Zee la kitaa
JF-Expert Member
- Oct 25, 2017
- 403
- 211
Katika hali ya kustahajabu; CHADEMA kimetoka katika msingi wake wa kuwa chama tumainiwa cha wananchi na kubaki chama cha maslahi ya watu fulani kutokana na misingi wa uendeshaji ulivyo kwa sasa.
Kumekuwa na matamko mbalimbali ya wanachadema inayotia shaka kuwa chama tumaini kutokana na maono ya kuanzishwa kwake.
Kwa hali ilivyo sasa inaonekana hakuna kuaminiana ndani ya CHADEMA na tumaini lililobaki ni Mhe. A. T. Lissu. Mhe. Mbowe uliulizwa swali kama Mhe. Lowassa alikupa taarifa ya kwenda Ikulu; ukajibu kisiasa.
Mhe. Lissu alihoji baada ya taarifa yako ya hivi majuzi kuhusu Lowassa kwenda Ikulu na maoni aliyoyatoa ni yake si msimamo wa chama; wengi walitaka kujua kama Mhe. Lowassa alikupa taarifa ya kwenda ikulu?
Jana ulipewa mrejesho wa safari ya Mhe. Lowassa kwenda ikulu; je matamko ya BAVICHA kulaani kitendo hicho yamekufa? Ukiona post za wanachadema mfano aliyoitoa Meya wa Ubungo utagundua hata Mhe. Mbowe haaminiki tena.
CHADEMA badala ya kujenga taasisi wanajenga na kumtukuza mtu. Ukijenga taasisi inasaidia kuimarisha watu kuliko kujenga watu.
Mhe. Mbowe jitahidi kurudi katika misingi ya kujenga taasisi mmepotea sana. Chadema hii hata viongozi wa umoja wa vijana wanakosa weredi wa kujenga hoja zenye mashiko. CHADEMA jengeni taasisi kuliko hali ilivyo sasa.
Kumekuwa na matamko mbalimbali ya wanachadema inayotia shaka kuwa chama tumaini kutokana na maono ya kuanzishwa kwake.
Kwa hali ilivyo sasa inaonekana hakuna kuaminiana ndani ya CHADEMA na tumaini lililobaki ni Mhe. A. T. Lissu. Mhe. Mbowe uliulizwa swali kama Mhe. Lowassa alikupa taarifa ya kwenda Ikulu; ukajibu kisiasa.
Mhe. Lissu alihoji baada ya taarifa yako ya hivi majuzi kuhusu Lowassa kwenda Ikulu na maoni aliyoyatoa ni yake si msimamo wa chama; wengi walitaka kujua kama Mhe. Lowassa alikupa taarifa ya kwenda ikulu?
Jana ulipewa mrejesho wa safari ya Mhe. Lowassa kwenda ikulu; je matamko ya BAVICHA kulaani kitendo hicho yamekufa? Ukiona post za wanachadema mfano aliyoitoa Meya wa Ubungo utagundua hata Mhe. Mbowe haaminiki tena.
CHADEMA badala ya kujenga taasisi wanajenga na kumtukuza mtu. Ukijenga taasisi inasaidia kuimarisha watu kuliko kujenga watu.
Mhe. Mbowe jitahidi kurudi katika misingi ya kujenga taasisi mmepotea sana. Chadema hii hata viongozi wa umoja wa vijana wanakosa weredi wa kujenga hoja zenye mashiko. CHADEMA jengeni taasisi kuliko hali ilivyo sasa.