toka vianze vyama vingi vya siasa, kumekuwa na uhasama mkubwa kati ya ccm na cuf kwa upande wa znz. Kwa mtazamo wa wengi, uhasama huu umesaidia kwa upande wa bara kwa sababu wa znz badala ya kudai haki zao za msingi kutoka bara wamekuwa wakigombana wenyewe kwa wenyewe. Wakati mwalimu nyerere yuko hai, wa znz walikuwa wakimuogopa sana, lakini toka amefariki na hofu yao imeondoka. Nimesafiri nchi nyingi sana, watu wengi kutoka europe, asia na america hawaijui tanzania, lakini wanaijuwa znz kutokana na historia yake. Watalii wengi wanakuja tanzania kutokana na umaarufu wa znz duniani. Neema kubwa tunayopata tanzania inatokana na kuweko kwa huu muungano. Hofu kubwa inayojitokeza ni kuwa endapo cuf na ccm wataelewana huenda ikapelekea wakadai haki zao nyingi ambazo upande wa bara wamekuwa wakiziminya, na hii inaweza pia ikaleta mvutano ambao ukasababisha kuvunjika kwa muungano!.. Wana jf mawazo yenu yanakaribishwa