu kwake kwa taifa la Tanzania linaloelekea kwenye hatua ya kila mwananchi kupata maziwa na asali.




mkuu nimekuelewa hata Mimi kama mdau Nina dukuduku kama LA kwako moyoni Juu ya Swala hili LA National Security asante
 
Sasa ateuliwe na raisi ila athibitishwe na bunge( bunge butu) watu wote wanasema ndioooo hakuna mawazo mbadala unategemea itakua na tija gani? Mara mia ungesema hio post ua uDG iombwe kama nafasi zingine mwenye sifa aongoze kwa weledi

Hiyo yaitwa "Scrutiny", ni muhimu kwenye kumchagua DG anaefaa na Bungeni ni mahali sahihi.

Lakini ili kuwepo na haki ya kuhoji uteuzi bungeni hiyo ni fursa tosha kwa wabunge wanaowakilisha wananchi kutumia haki yao kikatiba kutekeleza jukumu hilo la kidemokrasia.
 
Hiyo yaitwa "Scrutiny", ni muhimu kwenye kumchagua DG anaefaa na Bungeni ni mahali sahihi.

Lakini ili kuwepo na haki ya kuhoji uteuzi bungeni hiyo ni fursa tosha kwa wabunge wanaowakilisha wananchi kutumia haki yao kikatiba kutekeleza jukumu hilo la kidemokrasia.
Whats the impact & effect of such scrutiny?
 
Whats the impact & effect of such scrutiny?

If new DG is disapproved then the president is given opportunity to appoint another person.

The process ( the scrutiny) can go on and on until the suitable person is found.
 
If new DG is disapproved then the president is given opportunity to appoint another person.

The process ( the scrutiny) can go on and on until the suitable person is found.
Do you think Tanzania has parlimentary supremacy or presidential (executive supremacy)?
Tanzanias parliament is the Governments Rubber stamp..dont get it twisted
 
SEHEMU YA NNE.

Ajira ndani ya TISS


Kwa mujibu wa sheria ya Usalama wa taifa ya mwaka 1996 sehemu ya 7 kifungu 1-4 hakuna sehemu Inasemwa ni maofisa wenye sifa zipi ndo wanaaajiriwa.

Hivyo hali hii inatoa mwanya kuajiriwa kwa watu ambao pengine hawana sifa za kuwa maofisa wa TISS na hata wakati mwingine kuwepo kwa tuhuma za ajira kutolewa kwa misingi ya ukabila au undugu na urafiki.

Pia sheria hii inatoa mwanya kwa mkurugenzi wake pia kuweza kuidhinisha ajira mbalimbali ndani ya taasisi jambo ambalo linaweza kuepukwa ikiwa mkurugenzi mkuu nae anawajibika endapo ameajiri watu wasofaa.

Hivyo basi napendekeza kitengo cha rasilimali watu kuwa na maofisa maalum kabisa ambao watashughulikia suala la ajira za maofisa wapya kuanzia kwenye ile Polygraph nilioisema huko juu, hadi kwenye ngazi za mashuleni ambapo vijana wadogo wanaangaliwa kama wanafaa kuanza kujiunga taratibu kwenye taasisi hii.

Pia ikumbukwe kwamba taasisi hii ni ya watanzania wote ni iwe ni marufuku kwa mtu asie mtanzania kujaribu kufanya maobi ya kujiunga na taasisi hii.

Utaratibu wa kupata maofisa katika nchi za wenzetu walopiga hatua ni mgumu sana ambapo mbinu mbalimbali hutumika kuwapata vjana ikiwemo mbinu ya kuceza kwenye michezo ya computer kama zie za Xbox 1 na Play Station khasa PS4.

Mbinu zingine ni pamoja na kuanda mashindano ya hesabu ambapo vijana mahili wa hesabu wanakuwa wakisjindanai kupata wale maalum ambapo watafanya kazi inayohusiana na "coding" khasa kwa ujasusi wa kimataifa ambapo mbinu za kutumia alama na herufi huwa zatumika sana.

Nini maana ya Polygraph au polografia au lie detector.

Hiki ni kifaa maalum kinachotoa matokeo ya majibu ya mapigo ya moyo, mgandamizo wa damu au msisimko wa ngozi ya mwili na kupitia michoro kwenye karatasi maalum.

Hivyo mkanda wa kifaa hiki hufungwa katika mkono wa mtahiniwa na jibu lolote analotoa huendana na hali yae ya kisaikolojia ya wakti huo

Hivyo kama unadanganya basi majibu hayatakuwa yakilingana hivyo kushindwa mtihani.


TISS kuwa na chuo maalum.

TISS kuwa na chuo maalum ambacho kitafundisha masuala mbalimbali lwa maofisa wake ni jambo muhimu.

Kwa mfano, nchini Marekani mwaka 2002 aliekuwa mkurugenzi mkuu bwana George Tenet alianzisha chuo kikuu cha CIA ambacho kila mwaka kinatoa kozi mbalimbali kati ya 200 na 300.

Hivyo chuoni hapo wale maofisa wapya, wale wazoefu na waajiriwa wengine wa kawaida wanakuwa wakipigwa msasa kwenye maeneo ya teknolojia, ubunifu, demokrasia, siasa zisizofungamana na upande wowote na hata kuheshimu sheria na miiko ya kazi zao.

Hivyo pamoja na kwamba TISS wanaweza kuwa na chuo chao lakini bado kuna haja ya kukiboresha chou hicho ili kulikngana na hali halisi.

Masuala kama ujasusi wa kiteknolojia na mawasiliano. yameshika kasi sana hivyo ni muhimu taasisi hii ikawa haiachiwi nyuma kwenye maeneo hayo.

Miaka mitatu ilopita iliwahi kuandika kuhusu ujasusi wa kiteknolojia na kiuchumi na madhara yake endapo Tanzania haitakuw tayari kupitia hapa :



Itaendelea.
 
Mkuu unatoa madini ya muhimu sana ila ukweli mchungu ni kuwa viongozi wetu hawana nia ya dhati kututoa hapa tulipo.

Kama inshu ya muhimu kupata katiba mpya ilishindikana, amini nakuambia hakuna kitu cha maana tutakachokiweza.
Tumejaa ubinafsi uliopitiliza.
 
Katika miezi ya hivi karibuni kumekuwepo na mijadala mbalimbali inayohusu idara ya usalama Tanzania ijulikanayo kama TISS.

Mijadala hiyo imeelekezwa zaidi kwenye kuishutumu idara hiyo kwa kujishughulisha zaidi ya ukandamizaji wa haki za binadamu na kuwadhibiti wapinzani wa serikali inayoongozwa na chama tawala cha CCM.

Mimi, binafsi lazima niseme ukweli, nimependezwa sana na kasi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali na sekta mbalimbali nchini mwetu.

Pia nimependezwa na juhudi za raisi John Magufuli kuisimamisha Tanzania kwenye ramani yake halisi barani Afrika na kwingineko.

Nimekuwa namuunga mkono raisi Magufuli katika michango mingi humu JF na kila mara nimekumbana na kasi kubwa ya mashambulizi kutoka kwa wanachama wenzangu ambao (kwa mtazamo) wao wanaona raisi John Magufuli anakosea kwenye baadhi ya mambo hususani uendeshaji wa idara ya usalama wa taifa ya TISS.

Ni juzi tu raisi Magufuli amemteua bwana Diwani Athumani kuwa mkurugenzi mkuu wa TISS uteuzi ambao si tu umenistua bali pia umeiacha na masuali mengi.

Masuali hayo pamoja na mengine ndo yamenisukuma kuandika haya maoni khasa kwenye eneo la uteuzi na kwamba kuna haja ya TISS kuundwa upya na pia uteuzi wa mkurugenzi mkuu kuwepo na nafasi ya Bunge letu tukufu kupitia sifa za mteule mpya wa TISS na kumthibitisha kabla ya kuapishwa rasmi na raisi.

Mimi pia ni mdau tu hivyo maoni haya yasichukuliwe kuwa ni kuingilia shughuli za idara hiyo bali ni kupeana ushauri na mapendekezo yanayolenga kuilinda nchi yetu katika masuala yote yanayohusu maslahi yake, uchumi wake na nyanja zingine muhimu.

Twende kazi.

Mpaka sasa sheria ya usalama wa taifa ni ile ya mwaka 1996 ambayo inaelezea muundo wa TISS kama idara chini ya ofisi ya raisi.

Ushauri ni kwamba sheria inayounda TISS ipitiwe upya na ikiwezekana kuwe na sheria mpya kabisa ya kuundwa kwa idara hii na vitengo vingine ndani yake vitakavyokuwa na majukumu tofauti ya TISS.

Sheria hiyo mpya itakuwa inafafanua wazi kwamba TISS ipo kwa ajili ya maslahi ya taifa na usalama wake, uchumi wake na raia wake. na ipo kuzuia hujuma dhidi ya taifa letu, ugaidi, na vitendo voyote vinavyohatarisha usalama wa nchi na shughuli za kimaendelao na demoktasia kwa ujumla.

Hivyo basi, TISS haitaonekana kwamba ipo kwa ajili ya chama taala pekee bali ni kwa kila mtanzania.

Yaani: TISS ni Usalama wa taiifa chini ya mkurugenzi wake mkuu na mitandao yake yote nchi nzima.

Mkurugenzi wake mkuu ateuliwe na raisi lakini aidhinishwe na Bunge kwa sababu katika nchi zingine huyu bosi ana level moja na waziri yoyote yule yaani anakaa kwenye kikao cha BLM.

Akiidhinishwa Bunge anakuwa amepitia chujio.

Huyu DG anakuwa kama inavyojulikana anatoa PDB (taarifa za kila siku) kwa raisi kila usubuhi na hii PDB huwa inatoka kwenye idara zote nchi nzima na hata nje.

Hivyo DG wa TISS anaiongoza na kuielekeza TISS kwenye masuala na mpango mzima wa Usalama wa Taifa na pia ni mshauri wa raisi kama nilivyosema hapo juu kuhusu PDB.

Itaendelea, ntaongelea mapendekezo ya TISS mpya na vitengo vyake kikiwemo kitengo cha ujasusi wa nje ya Tanzania , maana suala la kuzuiwa ndege yetu ya ATCL kule Afrika Kusini limetutia aibu sana.

Pia ntaongelea tofauti yake na polisi lakini uwiano wake wa kazi na JWTZ.

Pia ntaongelea nini maana ya jumuiya ya wanausalama na umuhimu kwake kwa taifa la Tanzania linaloelekea kwenye hatua ya kila mwananchi kupata maziwa na asali.
TISS au TIS?
 
Binafsi mimi naona kosa la kimsingi pale tunapoita vyama vya upinzani badala ya chama mbadala, na nchi inapoongozwa kwa kutumia ilani ya chama badala ya kuwa na ilani ya nchi . na ilani ya chama ikatumika kuharakisha utekelezaji wa ilani ya nchi. Kutofautiana mawazo , itikadi na imani sio uadui. Kama kweli tuliridhia mfumo wa vyama vingi kwa hiari yetu bila shuruti basi tu jengo taifa moja bila ubaguzi wa kiitikadi.
 
Wachukulie kwamba ni watu wa kila rika na tofautitofauti.
 
SEHEMU YA TANO

Wanajumuiya ya inteligensia ni nani hawa?


Wanajumuiya ya inteligensia ni kundi la walio ndani ya TISS na idara zingine na wale walowahi kuwa watumishi. maofisa na viongozi mbalimbali wa TISS.

Watu hawa huunda baraza la usalama na baraza la ushauri kwa serikali, kamati za ulinzi na usalama za wilaya na mikoa na wakuu wa TISS.

Kundi hili hufanya shughuli zake kwa pamoja na kwa kushirikiana na maofisa waliko kwenye vituo mbalimbali ndani na nje ya nchi na kisha kutoa taarifa zao kupitia ofisi yao ambayo ipo chini ya mkurugenzi mkuu wa TISS.

Kwa kuwa taarifa za wanajumuiya zina thamani ya kipekee, zinaweza kumfikia raisi moja kwa moja na hapo kwa kuzingatia kwamba wale walioko nje wana uwezo wa kuwasiliana na mkurugenzi mkuu moja kwa moja.

Kwa mfano, suala la kuzuiwa kwa ndege ya ATCL nchini Afrika Kusini ambalo liliamsha mjadala mitandaoni na kwenye vikao kadha wa kadha, lingeweza kabisa kuepushwa endapo kungekuwa na mawasiliano bora baina ya wanajumuiya waliopo Afrika Kusini na Tanzania.

Madhara ya kuzuiwa kwa ndege hiyo ni pamoja na kukoseshwa mapato ambayo yangetokana na mauzo ya tiketi za ndege hiyo, kushushwa thamani ya usafiri huo wa ndege ya ATCL kwenda Afrika Kusini na pia kukosa kuwemo kwenye soko kwa muda kunakotokana na kusimamishwa kwa safari za ndege hiyo kwenda nchini humo.

Naamini TISS ni imara kama nilivyowahi kusema hapa:

https://www.jamiiforums.com/threads...kitine-waasisi-wa-tiss-imara-tanzania.966599/

Pia wanajumuiya wanatoka katika makundi ya wanafunzi, walimu, na raia wengine wenye sifa mbalimbali ambao wana uwezo wa kusaidia mawazo endapo msaada wo utahitajika.

Kwenye baadhi ya maeneo lakini kuna sehemu kama za Operesheni ambazo bado zinahitaji sheria kuangaliwa upya.

Kuna tuhuma kwa TISS kutumia watu wasojulikana ambao umezua imani kwamba hii taasisi inahusika kabisa.

Lakini endapo sheria itarekebishwa basi kutakuwepo na nidhamu katika utakelezaji wa shughuli zake na ambazo ni lazima ziwe ndani ya sheria.

Pia zipo tuhuma za kutumiwa watu kama Musiba ambae hujiita mwanaharakati huru ambae amekuwa kila mara akitoa shutuma nzito dhidi ya watu ambao walikuwa ni viongozi katika nchi hii.

Sheria hiyo mpya itazuia watu wa aina hii au itawataka kutoa ushahidi wa yale wanayoyaongelea hadharani au kutumia vyombo vyao vya habari.

Ntaendelea kesho katika sehemu ya mwisho ambayo itahusu ofisi ya naibu mkurugenzi, uhusiano wa TISS na JWTZ na ujasusi wa nje ya Tanzania kwa manufaa ya kila mtanzania ambapo uhakika wa maziwa na asali unakuwa ni jambo la kawaida.
 
Back
Top Bottom