Maoni ya Dr. Azaveli Lwaitama Juu ya Lowassa Kuingia UKAWA

Bukanga

JF-Expert Member
Dec 13, 2010
2,857
1,936
Historia inaonesha kuwa vipindi fulani katika mstakhabali wa nchi unalazimisha kupima nini ni janga zaidi ya jingine. Marehemu Samora Machel na Frelimo walikubali kutia saini Mkataba wa Nkomati wa ushirikiano na Makaburu kama mkakati wa kujinusuru na kutoa nafasi kukabiri janga kubwa kuliko zote wakati huo la kuondolewa serikali ya Frelimo na Renamo ikisaidiwa na Makaburu. Wakomunisti wa Afrika ya Kusini waliingia ubia na ANC ya mabweneyenye weusi ili kutokomeza kwanza ukaburu na mapambano na ubepari yaje baadaye. Katika Vita Kuu ya Dunia ya Pili wakomunisti walishirikiana na mabwenyenye wa mrengo wa kulia na kati kutokomeza janga kubwa zaidi wakati huo la ufashisti, yaani ubepari wa mrengo wa wa kulia kupitiliza. Hivyo hivyo mapambano ya kuleta uhuru wa Tanganyika yalivyo unganisha nguvu za mabwenyenye wazungu na waasia pamoja na zile za wakulima na wafanyakazi wa rangi zote kwa azimio lile la mkutano wa mkuu wa Tanu wa 1958 pale Tabora. Hivyo hivyo Mandela na ANC waliingia "urafiki wa mashaka" na De Clerk kiongozi wamakaburu ili kuondolewa ukaburu kuwe kwa amani ya "kula matapishi" ya kuwalaani huko nyuma kuwa ni wabaya wa Mwaafrika!!

Mabadiriko ya haraka haraka yanayoendelea hapa Tanzania yenye lengo la kuondoa CCM madarakani kama chama dola kinachodumaza na kudhoofisha ushindani wa kisiasa miongoni mwa mabwenyenye watabaka tawala Tanzania ni mbadiliko yatayoleta neema kwa Watanzania wote. Ile tu CCM kudhoofishwa na kujiunga UKAWA kwa Lowasa ni kuvuja kwa pakacha ambayo ni nafuu ya mchukuzi.....Nikuondoa kizingiti kikuu cha kushamiri kwa demokrasia pana na maendeleo endelevu Tanzania ambacho ni kuhodhiwa na ukiritimba wa chama dola cha CCM kinachojinadi kama chama cha mrengo wa kushoto wakati ni chama cha mrengo wa kulia kama vyama vyote vya siasa Tanzania kwa sasa.

Kumeguka kwa CCM-Mambo Leo kama taasisi ya kakundi kawana mtandao ulioingiza serikali ya sasa ya Tanzania madarakani mwaka 2005 ni faraja kwa wote wenye kuitakia mema nchi hii na ni kiashiria cha kukomaa kwa vuguvugu la ukombozi wa pili wa Tanzania utakao chukua sura ya demokrasia zaidi ilikuwa na na maendeleo endelevu zaidi yapatikane kupitia kupatikana nafasi chanya zaidi ya kupitishwa kwa Katiba Mpya kama ilivyopendekezwa ndani ya Rasimu ya Pili ya Tume ya Rais iliyoongozwa na Jaji Warioba. Kwa mara ya kwanza vyama vy siasa vya upinzani kiuhalisia ( tofauti na vile ambavyo vimebebwa na watawala wa sasa kwa lengo la kuua upinzani wa kisiasa kijanja kijanja kama ACT- Wazalendo) sasa vimeunganishwa na kupigania Katiba Mpya iliyotokana na maoni ya wananchi yaliyokusanywa na Tume ya Jaji Warioba ( UKAWA) badala ya kuunganishwa na kutaka kuondoa CCM madarakani pekee.

Ghafla mwanasiasa mwenye nguvu nyingi ndani ya chama cha kifisadi cha CCM, mwanasiasa ambaye umaaarufu wake umetokana na kuongoza mtandao uliouweka utawala wa sasa wa CCM madarakani, Ndugu Edward Lowasa, amekasirishwa na kukatwa jina lake na aliodhani ni rafiki zake ndani ya CCM na kuamua kusema basi na lolote liwe kwa kujiunga na vuguvugu la kupigania katiba mpya!! Naye sasa kang'amua kuwa Katiba ya sasa na ile Pendekezwa ni za ovyo maana haziruhusu kuwepo mgombea huru bila mizengwe. Hasira za Lowasa zimezaa tunda zuri la kug'amua kuwa Watanzania wanaitaji mabadailiko kupitia Katiba Mpya iliyobebwa ndani ya Rasimu ya Pili ya Tume ya Rais iliyoongozwa na Jaji Warioba. Hasira hizi za mkizi ni furaha ya kunguru na ni busara kwa viongozi wa Chadema na UKAWA kwa ujumla kutoongopa "kula matapishi yao" kwa kumkaribisha Ndugu Lowasa ...huyu huyu waliomwita fisadi... kujiunga na UKAWA na kugombea urais. Nafasi ya kihistoria imejitokeza ya kukiondoa CCM madarakani kwa amani!!

Sishangai wasaliti wa vuguvugu la kukiondoa CCM madarakani wanatushauri sisi Watanzania wenye shauku ya kuutumia upenyo huu wa mpasuko ndani ya CCM kukiondoa CCM madaraka!!!Eti tuombe radi kwa" kula matapishi yetu" wote tulio wahi kumwita Lowasa fisadi! Wao wanataka tuendelee kuvumilia kutawaliwa na CCM labda kwa miaka mitano au zaidi hivi mpaka chama kipya cha watakatifu kiitwacho ACT-Wazalendo kitakapo kuwa tayari kututawala badala ya CCM!! Sishangai kusikia ushauri huu kutoka kwa wasaliti hawa ambao kazi yao hata huko nyuma imekuwa nikuudhoofisha upinzani dhidi ya CCM na kukisaidia CCM kiendeleee kuwa madarakani!! Hawa jamaa ni wasomi sana na ni wajanja sana, ilo lazima kulikiri!!!

Sitashanga kama haya ninayoyasema yatapigwa madogo na wasaliti hawa!! Historia itakapoandikwa baada ya UKAWA kupata viti vingi zaidi Bunge lijalo au hata kuuchua urais na kupata Katiba Mpya iliyobebwa ndani ya Rasimu ya Pili ya Tume ya Rais iliyoongozwa na Jaji Warioba itawapa hukumu yao stahiki, wajanja na welevu hawa! Bila shaka wanaoomba UKAWA ishindwe kupata viti vingi Bunge lijalo na iukose urais na hivyo tuendelee kutawaliwa na CCM na wao wapate viti vya kutosha kuwa viongozi wakuu wa eti upinzani muruwa wenye maadili ya Azimio la Arusha Tanzania!! Ni haki yao ya binadamu kuendelea na matumaini haya kama na sisi tulivyo na haki ya kuendelea na matumani yetu ya uwezakano wa ushindi mnono chini ya UKAWA dhidi ya ukiritimba wa chama kimoja chama dola cha CCM!
Mwl. Lwaitama

Culled from Wanabidii..

Cc Mchambuzi Mzee Mwanakijiji Character X Mag3 Matola Ritz Lizaboni

 
ccm haijameguka akili zako ndio zimemeguka kwa kuona lowasa kajivua gamba kwa ufisadi sasa ccm imebaki cream safi kama imezaliwa leo safi kabisa ccm

usafi gani huo mkuu mlio nao ccm?

watoeni na weziwa EPA,KAGODA,MELEMETA,ESCROW na wezi wengine ambao hawajulikani mbele ya umma.

watoeni na hawa wanaokamatwa na takukuru wakitoa rushwa kwenye kura za maoni. naibu waziri,nape chambiri

hivi hata escrow aliyeiba alikuwa lowasa?

chenge,tiba,mnikulu,ngeleja, na wale wa stanibic

nani msafi ndani ya ccm?
 
Huyu
Mzee apewe kabisa uwaziri wa elimu

Muulizeni kama alishafuta namba ya simu ya Diallo. Kalivyopigwa mtama baada ya kufanya fujo kwenye ndege mbona kaliwapigia simu ccm haohao waje kukawekea dhamana?

Anasubiri wagombee wengine wapige kura wengine yeye aje kuukwaa uwaziri for free? mwambieni vyeo chadema vinauzwa hawagawi bure.
 
Asante sana Mzee Lwaitama kwa kututia moyo. Inabidi kutafuta less evil!
 
usafi gani huo mkuu mlio nao ccm?

watoeni na weziwa EPA,KAGODA,MELEMETA,ESCROW na wezi wengine ambao hawajulikani mbele ya umma.

watoeni na hawa wanaokamatwa na takukuru wakitoa rushwa kwenye kura za maoni. naibu waziri,nape chambiri

hivi hata escrow aliyeiba alikuwa lowasa?

chenge,tiba,mnikulu,ngeleja, na wale wa stanibic

nani msafi ndani ya ccm?

hao wote ni team lowasa, JP akichukua dola lazima wapande kisutu, EL anaomba siasa za kistaarabu mwambieni hazipo, mafisadi yote lazima yaende segerea.
 
this man stayed true since day one..sio yule profesa aliyeudhalilisha usomi wake(shivji).,najiuliza kama yupo nchi hii au yupo mumbai!!!!!akiongea sasa hivi hata mlevi hamsikilizi.
 
Mzee umemaliza tunasubiri kuapishwa

Jamaa kaandika vizuri sana, hamana mahali upinzani pure umewahi kuchukua madaraka kwa amani pasipo kwanza kupasu chama tawala! Ccm wanajua sasa hivi ngoma ni nzito walitarajia wapinzani watendelea kuimba ufisadi tu wakisubiri mtakatifu aingie ikulu! Mungu hafanyi kazi yake kama wanadamu wanavyo fikiri ni lazima jambo la Mungu liwashangaze wanadamu na ndivyo hata hili limewashangaza maana kwa akili za kibinadamu likikuwa haliwezekani! Yasiyowezekana kwa wanadamu kwa Mungu yote yanawezekana! Kama walidhani walipokuwa wanasema nibmpango wa Mungu walidhani Mungu atajibu kama wanadamu! God has proven that He is the only Him!
 
hao wote ni team lowasa, JP akichukua dola lazima wapande kisutu, EL anaomba siasa za kistaarabu mwambieni hazipo, mafisadi yote lazima yaende segerea.

anza na mwizi wa nyumba za serikali magufuli mchukua 10% kwa wakandarasi halafu mjumlishe baba mwanaasha(richmond+escrow) kisha funga kazi kwa mkapa(kiwira,nbc,mikataba ya madini).
 
Mpaka mwisho mwa wiki ijayo tutajuwa ukweli kutoka kwa wanataaluma na wanaharakati.Na huo ndio utakuwa mwongozo kwa watanzania wengi kuelekea kupata uhuru wa kiuchumi.
 
Back
Top Bottom