Maoni yangu baada ya hitimisho la siasa za makonda!

Iruru

JF-Expert Member
Jan 27, 2014
1,471
2,891
Habari zenu waungwana!
Baada ya kushuhudia hitimisho la kile kilichoitwa upambananaji wa madawa ya kulevya, nmejikuta nikifikia hitimisho kama ifuatavyo:

Mosi, ukiisoma na kufuatilia yote yaliyotokea, utagundua kuwa makonda alikuwa na sababu mficho nyuma ya zoezi hili. Hoja hii inashibishwa na mambo kadha wa kadha, kwanza kutofuata utaratibu na sheria zilizopo ziwe zile za makosa ya jinai au zile ambazo zinahusu moja kwa moja hii biashara ya madawa ya kulevya. Pia hata wale waliokiri kutumia madawa ya kulevya pamoja na kukiri kiumbe yule kuwa adhabu yao ni miaka 3 jela, hawajapelekwa mahamani na kiunbe yule amewaachia huru na sijui ametumia mamlaka na sheria ipi!

Pili, baada ya zoezi hili, madawa na biashara yake itapanda charti sana, kumbuka imepata promo ya hali ya juu, makonda ameeleza jinsi hii biashara ilivyo na faida kubwa na vijana wengi hasa wasio na kazi wameambiwa njia mbadala ya kutoka kimaisha!

Tatu, zoezi limeonyesha chuki na ubaguzi wa hali ya juu, kumbuka, pamoja na kwamba kuna watu wengi wameshutumiwa ila sio wote waliotangazwa hadharani na sio wote pia waliofanikiwa kulazwa sero kama kamanda siro alivyojisifia; huu ni ubaguzi mkubwa, watu wana tuhuma sawa ila treatment tofauti!!!

Nne mwisho, hili zoezi liliwalenga watu baadhi na ukiangalia vizuri, lilimlenga mtu fulani. Halikuwa zoezi la kitaifa, lililenga watu Ana nyumba Ana maeneo fulani tu basi..

Hili nmeshindwa kuliacha, zoezi limeonyesha jinsi gani serikali na hasa vyombo vya dola vilivyo dhaifu, kumbuka njia kadha wa kadha alizoeelezea makonda kuwa madawa yanapitai, maeneo yote haya yana vikosi vya doria, kwa madawa kupita wakiwepo ni ishara kuwa huwa hawaifanyi kazi yao. Pia serikali ya magu imevuliwa nguo, wameonekana wakiwa tenge, raisi kule, baraza kule na vyombo vingine vya usalama vikiwa kule....

Kama nawe, melifuatilia, unaweza kuongeza yale uliyojifunza........
 
hakunaga bongo movie isiyo na makosa lukuki hii nayo ni movie tu kama za kanumba
 
Nimelifuatilia nimejifunza kuna viongozi wana "kisebusebu na kiroho upapo" hayo ndio maoni yangu
Uongozi ni hekima, busara na maarifa.
Uongozi uliopo sasa unakosa baadhi ya hayo mambo matatu ....

Ebu fikiria mtu anaenda kutoa pole kwenye msiba - badala ya pole anatukana watu ... iko wapi hekima, iko wapi busara ..?

Unamshuku mtu na kumtangaza waziwazi kana kwamba una uhakika na na shutuma hizo .. iko wapi hekima, iko wapi busara ...
 
Back
Top Bottom