Maoni yangu kuhusu muelekeo wa taifa letu

Maoni yangu kuhusu muelekeo wa taifa letu

ngosh

Member
Joined
Dec 18, 2014
Posts
48
Reaction score
40
Nimefuatilia majadiliano ya mwelekeo wa taifa letu kuhusu halisi kuwa tunakwenda wapi? Nikiwa mwananchi mzalendo napenda nitoe ya moyoni. Taifa letu, ukirejea Katiba yetu linafuata siasa ya ujamaa na kujitegemea, lakini katika utekelezaji tuko kwenye mfumo wa soko huria au ubepari. Mimi nashauri tujifunze kutokana ufanisi wa mifumo na kasi ya maendeleo kati ya nchi za Magharibi na Asia, hasa nchi ya china ambapo kasi ya China ni kubwa sana hivyo ningependa tuendelee na siasa ya ujamaa na tuige mfumo wa China katika kuendesha mambo yetu tutafanikiwa kupiga hatua ya maendeleo kwa haraka. Nakaribisha maoni yenu kuhusu muelekeo wa taifa letu.
 
Back
Top Bottom