benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,035
Uteuzi wa viongozi watano wakiwemo wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) uliofanywa jana na Rais Samia Suluhu Hassan, umewaibua wadau mbalimbali wa kia-siasa baadhi wakipongeza na wengine wakidai hauna tija kwa kuwa wamerudishwa watu walewale.
Jana Rais Samia alimteua Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani, Mbarouk Salim Mbarouk kuwa makamu mwenyekiti wa NEC kwa kwa kipindi cha pili. Vilevile, katika uteuzi huo alimteua tena Balozi Omary Ramadhan Mapuri kuwa mjumbe wa tume hiyo kwa kipindi cha pili huku akimteua Dk Zakia Mohamed Abubakar kuwa mjumbe wa Tume hiyo.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, uteuzi wa wajumbe hao unaanza kesho Julai mosi. Pamoia na hao pia alimteua aliyekuwa Naibu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Benjamin Magai kuwa Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali. Pia Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali
(TGFA), Profesa Idrissa Mshoro naye aliteuliwa kwa kipindi cha pili.
Wapongeza, wakosoa
Baada ya uteuzi huo, wadau mbalimbali walitoa maoni tofauti baadhi wakipongeza na wengine wakidai hauna tija kwa kuwarudisha watu walewale waliokuwa wajumbe wa Tume ilivonyooshewa kidole kwa namn a ilivyoendesha uchaguzi uliopita.
Hata hivyo, Profesa Mohammed Makame Haji wa Zanzibar alisema anaamini watu walioteuliwa wanaweza kufanya kazi inayotakiwa kwa kutenda haki kwa kuzingatia misingi ya kisheria muda wote.
"Jaji Mbarouk ni mzoefu amekuwa akisimamia shughuli za kisheria kwa muda mrefu na amekuwa akipanda ngazi kwa hatua, tangu alipoanza hadi kuwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, hii imethibitisha uwezo aliokuwa nao," alisema.
Alimwelezea Balozi Mapuri kuwa ni mtu mwenye uzoefu wa kutosha hasa mabadiliko historia na mwelewa katika ugha wa kidiplomasia, akiwa ametumikia nafasi nyingi za kisiasa kwa upande wa Zanzibar na Tanzania Bara.
"Kwa nafasi yake katika Tume anaweza kuwa na mchango mkubwa katika kusimamia kwa kuwa amebobea katika maeneo hayo, alisema. Kuhusu Dk Zakia, Profesa Haji alisema naye ni mtu aliyetumikia nafasi mbalimbali na mara mwisho alikuwa makamu mkuu wa Chuo Kikuu Zan-zibar, na kwa kuwa nafasi hiyo inahitaji watu wenye maono, inamfaa kuwatumikia Watanzania.
"Uwepo wao utasaidia kwa kuwa wote hao wana uwezo wa kusoma mabadiliko ya jamii inayohusi-ka lakini ni watu wanaojua mabadiliko mbalimbali ya siasa zetu kwa kuzingatia mahitaji yetu,"alisema Profesa Haji.
Wakati msomi huyo akisema hivyo, Mkurugenzi Mtendaii wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Bob Wangwe alikuwa na mtazamo tofauti akisema uteuzi huo unamsikitisha kwa kuwa umewarudisha watendaji walewale ambao katika uchaguzi mkuu uliopita walikuwa wananyoshewa kidole kwa kuuharibu.
"Hali hivo inaonyesha Rais alifurahia kilichotokea katika uchaguzi uliopita, binafsi nilikuwa nategemea yafanyike mabadiliko makubwa ya watendaji kwa kuingiza wapya ili kurejesha nidhamu na weledi na kuwaaminisha Watanzania kuhusu mwenendo wa uchaguzi ujao," alisema Wangwe. Hi ni mara ya pili mjadala wa kisiasa kama huo kuibuka kuhusu uteuzi wa ama watendaji au wajumbe wa NEC, baada ya kufanywa na Rais Samia.
Februari 26, 2023 Rais Samia alimteua Ramadhan Kailima kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, akichukua nafasi ya Dk Wilson Mahera aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu Tamisemi. Kabla ya Dk Mahera, nafasi hivo iliwahi kushikwa na Dk Athumani Kihamia ambaye alichukua wadhifa huo Julai 2018 kutoka kwa Kailima aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu.
Chanzo: Mwananchi
Jana Rais Samia alimteua Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani, Mbarouk Salim Mbarouk kuwa makamu mwenyekiti wa NEC kwa kwa kipindi cha pili. Vilevile, katika uteuzi huo alimteua tena Balozi Omary Ramadhan Mapuri kuwa mjumbe wa tume hiyo kwa kipindi cha pili huku akimteua Dk Zakia Mohamed Abubakar kuwa mjumbe wa Tume hiyo.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, uteuzi wa wajumbe hao unaanza kesho Julai mosi. Pamoia na hao pia alimteua aliyekuwa Naibu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Benjamin Magai kuwa Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali. Pia Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali
(TGFA), Profesa Idrissa Mshoro naye aliteuliwa kwa kipindi cha pili.
Wapongeza, wakosoa
Baada ya uteuzi huo, wadau mbalimbali walitoa maoni tofauti baadhi wakipongeza na wengine wakidai hauna tija kwa kuwarudisha watu walewale waliokuwa wajumbe wa Tume ilivonyooshewa kidole kwa namn a ilivyoendesha uchaguzi uliopita.
Hata hivyo, Profesa Mohammed Makame Haji wa Zanzibar alisema anaamini watu walioteuliwa wanaweza kufanya kazi inayotakiwa kwa kutenda haki kwa kuzingatia misingi ya kisheria muda wote.
"Jaji Mbarouk ni mzoefu amekuwa akisimamia shughuli za kisheria kwa muda mrefu na amekuwa akipanda ngazi kwa hatua, tangu alipoanza hadi kuwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, hii imethibitisha uwezo aliokuwa nao," alisema.
Alimwelezea Balozi Mapuri kuwa ni mtu mwenye uzoefu wa kutosha hasa mabadiliko historia na mwelewa katika ugha wa kidiplomasia, akiwa ametumikia nafasi nyingi za kisiasa kwa upande wa Zanzibar na Tanzania Bara.
"Kwa nafasi yake katika Tume anaweza kuwa na mchango mkubwa katika kusimamia kwa kuwa amebobea katika maeneo hayo, alisema. Kuhusu Dk Zakia, Profesa Haji alisema naye ni mtu aliyetumikia nafasi mbalimbali na mara mwisho alikuwa makamu mkuu wa Chuo Kikuu Zan-zibar, na kwa kuwa nafasi hiyo inahitaji watu wenye maono, inamfaa kuwatumikia Watanzania.
"Uwepo wao utasaidia kwa kuwa wote hao wana uwezo wa kusoma mabadiliko ya jamii inayohusi-ka lakini ni watu wanaojua mabadiliko mbalimbali ya siasa zetu kwa kuzingatia mahitaji yetu,"alisema Profesa Haji.
Wakati msomi huyo akisema hivyo, Mkurugenzi Mtendaii wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Bob Wangwe alikuwa na mtazamo tofauti akisema uteuzi huo unamsikitisha kwa kuwa umewarudisha watendaji walewale ambao katika uchaguzi mkuu uliopita walikuwa wananyoshewa kidole kwa kuuharibu.
"Hali hivo inaonyesha Rais alifurahia kilichotokea katika uchaguzi uliopita, binafsi nilikuwa nategemea yafanyike mabadiliko makubwa ya watendaji kwa kuingiza wapya ili kurejesha nidhamu na weledi na kuwaaminisha Watanzania kuhusu mwenendo wa uchaguzi ujao," alisema Wangwe. Hi ni mara ya pili mjadala wa kisiasa kama huo kuibuka kuhusu uteuzi wa ama watendaji au wajumbe wa NEC, baada ya kufanywa na Rais Samia.
Februari 26, 2023 Rais Samia alimteua Ramadhan Kailima kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, akichukua nafasi ya Dk Wilson Mahera aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu Tamisemi. Kabla ya Dk Mahera, nafasi hivo iliwahi kushikwa na Dk Athumani Kihamia ambaye alichukua wadhifa huo Julai 2018 kutoka kwa Kailima aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu.
Chanzo: Mwananchi