Maono yangu juu ya Tanzania ijayo

Maono yangu juu ya Tanzania ijayo

usisahau kuwa mahakama ni blood stream ya ccm

Hauwezi kukata tamaa wakati haujajaribu.Siyo wakati wote mahakama inaegemea kwa CCM,angalia kesi za Mtikila zimeifanya Serikali iamue mambo mengine kwa sababu ya kesi hizi.Unajua ni mwiko kusema "I wish" bali tunatakiwa kusema "I will" mara zote.Hata ukianguka basi Serikali yetu sikivu ujumbe utakuwa umeifikia.lakini tukiendelea kunyamaza na kufikiri kwa kunyamaza kwetu ndiyo tutashinda basi imekula kwetu.

Vyama vya siasa vyote havitakiwi kutegeana,vishirikiane na kwenda hatua moja mbele.
 
kuliko tuwape nchi wachaga bora ccm itawale milele
Siku zote wapumbavu ndiyo wanaoweza kutoa comments za aina hii. Mimi ni ccm damudamu lakini ujinga wa aina hii ni wa kulaaniwa kwa nguvu zote na wapenda amani wote Tz.
 
Mkuu naomba nikupunguzie ujiko. Ulichosema si maono ni FACT (labda kama unataka kuwafikia wanaoishi kwa mitizamo ya imani za kidini zaidi). Mtu yeyote mwenye uelewa wa kutosha wa mazingira ya kisiasa ya TZ au mwenye uwezo wa kusoma mazingira ya kisiasa popote pale atakiona unachokisema. Dhana muhimu ya siasa na vyama vya siasa ambayo Watanzania wengi hawajaipata ni kule kufikiri kuwa uhakika wa maisha mazuri/bora na yanayokubalika utaletwa na chama fulani cha siasa au mwanasiasa fulani kuwepo na/au kudumu madarakani. BIG MISTAKE. Hata Nyerere alichokwa.

Mantiki (logic) ya kawaida kabisa inatuthibitishia kuwa ukimhakikishia binadamu nafasi ya kudumu na maslahi ya kudumu mahali pazuri madarakani bila kujali utendaji wake au "madhambi" yake, basi kaa tayari hata kukanyagwa kichwani. Hakuna kosa kubwa kama kutoa guarantee kwa chama, watu au vikundi vya watu kudumu madarakani bila masharti na tishio halisi la kung'olewa wakivurunda. Ndilo kosa tulilofanya Watanzania kuihakikishia CCM "urojo" wa milele; nao bila hiyana wakajimilikisha kikamilifu zana za dola kwa "matumizi binafsi".

Aidha, sikubaliani na wanaoona kuwa CCM ndio tatizo; wala siendani na hoja ya kufikiri kuwa CCM ni chama kibaya - eti cha kishetani! (sera na makabrasha yake hayatuelekezi huko - yanatuhakikishia pepo!). Na chama ni sera; ni imani; ni mikakati iliyoainishwa kwenye maandishi yake. Ni jukumu letu wananchi kupima na kuhukumu utekelezaji. Tatizo ni binadamu tulioamua kuwapa "gerentii" ya kukihujumu chama na kukitumia kama nyenzo ya kuhujumu nchi na watu wake. Ni sisi ndio tumeshindwa kazi ya kuiwajibisha CCM na kuiweka kwenye mstari sahihi au pembeni isituletee ujinga.

Ni kwa sababu hiyo, ningependa kuona chama kikingine kikiingia madarakani LAKINI (sisi wananchi) tukiwa na mtazamo sahihi usio na ushabiki wa kijinga na wenye kutoa tahadhari chama chochote au mtu yeyote kuwa "ukituletea ujinga hata robo tu, tunakupiga kibuti sawia!" Na kwa hapo, niko tayari kuona serikali ikibadilika mara kwa mara hata kwa mtindo wa Italia ili wababaishaji wote wajue Watanzania si wa kuchezewa.

Kwa hali inavyoendelea sasa na kwa akili ya Watanzania wengi, nakubali CCM itaendelea kula urojo hadi pale maumivu yatakapofikia kiwango sahihi cha kuamsha "TZ spring". Na kibaya zaidi kama ulivyosema, hivi leo CCM si nyenzo ya mafisadi wa ndani tu; bali ni zana muhimu sana kwa mabeberu waliokamia rasilimali zetu. Hapo pana kazi.
 
nilipokuta tu hii sentesi kwenye post yako nikakupuuza kwasababu nimekuona wewe ni wa hovyo kabisa '''''bado hazitatosha maana vyama vingine ukiacha CHADEMA ni kama havipo.''''
CCM haitaachia madaraka kwa sanduku la kura. Hii haitatokea. Wapinzani wakiunganisha nguvu, bado hazitatosha maana vyama vingine ukiacha CHADEMA ni kama havipo.

Uchaguzi ujao CCM itashinda kwa kuwa wana mbinu za kufanya hivyo. Si kwa ilani wala kwa sera bali kwa ghiliba.

Kwa kuwa Dola ni damu ya chama tawala, tusitegemee chama tawala kukubali kuvuja damu.

Hali ikiendelea hivi ni kwamba upinzani utapungua nguvu na wananchi watakosa imani na siasa za nchi hii kwa ujumla. CHADEMA iepukane na kundi la vijana ambao hawajitambui maana wengi si wapiga kura.

Kwa CCM kutoka madarakani ni nguvu toka nje ya Tanzania itatumika. Hadi sasa haiwezekani kufanyika hivyo kwa kuwa ccm wanakula vizuri na mabeberu rasilimali zetu.

CCM itatoka madarakani kwa mapinduzi. Na mambo yasipoenda vyema tutageuka sierra leone nyingine. Hakutatokea chama cha upinzani kitakachokuja kuwa na nguvu kama CHADEMA.

Mwisho, kama hayo hapo juu hayatatokea, na kama tunahitaji mbadala wa CCM, basi tuanze kuiamini kauli ya Nyerere. Tusubiri CCM imeguke. Hili halishindikani. Yangu macho
 
CCM haitaachia madaraka kwa sanduku la kura. Hii haitatokea. Wapinzani wakiunganisha nguvu, bado hazitatosha maana vyama vingine ukiacha CHADEMA ni kama havipo.

Uchaguzi ujao CCM itashinda kwa kuwa wana mbinu za kufanya hivyo. Si kwa ilani wala kwa sera bali kwa ghiliba.

Kwa kuwa Dola ni damu ya chama tawala, tusitegemee chama tawala kukubali kuvuja damu.

Hali ikiendelea hivi ni kwamba upinzani utapungua nguvu na wananchi watakosa imani na siasa za nchi hii kwa ujumla. CHADEMA iepukane na kundi la vijana ambao hawajitambui maana wengi si wapiga kura.

Kwa CCM kutoka madarakani ni nguvu toka nje ya Tanzania itatumika. Hadi sasa haiwezekani kufanyika hivyo kwa kuwa ccm wanakula vizuri na mabeberu rasilimali zetu.

CCM itatoka madarakani kwa mapinduzi. Na mambo yasipoenda vyema tutageuka sierra leone nyingine. Hakutatokea chama cha upinzani kitakachokuja kuwa na nguvu kama CHADEMA.

Mwisho, kama hayo hapo juu hayatatokea, na kama tunahitaji mbadala wa CCM, basi tuanze kuiamini kauli ya Nyerere. Tusubiri CCM imeguke. Hili halishindikani. Yangu macho

Mkuu wewe umefanya kosa la kufikiri kama viongozi wa CCM na wapambe wao! ie Ukitaka kutawala kwa ulaini kabisa bila bughula, ufanye utakavyo, basi ua vyama vya upinzani na hasa Chadema! Imefikia mahali CCM imefadhili hata uundwaji wa chama fake cha upinzani eti ili kipambane na Chadema.... lakini hebu tujiulize...kina Gadafi (Libya), Nicolae Ceaușescu (Romania) etc waliondolewa na chama gani cha upinzani? Au utakuja tena na jibu ambalo hata CCM wanajifariji nalo kila siku... ''watanzania ni wapole kazi kulalamika tu, hawawezi kufanya kitu''... Lakini mimi nakuambia chunga sana sana watu wa aina ya watanzania....nani alikuwa anajua kuwa Mtwara siku moja itachafuka mpaka jeshi litumike? Nani alikuwa najua Mabina kuna siku atauawa kwa mawe kama kibaka na wapiga kura wake?
 
1. Hivi watu waliojiandikisha 2010, walikuwa ni CCM! na kama ndio kwa nini?

2. Kuna hoja kwamba vijana ndio wanaounga mkono upinzani lakini hawako kwenye daftari la kudumu.Sasa;

(a) Ina maana watu waliokuwa na miaka 18, mwaka 2010, leo 2014 washakuwa wazee? au tunaposema vijana tunakusudia nini?

(b) je! tuna data ya idadi ya vijana wanaounga mkono upinzani na tukajua wingi wao au tuna kisia?

(c) Ni kitu gani kinachofanya vijana wenye umri wa miaka chini ya 22, ndio wawe waungaji mkono wa upinzani, na wenye umri zaidi ya hapo waunge mkono CCM?na kwa nini upinzani haufikirii kuwabadili hao wenye umri wa kuanzia miaka 22 ili wawaunge mkono?

(D)Hivi ni kweli kwamba hakuna vijana wanaounga mkono CCM? Kama wapo, tunajua ni wangapi? Kuangalia wanajitokeza kwenye mkutano si hoja maana si kila mtu anaenda kwenye mikutano.Nakumbuka hata watu walikuwa wanapima kukubalika kwa zitto kwa kuangalia wanaohudhuria mahakamani kumuunga mkono, lakini hoja ikatolewa simple tu kwamba wanaomuunga mkono wengi ni proffesionals, kwa hiyo kati kati ya wiki wako ofisini!.

(E) Hivi ni kweli kwamba vizazi vinavyochipukia wote ni wapinzani?, hivyo wakiandikishwa itakuwa walioandikishwa wapinzani? kama ndio hivyo, ina maana watu kama akina Paul Makonda wanalea chipkizi ambao si CCM?

(F) je! hao watu zaidi ya nusu ambao wamajiandikisha kwenye daftari lakini hawana tabia ya kupiga kura ni akina nani na kwa nini? je! hatuoni hata baada ya kuboresha bado watajiandikisha tu na kura hawapigi ng'o! hivi ni kweli hatujui kwa nini hawapigi?

Kama daftari la wapiga kura likiwa la kidemokrasia, likaruhusu vijana wote wenye umri wa miaka 18 na kuendelea kujiandikisha, CDM watashinda. CCM wataiba lakini hawataweza kuiba vya kutosha.

Hatuwezi kutawaliwa daima na wezi na wanyang'anyi. Vijana ni nguvu ya CHADEMA. Kwa sasa hawapigi kura kwani hawaruhusiwi kujiandikisha. This ought to be challenged in court
 
unazungumzia vijana wa moshi na arusha au vijana wa wapi? hakuna kijana anaejitambua atakaepigia kura chadema

Hivi sisi watanzania ni nani ameturoga. Pamoja na shida zote hizi ambazo serekali hii imeshindwa kuzitatua bado kuna watu wanaona ni afadhali kuendelea na shida kuliko kutafuta mbadala.
 
Mkuu wewe umefanya kosa la kufikiri kama viongozi wa CCM na wapambe wao! ie Ukitaka kutawala kwa ulaini kabisa bila bughula, ufanye utakavyo, basi ua vyama vya upinzani na hasa Chadema! Imefikia mahali CCM imefadhili hata uundwaji wa chama fake cha upinzani eti ili kipambane na Chadema.... lakini hebu tujiulize...kina Gadafi (Libya), Nicolae Ceaușescu (Romania) etc waliondolewa na chama gani cha upinzani? Au utakuja tena na jibu ambalo hata CCM wanajifariji nalo kila siku... ''watanzania ni wapole kazi kulalamika tu, hawawezi kufanya kitu''... Lakini mimi nakuambia chunga sana sana watu wa aina ya watanzania....nani alikuwa anajua kuwa Mtwara siku moja itachafuka mpaka jeshi litumike? Nani alikuwa najua Mabina kuna siku atauawa kwa mawe kama kibaka na wapiga kura wake?

Sina hakika kama umesoma bandiko langu. Nimeitaja Sierra Leone huko juu. Hii nchi ilikuwa tulivu zaidi ya Tanzania. Lakini siku isiyo na jina ilitokea vita kubwa sana ikiongozwa na uasi wa Fodey Sanko. Ndio maana nikasema tusije tukafika huko. Najua Tanzania hii kuna mabomu mengi mabomu mengi sana ambayo yanahitaji wataalamu kuyategua, la sivyo hayo ya kina Mabina na Mtwara ni tone tu.
 
CCM haitaachia madaraka kwa sanduku la kura. Hii haitatokea. Wapinzani wakiunganisha nguvu, bado hazitatosha maana vyama vingine ukiacha CHADEMA ni kama havipo.

Uchaguzi ujao CCM itashinda kwa kuwa wana mbinu za kufanya hivyo. Si kwa ilani wala kwa sera bali kwa ghiliba.

Kwa kuwa Dola ni damu ya chama tawala, tusitegemee chama tawala kukubali kuvuja damu.

Hali ikiendelea hivi ni kwamba upinzani utapungua nguvu na wananchi watakosa imani na siasa za nchi hii kwa ujumla. CHADEMA iepukane na kundi la vijana ambao hawajitambui maana wengi si wapiga kura.

Kwa CCM kutoka madarakani ni nguvu toka nje ya Tanzania itatumika. Hadi sasa haiwezekani kufanyika hivyo kwa kuwa ccm wanakula vizuri na mabeberu rasilimali zetu.

CCM itatoka madarakani kwa mapinduzi. Na mambo yasipoenda vyema tutageuka sierra leone nyingine. Hakutatokea chama cha upinzani kitakachokuja kuwa na nguvu kama CHADEMA.

Mwisho, kama hayo hapo juu hayatatokea, na kama tunahitaji mbadala wa CCM, basi tuanze kuiamini kauli ya Nyerere. Tusubiri CCM imeguke. Hili halishindikani. Yangu macho
kama imefikia sisi wenyewe kuikataa Tanganyika yetu kinyume na wazanzibar wanaohakikisha jina lao la zanzibar halipotei na serikali yao haipotei tutawezaje kujikomboa
 
kama imefikia sisi wenyewe kuikataa Tanganyika yetu kinyume na wazanzibar wanaohakikisha jina lao la zanzibar halipotei na serikali yao haipotei tutawezaje kujikomboa

namsikiliza kingunge hapa tbc akizungumzia kwa machungu historia ya jina la kikoloni na la kidhalilishaji la Tanganyika. Nasa
hangaa pia zanzibar ilikuwa chini ya ukoloni na jina hilohilo. hoja ya kingunge ni nyepesi sana
 
Back
Top Bottom